Uteuzi wa Dr. Hussein Mwinyi Wizara ya Afya Umezingatia Masuala ya Muungano?

Nikitafakari sana mambo ya Muungano huwa kichwa kinaniuma. Cha ajabu wanaoufaidi sana Muungano ndo wanaoongoza kuupinga. Wanaoumizwa ndo wanautetea. Binafsi sijawahi ona faida ya Muungano. Lord have mercy on me...
 
Mkuu Mwita, masuala ya Muungano yamenichosha, ujadiliwe upya.

Mkuu MNYISANZU,
Mkuu wa kaya hataki muungano ujadiliwe kabisa.
Baada ya jumuiya za uamsho na mihadhara huko zanzibar kuwasha moto wa kupata sahihi za wazanzibari kutaka kura ya maoni juu ya muungano, SUK Zanzibar imewapiga marufuku, sasa hapo ndio uone wakubwa wanavyoulinda muungano hawataki uguswe kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri suala la muungano halikuzingatiwa hapa ila kilichoangaliwa zaidi ni taaluma aliyonayo Dr Mwinyi na mhe President anaamini atafit zaid katika wizara hiyo ya afya kuliko ile ya ulinzi so suala la muungano halihusiki kwa hapo.
 
Nikitafakari sana mambo ya Muungano huwa kichwa kinaniuma. Cha ajabu wanaoufaidi sana Muungano ndo wanaoongoza kuupinga. Wanaoumizwa ndo wanautetea. Binafsi sijawahi ona faida ya Muungano. Lord have mercy on me...

Asprin
Nina uhakika watanganyika wengi hawanufaiki na muungano na hawauhitaji lakini kitu cha ajabu ni kwamba hawalalamiki hadharani kama wanavyofanya wazanzibari.
Nina uhakika ikiitishwa kura ya maoni juu ya muungano mapendekezo yatakuwa ni either serikali tatu ama kuuvunja.

Na kwa kulitambua hilo unaona viongozi wa nchi hawataki muungano uguswe katika mjadala wa katiba mpya.
 
Last edited by a moderator:
Asprin
Nina uhakika watanganyika wengi hawanufaiki na muungano na hawauhitaji lakini kitu cha ajabu ni kwamba hawalalamiki hadharani kama wanavyofanya wazanzibari.
Nina uhakika ikiitishwa kura ya maoni juu ya muungano mapendekezo yatakuwa ni either serikali tatu ama kuuvunja.

Na kwa kulitambua hilo unaona viongozi wa nchi hawataki muungano uguswe katika mjadala wa katiba mpya.

Unaweza kukubaliana na mimi sasa kuwa watanganyika tumelogwa na sasa karibia wote tumekuwa mazezeta? Watu takribani milioni 40 tutakubalije kuufyata kwa watu wasiozidi 100?
 
Last edited by a moderator:
Dr. Hussein Mwinyi ambaye ni mbunge wa Kwahani Zanzibar, ameteuliwa kuongoza wizara ya afya na ustawi wa jamii.

Kumbukumbu zangu zinanionyesha kwamba Masuala ya Afya si ya muungano na SUK Zanzibar wanaye waziri wa afya Juma Duni Haji.

Wizara zinazohusika na mambo ya muungano ni pamoja na Mambo ya Nje, Mambo ya Ndani, Ulinzi na JKT, Fedha, Habari, Vijana na Michezo na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Naomba ufafanuzi toka kwa mtu mwenye taarifa zaidi juu ya hili. Thanks!

wabongo bana mmeshaanza mambo yenu..dk hussein mwinyi he is a doctor by proffn so itakuwa rahisi kuongoza jahazi kuliko lile Li mponda lenu hata halijui kuwa panadol ni brand name...
 
tunataka kazi...awe znz au mtanganyika...sisi tunataka kazi!!!!

Wakati Nyerere na Karume wanaziunganisha Tanganyika na Zanzibar walikubaliana masuala ya muungano na mengine ambayo si ya muungano kutokana na muundo wa serikali mbili.
Usipojali hayo makubaliano basi kutakuwa hakuna sababu ya kuwa na serikali mbili kama makubaliano ya muungano yalivyo. Kwa mtazamo huu wako tunapaswa kuwa na serikali moja ili yeyote atakayeteuliwa tuseme hewala.
 
Nafikiri suala la muungano halikuzingatiwa hapa ila kilichoangaliwa zaidi ni taaluma aliyonayo Dr Mwinyi na mhe President anaamini atafit zaid katika wizara hiyo ya afya kuliko ile ya ulinzi so suala la muungano halihusiki kwa hapo.

huyu si alikuwepo 2005? Ni huyu na anna walileta siasa pale starlight na mgomo ukaendelea? Nanusa harufu ya mgomo utakaosababishwa na huyu jamaa kwa chuki zake binafsi.
 
wabongo bana mmeshaanza mambo yenu..dk hussein mwinyi he is a doctor by proffn so itakuwa rahisi kuongoza jahazi kuliko lile Li mponda lenu hata halijui kuwa panadol ni brand name...

Ndugu yangu Babyemma soma kwa taratibu ili uelewe kinachojadiliwa hapa.
Kila mmoja anafahamu kwamba Hussein Mwinyi kitaaluma ni Medical Doctor na hakuna anayezungumzia au kuhoji taaluma yake.
Kinachohojiwa hapa ni kama makubaliano ya muungano yamezingatiwa katika kuteuliwa kwake.
 
Last edited by a moderator:
This is a valid question to be asked. Jamani huu muungano ni wa aina gani? Changu changu, chako changu. Wao wanaongoza mambo yasiyowahusu huku kwetu, lakini kinyume chake ni balaa kubwa.
 
Unaweza kukubaliana na mimi sasa kuwa watanganyika tumelogwa na sasa karibia wote tumekuwa mazezeta? Watu takribani milioni 40 tutakubalije kuufyata kwa watu wasiozidi 100?

Tena aliyeturoga ameshafariki na vibuyu vyake vyote vimeshatiwa moto. Tunahitaji neema ya Mungu tu ili tuweze kupona upofu tulionao.
Wakati huu tunapoandika katiba mpya ndio muda muafaka wa kuuweka sawa muungano. Tukiacha kuuboresha wakati huu basi huko mbele ya safari tutarajie mambo makubwa sana tena ya hatari.
 
wabongo bana mmeshaanza mambo yenu..dk hussein mwinyi he is a doctor by proffn so itakuwa rahisi kuongoza jahazi kuliko lile Li mponda lenu hata halijui kuwa panadol ni brand name...

achana na mambo ya yeye kuwa dr, kwani yuko peke yake mle bungeni? Mbona mwakyusa yupo? Naibu wake naye si dr? Lazima tutende yale tunayoyaongea,haya mambo ya kutaka wengine wafaidi upande mmoja hayafai. Ndo maana watu wanataka serikali moja ili ieleweke kwambo wote sawa. Hawa jamaa kwao wanaubaguzi hata ukienda kufanya field sembuse kazi,,? Mbona wao wanafaidi kwetu?
 
Seriously, members wengine wanatuangusha! Ishu hapa sio ubaguzi wala hamna anaye-question integrity ya elimu yake. Swali ni utaratibu gani umetumika kumpa yeye uongozi wa mambo yasiyomhusu?
 
huyu si alikuwepo 2005? Ni huyu na anna walileta siasa pale starlight na mgomo ukaendelea? Nanusa harufu ya mgomo utakaosababishwa na huyu jamaa kwa chuki zake binafsi.

Naam Nyalotsi kwa kutukumbusha hili.

Wakati huo akiwa mbunge wa mkuranga, kabla hajakimbilia kwahani. Akateuliwa kuwa naibu waziri wa afya chini ya waziri anna abdallah.
Ule mgomo walishindwa kabisa kuuhandle hivyo kusababisha hali mbaya sana katika huduma za afya na kusababisha vifo vingi.

Labda sasa ameshakomaa ataweza kuimudu wizara ya afya inagawa bado swali langu la msingi ni kama Raisi amezingatia makubaliano ya muungano katika uteuzi wake.
 
Last edited by a moderator:
Ukienda Zanzibar kuomba kumiliki Ardhi wewe na Mtaliano, Mtaliano atapewa Ardhi ajenge Hoteli wewe utaambiwaArdhi si mambo ya Muungano. Wizara ya Afya si ya Muungano na hivyo haipaswi kuendeshwa na Mzanzibari watuachie tuendeshe mambo yetu sisi wenyewe na wao waendelee na "uamsho" wao!!
 
Seriously, members wengine wanatuangusha! Ishu hapa sio ubaguzi wala hamna anaye-question integrity ya elimu yake. Swali ni utaratibu gani umetumika kumpa yeye uongozi wa mambo yasiyomhusu?

MtamaMchungu,
Nakushukuru sana kwa kuona mantiki ya hoja yangu na kuielewa. Nadhani hawa wanaojaribu kujenga taswira ya ubaguzi katika hili ni katika namna ya kushindwa kujibu hoja ya msingi.
Hapa tuna mambo ya muungano ambayo ni muhimu sana tukayazingatia hata kama muundo wa muungano wenyewe bado haukubaliki kihivyo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom