Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,063
- 22,755
Watu watatu walituma maombi ya kazi usalama wa taifa. Wa kwanza alikuwa kijana wa miaka 25, wa pili alikuwa na miaka 35 na wa tatu alikuwa na miaka 45. Wote wakaitwa kwenye usaili wa utiifu na wakatakiwa kufika na wake zao na wakawa wanaitwa moja moja huku wake zao wakiwa wamewekwa vyumba tofauti.
Wa kwanza (25) akaitwa ndani na kupewa bastola akitakiwa kwenda aliko mkewe na kumpiga risasi. Kijana wa watu akaondoka lakini baada ya dakika zisizozidi 5 akarudi na kusema hakuweza kufanya hivyo kwa sababu bado anampenda sana mkewe.
Wa pili (35) akaingia ndani na kupewa maagizo kama yale yale. Huyu alichukua muda kidogo na baada ya dakika 15 akarudi na kusema hakuweza kumwua mkewe kwa sababu anawapenda sana watoto wake na bado wanaomhitaji mama yao.
Wa tatu (45) kupewa tu bastola akatoka na haikuchukua muda, mlio wa risasi ukasikika ukifwatiwa na vurumai kutoka chumbani aliko mkewe. Mlango kufunguliwa akakutwa jamaa kasimama na mbele yake kuna maiti ya mkewe. Kwa mshangao akaulizwa kafanya nini. Jamaa huku akihema akafoka, " Kuna mshenzi moja kaweka risasi bandia (blanks) na hivyo imebidi nimmalize kwa kumnyonga."
Wa kwanza (25) akaitwa ndani na kupewa bastola akitakiwa kwenda aliko mkewe na kumpiga risasi. Kijana wa watu akaondoka lakini baada ya dakika zisizozidi 5 akarudi na kusema hakuweza kufanya hivyo kwa sababu bado anampenda sana mkewe.
Wa pili (35) akaingia ndani na kupewa maagizo kama yale yale. Huyu alichukua muda kidogo na baada ya dakika 15 akarudi na kusema hakuweza kumwua mkewe kwa sababu anawapenda sana watoto wake na bado wanaomhitaji mama yao.
Wa tatu (45) kupewa tu bastola akatoka na haikuchukua muda, mlio wa risasi ukasikika ukifwatiwa na vurumai kutoka chumbani aliko mkewe. Mlango kufunguliwa akakutwa jamaa kasimama na mbele yake kuna maiti ya mkewe. Kwa mshangao akaulizwa kafanya nini. Jamaa huku akihema akafoka, " Kuna mshenzi moja kaweka risasi bandia (blanks) na hivyo imebidi nimmalize kwa kumnyonga."