Nicky82
JF-Expert Member
- Mar 14, 2009
- 941
- 64
Wengi watakubaliana na mimi kuwa biashara ya mavazi ni moja kati ya biashara isiyopitwa na wakatati, ni kama vile ilivyo biashara ya vyakula, kwani mtu atahitaji kula na kuvaa kila siku.
Linalonitatiza kwa sasa ni utitiri huu wa mitumba ya nguo ulionea kila kona ya nchi hii, na utamaduni unaozidi kujengeka wa watanzania kupenda kuvaa nguo za mitumba,viatu,n.k. Kuna wakati nahisi kuwa ni kama nchi yetu imegeuzwa dampo la wenzetu kutupia vitu used. Sina lengo la kuwakejeli wale wanaovaa mavazi hayo kwani hata mimi nilivaa wakati huo.
Swali mbalo najiuliza ni kuwa tumeshindwa kuendeleza viwanda vyetu vya ndani, au pamba haipatikani, au ni utamaduni wetu wa kupenda vya 'nje' au Watz wengi hawana uwezo wa kununua nguo mpya??
Sijasikia kwenye kampeni vyama vikiongelea hili la kufufua/kuimarisha viwanda vya nguo vya ndani, ni kwamba tumeridhika nalo au ni yaleyale ya liache bora liende.
Linalonitatiza kwa sasa ni utitiri huu wa mitumba ya nguo ulionea kila kona ya nchi hii, na utamaduni unaozidi kujengeka wa watanzania kupenda kuvaa nguo za mitumba,viatu,n.k. Kuna wakati nahisi kuwa ni kama nchi yetu imegeuzwa dampo la wenzetu kutupia vitu used. Sina lengo la kuwakejeli wale wanaovaa mavazi hayo kwani hata mimi nilivaa wakati huo.
Swali mbalo najiuliza ni kuwa tumeshindwa kuendeleza viwanda vyetu vya ndani, au pamba haipatikani, au ni utamaduni wetu wa kupenda vya 'nje' au Watz wengi hawana uwezo wa kununua nguo mpya??
Sijasikia kwenye kampeni vyama vikiongelea hili la kufufua/kuimarisha viwanda vya nguo vya ndani, ni kwamba tumeridhika nalo au ni yaleyale ya liache bora liende.