Utoto bwana!!

Tuliambiwa na kaka yetu kuwa ukitaja nyoka usipotema mate na kusema "Mungu pishia mbali sio mimi niliyesema ni mchawi" nyoka atatokea na kukung'ata. Basi kaka yetu mkubwa akawa anatutesa kweli mimi na mdogo wangu. Anakuja mbele yetu na kusema nyoka, nyoka, nyoka mara nyingi tu. Sisi kwa ajili ya imani kuwa nyoka atatokea tulikuwa tukitema mate na kusema hayo maneno hapo juu. Kwa kila mtajo mmoja wa nyoka tulikuwa tukitema mate na kusema hayo maneno. Basi kaka yetu anaweza kutamka hilo neno mfululizo hata mara 50. Tulitema mate hadi yanakauka mwisho tunalia na kumkimbilia mama tukidai kaka anatuchokoza, anataka nyoka waje. Utoto jamani! Lakini natamani nirudie utoto mie!

Nyinyi nanyi mlizidisha!!!!LOL!!!!
 
NA HII: Ukiota vibaka vyeupe kwenye kucha, ni ishara utapata utajiri wa ng'ombe 100 kwa kila kibaka!! :lol
 
ukimchungulia mtu anajisaidia mama yako anakatika titi.
nilikua nikimwona mtoto wa punda mbiooo..
kwenda kuoga kisimani then tunacheza mpaka giza then ha2ogi, kipigo cha hapo usisme...
 
halafu kuna ile michezo ya kibabababa na kimama..... me nilikuwa napenda kuwa baba.......
 
ukimruka aliyekaa au kulala bac yule uliyemruka atakua mfupi.

Bwana wee, mtu akikuruka unadai akuruke tena kurudi upande wa pili ili ku-counterbalance effect ya kuwa mfupi! Sijui kwa nini hatukifikiri akikuruka mara mbili utakuwa mfupi hata zaidi!
 
ukimchungulia mtu anajisaidia mama yako anakatika titi.
nilikua nikimwona mtoto wa punda mbiooo..
kwenda kuoga kisimani then tunacheza mpaka giza then ha2ogi, kipigo cha hapo usisme...

hahaha!!
Hiyo ya kukataa kuoga watu karibu wote tumepitia...
Sijui shida ninini!
 
hahaha!!
Hiyo ya kukataa kuoga watu karibu wote tumepitia...
Sijui shida ninini!
enzi hizo hakuna shida,kila christmass lazima ulilie nguo mpya...dah!sasa ivi majukumu nyomi na mimi naliliwa nguo na Evergreen "the boss"kumbe ndo maana Jd aliimba nataman kuwa kama mtoto,aliona mbali sana.
 
enzi hizo hakuna shida,kila christmass lazima ulilie nguo mpya...dah!sasa ivi majukumu nyomi na mimi naliliwa nguo na Evergreen "the boss"kumbe ndo maana Jd aliimba nataman kuwa kama mtoto,aliona mbali sana.

Hahahahahaaaaaaaaaaaaaa....lakini utoto ndio haurudi ng'o!!!!
 
Ukikalia Kinu utaota majipu kwenye masaburi... duuh wakubwa zetu walikuwa na mbinu za ajabu za kukukataza usifanye jambo.. Maana tulikuwa tunatahadharishana wenyewe kwa wenyewe
 
Nilishindwa kuvaa suruali, ilibidi dada yangu anivue suruali akimbie nyumbani kunichukulia kaptura safari ya kwenda kanisani iendelee, utoto bwana we acha tu, natamani kurudia utoto lakini ndo ishatoka hiyo.

hahahaaa. Wewe na dada yako wote nouma. Kwa hiyo ulibaki uchi barabarani?
 
Ya kuoga balaa. Sisi tulikuwa tunaenda bafuni, unanawa miguu mwisho magotini, mikono, kichwani unarashia maji ili mama ajue tumeshaoga. Siku nyingine si mama anashtukia unakaguliwa. Bas anafunua nguo hadi mapajan anakuta kuanzia gotin kwenda juu umechafuka vumbi ukizingtia umetoka kucheza rede. Hapo fimbo itakuhusu.
 
ukikalia kinu au mafiga huzai..... Mmenikumbusa mbal sana lakin watoto wa cku hiz wala hawainjoy maisha!
 
Ukitukana mtu mdomo utapinda, basi siku moja tukakutana na mtu mdomo wake umekaa upande mama akaniambia ''shauri zako we endelea kutukana tu!'' nikakoma hadi leo. Ukichapwa kwa mwiko je nani anakumbuka ishara yake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom