Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Jamani tokea hili bunge lianze nimekuwa nikiona spika, naibu au mwenyekiti, akiwa na kiu kubwa ya kuomba uthibitisho wa jambo fulani hasa lililotamkwa na wabunge wa upinzani. Wabunge wetu wamekuwa wanajitahidi sana kuthibitisha kwasababu kuu mbili moja ni kwamba wasipothibitisha hatua za kinidhamu huchukuliwa dhidi yao na pili wanafanya hivyo ili kuonyesha kwamba wanajua wakifanyacho. Sasa nataka kujua upande wa pili ni hatua gani imewahi kuchukuliwa baada ya kupata uthibitisho?
Kwa mfano Lema aliwahi kuthibitisha uongo wa Waziri mkuu bungeni, waziri mkuu alichukuliwa hatua gani? au kwasasa mwenyekiti anataka uthibitisho toka kwa Tundu Lisu ili aufanyie kazi gani?
Kwa mfano Lema aliwahi kuthibitisha uongo wa Waziri mkuu bungeni, waziri mkuu alichukuliwa hatua gani? au kwasasa mwenyekiti anataka uthibitisho toka kwa Tundu Lisu ili aufanyie kazi gani?