Utume wa viongozi wa kidini na 'siasa'

Kibunago

JF-Expert Member
Jan 11, 2008
300
122
Kwamba Maaskofu hawapaswi kuongelea mambo yanayohusu siasa au viongozi wa kisiasa ni ufinyu wa mawazo na kutokujua hakika utume wa viongozi wa kidini na hata historia yake.

Mtume Mohammed (SA) alihubiri juu ya Mola Mmoja & Haki na Wakureshi (Quarash) na Viongozi wao waliokuwa wanafahidika na mfumo huo mbovu hawakumpenda kwa kuona kuwa anawaingilia. Hii ikasababibsha hadi kumfukuza Mtume toka Macca akaishi na familia yake ukimbizini katika milima ya Sho’be Abu Talibu. Kudai & kutenda haki ni kusudi mojawapo kuu la dini Islam. Mungu hutuamuru kutenda haki (Quran 16:90), Hakika Wanaohubiri ni Mitume wa kujenga Haki miongoni mwa jamii. “We sent Our Messengers with clear signs and sent down with them the Book and the Measure in order to establish justice among the people…” (Quran 57:25).

Kwamba, kwa ajili ya yenu (Wakristo) wamepewa, Yesu ambaye ni Mshauri wa ajabu na pia Bwana wa Amani (Isaya 9:6). Na hakika Mitume na Manabii wengi sana akina Hosea, Hagai, Amos, Isaya, Paulo nk walisimamia haki na kuisema kweli popote hata dhidi ya Watawala. Yohana Mbatizaji alitupwa gerezani na hata baadaye kukatwa kichwa zawadi iliyoombwa na mama Herodia kupitia binti wake kwa sababu alionekana mwiba juu ya ndoa batiri ya Herode Antipas. Isaya msahauri wa Wafalme kufuatana na masimulizi ya mapokeo ya Wayahudi, aliuawa wakati wa utawala wa mfalme mwovu Manase kwa njia ya kukatwa vipande viwili kwa msumeno (taz.Ebr 11:37).

Kama kuisema na kuitetea KWELI na kuonya juu ya MAOVU au KUTOTENDWA KWA HAKI mahala fulani ndiko kunaitwa kuingia katika Siasa au kuingilia Wanasiasa, basi hata Waasisi wa dini hizo na nyinginezo kama vile Yesu Kristo, Mtume Mohammed (SA) na karibu Mitume na Manabii wote walikuwa Wanasiasa!

Hebu pata Facts:



  • Ni wajibu wao Maaskofu kama sehemu ya jamii (Civil Society) na pia kama Viongozi wanaohubiri na kusimamia haki (bila jeshi) ya Waasisi wao, Maaskofu kulaani na kutoa pole kwa mauaji yaliyotekea Arusha hivi karibuni.

  • Hao Maaskofu walioongea ni sehemu ndogo sana ya Maaskofu au tuseme Viongozi wa Madhehebu ya Kikristo Tanzania. Kuna Madhehebu kibao ambayo hayako chini ya TEC wala CCT. Na hata leo tungepitisha survey najua wako wengi tu (hata ndani ya TEC & CCT) ambao wangepinga au kubeza au kulaani walichokifanya hao Maaskofu! Na ndivyo ilivyotokea hata wakati wa Mauaji ya Mwembe-Chai, si wote walikaa kimya au sema si wote walilaani mauaji yale! Ni uzembe wa kufikiri kulaani dini yote ya Kikristo au Kiislam kwa wachache kuwa kimya au wachache kuongea.

  • Suala la Maaskofu kutomtambua Meya wa Arusha lina mitamo miwili:
i. kwa wale wanaounga mkono Utume wa kuikabiri kweli kwa nguvu zote hata kama inauma (the mission of confronting the truth) watakubaliana nami kuwa haki inapopindishwa haitakiwi kumungúnya maneno au kutafuta misamiati ya kulemba. Kama ukweli unajulikana kwa uchaguzi hakufanyika katika mazingira ya haki na huru na kwamba mujibu wa namba ya Madiwani toka CHADEMA Kuwa hata kesho kura ikiitishwa na kusimamiwa kwa haki; huyo Meya aliyepo sasa hatashinda; basi asiyemun’gunya maneno atasema kuwa huyo hatumtambui maana tunajua mazingira ambayo kwayo alipatikana.

ii. Kwa wale wasiounga mkono Utume wa kuikabiri kweli kwa nguvu zote, yaani ni wale ambao watapenda kuliita koleo, kijiko kikubwa wangependa Maaskofu waseme tu kuwa ‘Kuna mgogoro katika Manispaa ya Arusha uliotokana na uchaguzi wa meya na hivyo vyombo husika vilisimamie jambo hilo pasi kupoteza muda. Mtizamo wao huwa ni kujaribu kuepuka kuamsha hisia na hasira za watu na hatimaye kuibuka kwa migogoro katika jamii; (ingawa ukweli unaweza kuwa ukazuia mgogoro kwa muda mfupi lakini baadaye hata baada ya miaka kukazuka migogoro mikubwa zaidi ya visasi ambayo chanzo chake ni ‘Utume wa kuepuka mgogoro’ wa leo!). Aidha pia kundi hili laweza kuwa ni wale pia wanaoona kuwa Maaskofu hawana kazi ya kuwatambua au kutowatambua Viongozi waliochaguliwa bali Tume za Chaguzi na au Mahakama.

Popote unapoosimamia kuhusu hili, binafsi nasema kuwa Maaskofu walivyotamka kuhusu Meya, ni maoni yao katika uchache / wingi wao baada ya uchambuzi wao. Sasa chombo kinachohusika kiteremke Arusha kiitishe uchaguzi huo halafu tuone matokeo yake na watakao chaguliwa wawe Meya na Msaidiazi wake! Na hapo turudi katika jukwaa hili katika mada hii ili tukamilishe hitimisho.
 
Kwamba Maaskofu hawapaswi kuongelea mambo yanayohusu siasa au viongozi wa kisiasa ni ufinyu wa mawazo na kutokujua hakika utume wa viongozi wa kidini na hata historia yake.

Mtume Mohammed (SA) alihubiri juu ya Mola Mmoja & Haki na Wakureshi (Quarash) na Viongozi wao waliokuwa wanafahidika na mfumo huo mbovu hawakumpenda kwa kuona kuwa anawaingilia. Hii ikasababibsha hadi kumfukuza Mtume toka Macca akaishi na familia yake ukimbizini katika milima ya Sho'be Abu Talibu. Kudai & kutenda haki ni kusudi mojawapo kuu la dini Islam. Mungu hutuamuru kutenda haki (Quran 16:90), Hakika Wanaohubiri ni Mitume wa kujenga Haki miongoni mwa jamii. "We sent Our Messengers with clear signs and sent down with them the Book and the Measure in order to establish justice among the people…" (Quran 57:25).

Kwamba, kwa ajili ya yenu (Wakristo) wamepewa, Yesu ambaye ni Mshauri wa ajabu na pia Bwana wa Amani (Isaya 9:6). Na hakika Mitume na Manabii wengi sana akina Hosea, Hagai, Amos, Isaya, Paulo nk walisimamia haki na kuisema kweli popote hata dhidi ya Watawala. Yohana Mbatizaji alitupwa gerezani na hata baadaye kukatwa kichwa zawadi iliyoombwa na mama Herodia kupitia binti wake kwa sababu alionekana mwiba juu ya ndoa batiri ya Herode Antipas. Isaya msahauri wa Wafalme kufuatana na masimulizi ya mapokeo ya Wayahudi, aliuawa wakati wa utawala wa mfalme mwovu Manase kwa njia ya kukatwa vipande viwili kwa msumeno (taz.Ebr 11:37).

Kama kuisema na kuitetea KWELI na kuonya juu ya MAOVU au KUTOTENDWA KWA HAKI mahala fulani ndiko kunaitwa kuingia katika Siasa au kuingilia Wanasiasa, basi hata Waasisi wa dini hizo na nyinginezo kama vile Yesu Kristo, Mtume Mohammed (SA) na karibu Mitume na Manabii wote walikuwa Wanasiasa!

Hebu pata Facts:




  • Ni wajibu wao Maaskofu kama sehemu ya jamii (Civil Society) na pia kama Viongozi wanaohubiri na kusimamia haki (bila jeshi) ya Waasisi wao, Maaskofu kulaani na kutoa pole kwa mauaji yaliyotekea Arusha hivi karibuni.



  • Hao Maaskofu walioongea ni sehemu ndogo sana ya Maaskofu au tuseme Viongozi wa Madhehebu ya Kikristo Tanzania. Kuna Madhehebu kibao ambayo hayako chini ya TEC wala CCT. Na hata leo tungepitisha survey najua wako wengi tu (hata ndani ya TEC & CCT) ambao wangepinga au kubeza au kulaani walichokifanya hao Maaskofu! Na ndivyo ilivyotokea hata wakati wa Mauaji ya Mwembe-Chai, si wote walikaa kimya au sema si wote walilaani mauaji yale! Ni uzembe wa kufikiri kulaani dini yote ya Kikristo au Kiislam kwa wachache kuwa kimya au wachache kuongea.



  • Suala la Maaskofu kutomtambua Meya wa Arusha lina mitamo miwili:

i. kwa wale wanaounga mkono Utume wa kuikabiri kweli kwa nguvu zote hata kama inauma (the mission of confronting the truth) watakubaliana nami kuwa haki inapopindishwa haitakiwi kumungúnya maneno au kutafuta misamiati ya kulemba. Kama ukweli unajulikana kwa uchaguzi hakufanyika katika mazingira ya haki na huru na kwamba mujibu wa namba ya Madiwani toka CHADEMA Kuwa hata kesho kura ikiitishwa na kusimamiwa kwa haki; huyo Meya aliyepo sasa hatashinda; basi asiyemun'gunya maneno atasema kuwa huyo hatumtambui maana tunajua mazingira ambayo kwayo alipatikana.

ii. Kwa wale wasiounga mkono Utume wa kuikabiri kweli kwa nguvu zote, yaani ni wale ambao watapenda kuliita koleo, kijiko kikubwa wangependa Maaskofu waseme tu kuwa 'Kuna mgogoro katika Manispaa ya Arusha uliotokana na uchaguzi wa meya na hivyo vyombo husika vilisimamie jambo hilo pasi kupoteza muda. Mtizamo wao huwa ni kujaribu kuepuka kuamsha hisia na hasira za watu na hatimaye kuibuka kwa migogoro katika jamii; (ingawa ukweli unaweza kuwa ukazuia mgogoro kwa muda mfupi lakini baadaye hata baada ya miaka kukazuka migogoro mikubwa zaidi ya visasi ambayo chanzo chake ni ‘Utume wa kuepuka mgogoro' wa leo!). Aidha pia kundi hili laweza kuwa ni wale pia wanaoona kuwa Maaskofu hawana kazi ya kuwatambua au kutowatambua Viongozi waliochaguliwa bali Tume za Chaguzi na au Mahakama.

Popote unapoosimamia kuhusu hili, binafsi nasema kuwa Maaskofu walivyotamka kuhusu Meya, ni maoni yao katika uchache / wingi wao baada ya uchambuzi wao. Sasa chombo kinachohusika kiteremke Arusha kiitishe uchaguzi huo halafu tuone matokeo yake na watakao chaguliwa wawe Meya na Msaidiazi wake! Na hapo turudi katika jukwaa hili katika mada hii ili tukamilishe hitimisho.
Excellent from Kibunago!
Kwa mara yangu ya kwanza kusoma maandishi yako yanayohusu siasa, nimekuwa baffled na content hii!
CCM wanajua kupindisha kila neno linalowakandamiza na kuwakosoa!
 
Brevo! Hii message ingepaswa imfikie huyo mama na a confirm kwamba kaisoma na kupima kisha aamue
 
Mkuu Kibunango usemayo ni kweli kabisa ni nikusifu kwa kutotaka kujiegemeza na upande wowotn japokuwa una upande unaoamini kuwa uko sahihi. Kwa mtazamo wangu suala la Arusha lilikuwa ni dogo sana kama wadau wangejipa shida ya kuepuka jazba.... Machozi yananidondoka. Ntarejea baadaye
 
Yusuph kila maji yakimfika shingoni anakimbilia mistari ya Biblia tena ni ile mistari ambayo kwa ufinyu wake anaiona kama hirizi yake lakini mashehe na maaskofu wanapo kemea ufisadi wanawekewa mkwala eti kavaeni jezi mje majukwaani hivi kweli maaskofu na mashehe wapande majukwaani kuuvua nguo ufisadi hawa makamba$company watabaki?
 
VIONGOZI WA CCM WALISEMA SIASA NA DINI HAZIENDANI NA MARA YA KWANZA WALIMUZUIA KAKOBE MWAKA 2000 LAKINI KAWASHINDA KWENYE KITIMOTO PALE KILIMANJARO HOTEL.
UKWELI NI KWAMBA, DAUDI ALIKUWA MFALME (RAIS) WAKATI HUOHUO NI MTUMISHI WA BWANA (ZAIDI YA ASKOFU) PIA ALIONGOZA VITA NA MAPAMBANO MENGI YA KIJESHI NA SIASA.
MFALME SULEIMAN ALIKUWA kIONGOZI WA SERIKALI HUKU ANAFANYA KAZI YA MUNGU. wAPO WENGI , KAMA YOSHUA ALIYE watuma wapelelezi kaanani na ndiye aliye unda massadi shirika la ujasusi la ISRAELI MPAKA SASA


MAKAMBA ANATAKA VIONGOZI WA DINI WASISHIRIKI SIASA ILIAENDELEE KUIBA NA AKINA ROSTAM
 
Nionavyo mimi, siasa na dini vitu vinavyomhudumia mwanadam kwa pamoja ktk mazingira tofauti tofauti. Viongozi wa dini wawafundishe(kuwaasa) watu juu ya umuhimu wa kuwa waadilifu bila kujiingiza kwenye migogoro ambayo imejitokeza. Naamini hata viongoz uliowataja walijua mipaka ya watu wanaowatawala kwa wakati(kiserikali au kidini) hapa unataka kutuambia kuwa viongozi wa dini? Kumbuka viongoz wa dini wanatawala sehemu ndogo ya watu na hawana mamlaka ya kumwamuru mtu cha kufanya zaidi ya kumshauri. Na ndio maana mtu anaweza kuhama dini moja kwenda nyingine atakavyo na sio kiongozi wa serkl moja kwenda kuitawala nyingine. Pia ktk dini kanuni na taratibu za dini moja zinatofautiana na dini nyingine. Mathalani JK atakapoamua kuoa wake zaidi ya mmoja itakuwaje wakati sheria inatambua kuwepo kwa mke mmoja wa rais (FIRST LADY). Je sheria hii ilitungwa kuzingatia upande upi? Akifanya hivyo maaskofu ndio watakao kuwa wa kwanza kulalamika. Malalamiko ya upande wa viongozi wa dini lazma yatiliwe shaka na upande wa pili. Mfumo mbaya tuliojengewa. Tufumue. Nawasilisha hoja. Ahsante.
 
Back
Top Bottom