Mwenyekiti ni salama ahmed, kuna el mamry, na Nasoro khamis. Sekretariati ni andrew,fadhila, othman na wengineo. Mwenyekiti anatoa ufafanuzi wa kazi zao. Anaelezea mchakato ulivyoanza mpaka sasa. Anaeleza kwamba kila mtu yuko huru kutoa maoni kwani analindwa na sheria
Madaraka ya rais kila anayekuja analizungumzia kuhusu kupunguzwa. Kila mwananchi amekerwa na namna jk alivyozitumia weakness za katiba hii kunufaisha familia na rafiki zake
Aisee, nimegundua wananchi wanajua vitu vingi kuliko inavyodhaniwa. Wanafunguka kama kuna mtu kawakaririsha. Kuna oni la viongozi washitakiwe baada ya kutoka madarakani. Pia yoyote anayetoa ahadi za uongo wakati wa kampeni washtakiwe ili watu wasiwe wanaongea uongo hadharani. Mwenge, mwenge jamani! Wananchi wamechoka nao na uzinzi unaofanyika. Watu wanataka uwekwe museums
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.