Uteuzi wa Dr. Hussein Mwinyi Wizara ya Afya Umezingatia Masuala ya Muungano?

Dr Mwinyi ni Mtanzania kama walivyo watanzania wengine. Hata Mtkila alipohoji Mahakamani kuhusu suala la Wazanzibari kuteuliwa kwenye Wizara zisizo za Muungano hoja yake ilishindwa vibaya! Tatizo linalotusumbua sasa hivi watz ni ubaguzi uliopandikizwa na wanasiasa! Utasikia siku hizi "Rais wa safari hii atatoka Kaskazini!" Tutafika kweli kwa style hii?


Nilikuwa naongea na rafiki yangu asubuhi hii kuhusu baraza jipya na nilipomtaja Mwinyi kuwa yeye ameteuliwa waziri wa afya kauli ya kwanza alisema "afya haiko muungano na huyu ni mbunge wa Zanzibar, ameingiaje? Hii ni kauli ya mzanzibari.tuachie hapo.

Sasa turudi kwenye muungano wenyewe, kuna makubaliano kuhusu wizara/mambo gani yawe ya muungano ya yape yasiwe ya muungano, sasa kama hayo mambo hayazingatiwi kwenye uteuzi wa mawaziri kuna sababu gani ya kuwa na makubalino ya muungano? Hoja hapa ni kuheshimu taratibu na makubaliano ya muungano. simple.

Mwisho, huu uteuzi wa Dr. Mwinyi unawaweka wapi wabunge wa CCM toka Tanzania bara? Kwamba miongoni mwao hakuna anayefaa kuongoza wizara ya afya na hivyo rais amelazimika kukopa toka Zanzibar? Nadhani wakati mwingine matatizo ya CCM yanasababishwa na wao wenyewe kama huu uteuzi. Hapa jukwaani tunaongea but I am sure ndani ya CCM kwenyewe watu wanahasira.
 
Dr
Mwinyi ni Mtanzania kama walivyo watanzania wengine. Hata Mtkila alipohoji Mahakamani kuhusu suala la Wazanzibari kuteuliwa kwenye Wizara zisizo za Muungano hoja yake ilishindwa vibaya! Tatizo linalotusumbua sasa hivi watz ni ubaguzi uliopandikizwa na wanasiasa! Utasikia siku hizi "Rais wa safari hii atatoka Kaskazini!" Tutafika kweli kwa style hii?

nafkiri wewe ndio mbaguzi!kwanini hutaki kuongelea hoja na kutuonesha kama ni sahihi au lah unakimbilia conclusion zisizo na basis?mwinyi alikuwa waziri kwenye wizara ambayo inahusika na mambo ya muungano,hakuna aliyehoji maana hatukuona utata hapo.Nahodha hakuwa mbunge wa jmt akateuliwa kwanza afu akapewa wizara inayohusika na mambo ya muungano..ikawa sawa kabisa wala hatukuhoji maana uzanzibari haikuwa ishu hapo maana mambo hayo ni ya muungano.
Inawezekana, kwa mfano, dr hamis kigwangala akateuliwa waziri wa afya zanzibar?
TUENDELEE KUZUNGUMZIA HOJA YA MSINGI.
 
Uteuzi wa Dr. Mwinyi kuwa Waziri wa afya na Ustawi wa Jamii ni mzuri sana kuliko wa Mh. Nchimbi kuwa waziri wa Mambo ya Ndani? Ukizingatia uozo ulipo Immigration, Jeshi la Polisi na wizara yenyewe kuandikisha NGO zisizo na mbele wala nyuma hapo kuna walakini alitakiwa mtu kama Sitta, au Wassira au Ngwilizi kuweza kujenga nidhamu ndani ya Wizara hii chafu?
 
achana na mambo ya yeye kuwa dr, kwani yuko peke yake mle bungeni? Mbona mwakyusa yupo? Naibu wake naye si dr? Lazima tutende yale tunayoyaongea,haya mambo ya kutaka wengine wafaidi upande mmoja hayafai. Ndo maana watu wanataka serikali moja ili ieleweke kwambo wote sawa. Hawa jamaa kwao wanaubaguzi hata ukienda kufanya field sembuse kazi,,? Mbona wao wanafaidi kwetu?
mkuu hapa si suala la kufaidi au kutofaidi ni suala la katiba haifuatwi kwanini!?
 
nafkiri wewe ndio mbaguzi!kwanini hutaki kuongelea hoja na kutuonesha kama ni sahihi au lah unakimbilia conclusion zisizo na basis?mwinyi alikuwa waziri kwenye wizara ambayo inahusika na mambo ya muungano,hakuna aliyehoji maana hatukuona utata hapo.Nahodha hakuwa mbunge wa jmt akateuliwa kwanza afu akapewa wizara inayohusika na mambo ya muungano..ikawa sawa kabisa wala hatukuhoji maana uzanzibari haikuwa ishu hapo maana mambo hayo ni ya muungano.
Inawezekana, kwa mfano, dr hamis kigwangala akateuliwa waziri wa afya zanzibar?
TUENDELEE KUZUNGUMZIA HOJA YA MSINGI.

Hivi huyu Nahodha si mjumbe pia wa Baraza la Wawakilishi kule Zanzibar? Kama ndivyo, huu Muungano wetu una tatizo kubwa kuliko tunavyodhani.
 
Jk"Usipokubali kuliwa kidogo huli,sasa wewe unataka kula tu bila kuliwa haiwezèkani'! Ili tuendelee kuwala wazenji lazma tulìwe kidogo.
 
Hussein Mwinyi kateuliwa kwa sababu ya "Utanzania" wake na si kwa sababu ya "Uzanzibari" wake!
naomba uwe serous kidogo, Tusicheze na nchi ya watu, nadhani watu wanakumbuka issue ya mafuta. wakitaka tuwe watanzania wafute uzanzibari kama sisi tulivyofuta utanganyika. TUWE NA SERIKALI MOJA YENYE TIJA.
 
dr mwinyi ni mtanzania kama walivyo watanzania wengine. Hata mtkila alipohoji mahakamani kuhusu suala la wazanzibari kuteuliwa kwenye wizara zisizo za muungano hoja yake ilishindwa vibaya! Tatizo linalotusumbua sasa hivi watz ni ubaguzi uliopandikizwa na wanasiasa! Utasikia siku hizi "rais wa safari hii atatoka kaskazini!" tutafika kweli kwa style hii?
duu haya maneno unayatoa moderator wa jf, ndo maana watu wanapigwa bun hovyo!
 
Jk"Usipokubali kuliwa kidogo huli,sasa wewe unataka kula tu bila kuliwa haiwezèkani'! Ili tuendelee kuwala wazenji lazma tulìwe kidogo.
 
Mwinyi ameingia BUNGENI kwa mambo ya Muungano and not otherwise. He is only responsible 4 it.
 
..when will JK be serious??

..kwanini anafanya kazi kwa mizaha-mizaha na kulipua-lipua kiasi hiki?

..what is so difficult kutenganisha wizara za muungano, na wizara zisizo za muungano, na kuteua mawaziri kuzingatia katiba??


..Raisi has just appointed Dr.Hussein Ali Hassan Mwiyi, mbuge wa kwahani Zanzibar, kuwa Waziri wa Afya, wakati inaeleweka kwamba afya si suala la muungano!!

Kwa jicho jingine, sidhani kama inawezekana Rais hajui au mjinga kiasi hicho! Hapa nahisi kuna bomu amewategea hasa CHADEMA ili kuendelea kuwadhoofisha hasa upande wa Zanzibar na hatimaye Bara. Kivipi? Iko hivi:-

- Rais anajua wabunge wa chama chake ni mazuzu wa kutupwa na kwa "nidhamu ya chama" chao waliyo nayo hakuna jinsi wataweza kuhoji.

- Rais anajua ni lazima watu makini na hasa CHADEMA na wabunge wao kwa vyovyote watahoji. Kwa mfano, binafsi sioni ni kwa vipi mtu kama Dr. Slaa au Mh. Tundu Lissu ataacha kuhoji hiki kitu.

- Kwa ile ndoa ya CCM na CUF kule Zanzibar, kwa kuwa ni wamoja, watakuwa against na hoja za CHADEMA kwamba ni za kibaguzi dhidi ya Zanzibar na kwa kuwa wenzetu wale wa upande wa pili ni mabingwa wa kulipuka bila kufikiri itaonekana kuwa ni kweli japo halina mantiki ya kikatiba na kisheria.

- Wakishaonesha "ubaguzi" wa CHADEMA kwa Zanzibar then watatumia baadhi ya viongozi wa dini kueneza propaganda kwamba kama CHADEMA imewabagua wa-Zanzibar kiasi hiki pamoja na nia njema ya Mwalimu J.K. Nyerere na Mzee Karume kuasisi Muungano itakuwaje CDM ikichukua madaraka?

- Na kwa kuwa waTanzania ni watu wa kupelekeshwa tu bila kuhoji, propaganda husika itakuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa hasa kuelekea 2015.

USHAURI: Viongozi wa Chadema kuweni makini sana na bomu hili katika mijadala mbali mbali vinginevyo lina athari kubwa sana kwa kuzingatia elimu duni ya uraia kwa wananchi. Hata hapa hapa JF tumeshashuhudia mawazo muflisi kuhusiana na hoja hii.

Nawasilisha.
 
Hivi hapa kwetu Tanzania, kweli katiba is a living document kama tunavyoamabiwa? Naona mara nyingi group interest zinazidi zile za katiba. Ndo maana kuna mazingaombwe mengi sana.
 
Huo muungano wenu kila kunavyokucha unazidi kukera, yaani dr. wa milipuko pamoja na uzembe wake ktk wizara ya ulinzi, hana sifa ya kupewa wizara nyeti kama ya afya, lkn bado wamepeana...! Wapi gobore langu nikawinde, na isitokee mmoja wao ajipendekeze kwenye anga zangu, maana hii nchi sasa ni kanuni za kìporipori tu.
 
Ni mwendawazimu pekee anayeweza kukubali Hussein Mwinyi kuwa Waziri wa Afya katika wizara isiyo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa isiyo ya Muungano.

Ndiyo nasema ni mwendawazimu pekee.

Kwani hata mjinga ama zuzu akielewesha hawezi kulikubali.

Ni kwanini watu wenye akili zenu timamu mnalichezea jambo hili? Ikiwa kama Mwinyi hakuwa na uchungu wala kujali kwa wabara waliokufa na kupata madhira makuu namna ile mara mbili, unategemea atakuwa na uchungu wa kupanga mikakati ya kuboresha huduma za afya za wabara?

Kikwete kavunja KATIBA, amekiuka makubaliano yalipo katika hati ya Muungano.

Mwinyi akijua wazi kuwa hastahili kuwepo katika MoHSW amekubali kwasababu ya uroho wa madaraka.

Suluhisho Mwinyi asiapishwe vinginevyo ugomvi wa wao wazanzibar na sisi watanganyika sasa utapamba moto. Binafsi sitamwacha Mwinyi kuongoza MoHSW. Tabia ya upopo siitaki. Mara yeye Mzanzibar, ooh! Mara mbara, NO!
 
Wengine walishawahi kujibu hivi hapa bungeni
1703.jpg
Kombo, Kombo Khamis [CUF]
Mgogoni Constituency
Session NoQuestion NoTo the Ministry ofSectorDate Asked
415VICE PRESIDENT'S OFFICE (UNION AFFAIRS)Union Affairs8 June 2011
Principal Question No
(a) Je, kuna Wizara ngapi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

(b) Je, ni Wizara ngapi zinahusiana na Mambo ya Muungano baina ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani?
ANSWERS TO PRINCIPAL QUESTION #15 SESSION # 4
1668.jpg
Answer From Hon. Suluhu, Samia Hassan
VICE PRESIDENT'S OFFICE (UNION AFFAIRS)
WAZIRI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kombo Khamis Kombo, Mbunge wa Mgogoni, lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a)Idadi ya Wizara za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikibadilika mara kwa mara kutokana na Rais anayekuwepo madarakani anavyoona inafaa kutekeleza kazi zake kulingana na mamlaka aliyopewa na Katiba. Kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 494 la tarehe 17 Desemba, 2010 kwa sasa kuna Wizara 26 zinazoongwa na Mawaziri 29.

(b)Mheshimiwa Spika, jibu ni kwamba zipo jumla za Wizara 6 ambazo ni za Muungano, Wizara hizo ni Ofisi ya Makamu wa Rais inayoshughulika na Mambo ya Muungano, Wizara ya Fedha kupitia GFC, BOT na Sera za Kifedha, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Aidha, zipo Wizara ambazo si za Muungano lakini zinasimamia masuala ya Muungano kama yalivyoorodheshwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Mfano Wizara hizo ni Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambao hushughulika na suala la Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge ambayo husimamia masuala ya Bunge, Wizara ya Nishati na Madini ambayo husimamia suala la mafuta na gesi asilia, Wizara ya Katiba na Sheria ambayo husimamia suala la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Viwanda na Biashara ambao husimamia masuala ya Biashara za Nje, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia inayosimamia Masuala ya Mawasiliano, Wizara ya Uchukuzi ambayo husimamia suala la usafiri wa anga na majini na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo husimamia suala la Elimu ya Juu na Baraza la Mitihani la Taifa.

Hapo sijaona Wizara ya Afya ikiorodheshwa kama ni ya Muungano!
 
..when will JK be serious??

..kwanini anafanya kazi kwa mizaha-mizaha na kulipua-lipua kiasi hiki?

..what is so difficult kutenganisha wizara za muungano, na wizara zisizo za muungano, na kuteua mawaziri kuzingatia katiba??

..Raisi has just appointed Dr.Hussein Ali Hassan Mwiyi, mbuge wa kwahani Zanzibar, kuwa Waziri wa Afya, wakati inaeleweka kwamba afya si suala la muungano!!

Mkuu JokaKuu,
Hakuna sheria wala kifungu kilichovunjwa hapo. Sifa ya kuwa waziri kwenye wizara yoyote TZ ni kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano.

Pia kumbuka Dr. Mwinyi alikuwa naibu wa wizara hiyo hiyo wakati wa rais Mkapa. Ingawaje wakati huo nafikiri alikuwa mbunge upande wa bara. Baadaye kaenda kugombea kwao Visiwani.

Mfumo wetu hauna tofauti na wa Waingereza ambapo Kama unavyojua Wabunge toka Scotland na Wales wanaongoza wizara ambazo zinahusika na mambo ya England pekee.

Kikawaida Wazanzibari wamekuwa wakipewa wizara za muungano zaidi ila huo ni utaratibu tu japo sio sheria.
 
Asprin
Huu muungano si wa bara tunanufaika na nini?
Ukiangalia wa Zanzibar ndo wanao nufaika zaidi maana bidhaa nyingi zinatoka bara kwenda ZNZ na hao hao wazanzibari hawautaki huu muungano je si wa bara tunao ng'ang'ania tunanufaika na nini?
 
JK NI JANGA LA TAIFA hakuna ubishi, na kama siyo mbishi katika uteuzi na utendaji wake nafikri hana washauri.Tazama aibu aliyofanya jana kumteua yule mama kutoka zanzibar kuwa mbunge na hapo kuwa naibu waziri wa fedha,je hapo vetting imefanyika saa ngapi na kupata uhalali wake pia inaonekana.JK KWANGU MIE MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU na kama unafanya appraisal mostly is not viable and sustainable at all in any way.:baby:
 
Kazi ipo...nadhani principle iliyotumika ni ifuatavyo:

Waziri yeyeote katika serikali ya muungano anatokana na mbunge yeyote wa bunge la muungano (ikiwamo wale wa kuteuliwa na Rais). Wajumbe wa baraza la wawakilishi (typical wabunge wa Zanzibar) hawa-qualify kuwa mawaziri wa muungano unless kupitia kwa uteuzi maalum wa Rais kuwa wabunge wa bunge la muungano.

On the other hand, wabunge wa bunge la muungano specifically kutoka bara (Tanganyika) hawa-qualify kuwa wajumbe wa baraza la wawakilishi la Zanzibar (typical bunge la Zanzibar), wala kuwa mawaziri katika serikali nusu (semi-autonomous govt) ya Zanzibar.

Kwa kifupi huu muungano wetu ni fumbo mshazari ambalo wanalolijua jibu lake walishakufa sisi tutabaki kuumia vichwa kujaribu kufumbua mpaka na sisi tutakapo aaga Dunia.:hat:
 
Back
Top Bottom