Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Katika hali inayothibitisha ukiukwaji na uporomokaji wa maadili katika sekta ya umma ni uteuzi wa Jaji Werema uliofanywa na JK kuwa Mwanasheria Mkuu..........Kisa ni kugonganisha mihimili mitatu ya dola.........
Katika hukumu iliyotolewa na Majaji 3 nchini Kenya kwenye kesi ya Harun Mwau dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Kenya na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa nchini Kenya iliamuliwa ya kuwa ni makosa kwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Bw. Aaron Ringera au Mwanahaki yeyote kuwa Mkurugenzi Mkuu wa K.A.C.C.- yaani Taasisi ya kuzuia rushwa......................
Majaji hao kwenye uamuzi wao waliona kuna mgongano mkubwa wa kikatiba kwa Jaji ambaye jamii inamtarajia kuwa ni mtoa haki kuwa upande wa kuwashitaki raia na hivyo hali hiyo ingepunguza imani ya raia kama Mahakama zingeliwatendea haki bila ya upendeleo wakati mmoja wao ni sehemu ya uendesha mashitaka......
Kwa kauli moja walitengua uteuzi wa Jaji Ringera kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia rushwa ya Kenya......
Nasi, JK katuingiza kwenye mgogoro wa kikatiba kwa kumteua Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu na kusababisha mikanganyiko mikubwa ya kikatiba..........
Kama Jaji, raia tunamtegemea Jaji Werema awe upande wa kutoa haki na kama Mwanasheria Mkuu tunamtegemea awe mdai haki................kazi mbili zenye migongano ya masilahi na ni kazi ambazo haziwezi kufanywa na mtu mmoja....................
Ni vigumu kwa raia wa kawaida kuona kuwa hakuna upendeleo pale ambapo Jaji wa Mahakama kuu anapokuwa ni sehemu ya kudai haki na dhana ya upendeleo ipo wazi kabisa na uteuzi wa Jaji Werema ni dhahiri unakinzana na katiba.................
Kwenye kesi inayofanana na hiyo hapa nchini iliyohusu mawakili kuwa wabunge, Mahakama kuu ilisema katiba inakataza mwingiliano wa mihimili mitatu ya dola lakini Bunge halijatunga sheria za kukataza ushiriki wa mtu mmoja mmoja kuwepo kwenye zaidi ya muhimili mmoja na hivyo mahakama mikono yake imefungwa..............How pathetic....
Hoja hizi ni dhaifu kwa sababu kazi ya Mahakama Kuu ni kutafsiri sheria na kama sheria hazipo bado wanatakiwa kutoa msimamo wa kisheria unaopaswa kufuatwa...............
Jingine uamuzi huu siyo wa mwisho kwa sababu Mahakama ya Rufaa haikupewa nafasi ya kutoa tafsiri sahihi ya kisheria.......................kuna uhaja wa uteuzi wa Jaji Werema kuhojiwa Mahakama Kuu na kama majibu ya awali yatarudiwa basi swala hili likakatiwa rufaa mahakama ya juu kabisa ili tuwe na tafsiri sahihi ya kisheria kuhusiana na haya matumizi mabaya ya madaraka ambayo JK amekuwa akiyafanya kwa kuikandia katiba...............
Jingine hii ni hoja nyingine ya kuwa na Katiba mpya kuondoa migongano ya mihimili mitatu ya dola inayosababishwa na watendaji kwa ubinafsi wao................haina maana kukataza mwingiliano wa mihimili tajwa lakini tukasubiri sheria zitungwe kukataza watu binafsi kutoleta hyo migongano.................huu ni upuuzi wa wazi wa kuibeza katiba kwa kupooza malengo yake kwa kunyima sheria kuundwa.............................
Ushauri wangu ni kuwa uteuzi wa Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu ni ukiukwaji mkubwa wa katiba yetu inayokataza mwingiliano wa mihimili mitatu ya dola na kuna uhaja wa kuangalia uwezekano wa kuiomba Mahakama kuu na hata ikibidi Mahakama ya Rufaa kutoa tafsiri sahihi ya kisheria.........................
Katika hukumu iliyotolewa na Majaji 3 nchini Kenya kwenye kesi ya Harun Mwau dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Kenya na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa nchini Kenya iliamuliwa ya kuwa ni makosa kwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Bw. Aaron Ringera au Mwanahaki yeyote kuwa Mkurugenzi Mkuu wa K.A.C.C.- yaani Taasisi ya kuzuia rushwa......................
Majaji hao kwenye uamuzi wao waliona kuna mgongano mkubwa wa kikatiba kwa Jaji ambaye jamii inamtarajia kuwa ni mtoa haki kuwa upande wa kuwashitaki raia na hivyo hali hiyo ingepunguza imani ya raia kama Mahakama zingeliwatendea haki bila ya upendeleo wakati mmoja wao ni sehemu ya uendesha mashitaka......
Kwa kauli moja walitengua uteuzi wa Jaji Ringera kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia rushwa ya Kenya......
Nasi, JK katuingiza kwenye mgogoro wa kikatiba kwa kumteua Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu na kusababisha mikanganyiko mikubwa ya kikatiba..........
Kama Jaji, raia tunamtegemea Jaji Werema awe upande wa kutoa haki na kama Mwanasheria Mkuu tunamtegemea awe mdai haki................kazi mbili zenye migongano ya masilahi na ni kazi ambazo haziwezi kufanywa na mtu mmoja....................
Ni vigumu kwa raia wa kawaida kuona kuwa hakuna upendeleo pale ambapo Jaji wa Mahakama kuu anapokuwa ni sehemu ya kudai haki na dhana ya upendeleo ipo wazi kabisa na uteuzi wa Jaji Werema ni dhahiri unakinzana na katiba.................
Kwenye kesi inayofanana na hiyo hapa nchini iliyohusu mawakili kuwa wabunge, Mahakama kuu ilisema katiba inakataza mwingiliano wa mihimili mitatu ya dola lakini Bunge halijatunga sheria za kukataza ushiriki wa mtu mmoja mmoja kuwepo kwenye zaidi ya muhimili mmoja na hivyo mahakama mikono yake imefungwa..............How pathetic....
Hoja hizi ni dhaifu kwa sababu kazi ya Mahakama Kuu ni kutafsiri sheria na kama sheria hazipo bado wanatakiwa kutoa msimamo wa kisheria unaopaswa kufuatwa...............
Jingine uamuzi huu siyo wa mwisho kwa sababu Mahakama ya Rufaa haikupewa nafasi ya kutoa tafsiri sahihi ya kisheria.......................kuna uhaja wa uteuzi wa Jaji Werema kuhojiwa Mahakama Kuu na kama majibu ya awali yatarudiwa basi swala hili likakatiwa rufaa mahakama ya juu kabisa ili tuwe na tafsiri sahihi ya kisheria kuhusiana na haya matumizi mabaya ya madaraka ambayo JK amekuwa akiyafanya kwa kuikandia katiba...............
Jingine hii ni hoja nyingine ya kuwa na Katiba mpya kuondoa migongano ya mihimili mitatu ya dola inayosababishwa na watendaji kwa ubinafsi wao................haina maana kukataza mwingiliano wa mihimili tajwa lakini tukasubiri sheria zitungwe kukataza watu binafsi kutoleta hyo migongano.................huu ni upuuzi wa wazi wa kuibeza katiba kwa kupooza malengo yake kwa kunyima sheria kuundwa.............................
Ushauri wangu ni kuwa uteuzi wa Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu ni ukiukwaji mkubwa wa katiba yetu inayokataza mwingiliano wa mihimili mitatu ya dola na kuna uhaja wa kuangalia uwezekano wa kuiomba Mahakama kuu na hata ikibidi Mahakama ya Rufaa kutoa tafsiri sahihi ya kisheria.........................