mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,837
- 8,221
Jana nimesikiliza radio ya Kiislamu ,ambapo mtaalamu wa mambo ya dini ya Kiislamu alikuwa anaelezea jinsi ya Kadhi Mkuu atakavyopatikana,amesema masheikh watakaa na kumpendekeza mtu watakaye muona anafaa kuwa Kadhi Mkuu ambaye kwao wao ndiye atakuwa kama mkuu wa mambo ya maamuzi ya kisheria yahusuyo masuala ya waumini wa Kiislamu hapa Tanzania,na wakimpendekeza huyo mtu ,jina lake litapelekwa kwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,ambaye ndiye atakaeidhinisha na kuwa Kadhi Mkuu ni .............,sasa mimi nilichoshangaa ni je kwanini Raisi wa Jamhuri ya Muungano ndie aidhinishe uteuzi wa Kadhi Mkuu?kwani je serikali ina dini?na kwa Kadhi Mkuu kuidhinishwa na Raisi ina maana ni mwaajiriwa wa serikali? na kama ndio hivyo je atafuata masharti ya ajira ya serikali na kwa kuwa Raisi ndie atakayeidhinisha ina hela yangu ya kodi mimi mkiristo ndio italipa mshahara na marupurupu ya muislam?
Hakika kama mambo ndio hivyo basi sina budi kusema Serikali kwa kukubali suala la Kadhi Mkuu kushughulikiwa na serikali inatupeleke mahali kusiko sisi watu wa dini nyingine,mwishowe hata wapagani watadai wawe na musimamizi wa mambo yao ya kisheria atakayelipwa na serikali.
Hakika kama mambo ndio hivyo basi sina budi kusema Serikali kwa kukubali suala la Kadhi Mkuu kushughulikiwa na serikali inatupeleke mahali kusiko sisi watu wa dini nyingine,mwishowe hata wapagani watadai wawe na musimamizi wa mambo yao ya kisheria atakayelipwa na serikali.