Uteuzi wa Bilal Neema Kambi ya Lowassa 2015

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
I said it yesterday (angalia hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...lal-alikuwa-aondoke-ccm-7.html#post986362),na inaelekea jamaa wa Majira wana mtizamo kama huo.

Uteuzi wa Bilal neema kambi ya Lowassa 2015
Wednesday, 14 July 2010 04:56
Na Tumaini Makene

SIKU tatu baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukamilisha uteuzi wa wagombea wake wa nafasi za juu katika uchaguzi mkuu ujao, imefahamika kuwa hatua hiyo ni kicheko kwa moja ya makundi yanayokamia kupata urais mwaka 2015 kwa kuwa limefanikiwa kupanga safu yake.

Uchaguzi wa mgombea wa urais wa CCM Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein na uteuzi wa mgombea mwenza wa urais wa muungano, Dkt. Mohamed Gharib Bilal umeelezwa na vyanzo mbalimbali vya habari ndani ya CCM, kuwa ni moja ya karata za muhimu katika mipango ya kundi hilo.



Kundi hilo linampigia chapuo Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa kuingia ikulu baada ya rafiki yake, Rais Jakaya Kikwete kumaliza muda wake.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo pamoja na baadhi ya wadadisi wa masuala ya siasa nchini, kundi hilo linaloelezwa kuwa chini ya wafanyabishara na wanasiasa maarufu nchini, kwa muda mrefu sasa limekuwa likijipanga kwa njia nyingi, ikiwemo ya kuweka safu ndani ya serikali na CCM, ili muda muafaka utakapofika lisiwe na kikwazo cha kutimiza lengo lake.

Kundi hilo linatajwa kujipenyeza na kuwa nyuma ya Dkt. Bilal katika harakati zake za kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar, na kuwa huo ulikuwa mkakati wa kujiweka karibu na mmoja wa watu waliokuwa na mvuto na nafasi ya kupata nafasi hiyo.

"Mpaka sasa haieleweki kundi hilo lilijitokeza vipi na kudandia safari ya Dkt. Bilal, maana tayari alikuwa maarufu na alikuwa akikubalika wala hakuhitaji nguvu yao na fedha. Lakini kinachoonekana kundi hili lilitaka kutisha na kuonesha ubavu wake kwa mwenyekiti wa chama ambaye alionekana kuwa nyuma ya harakati za Dkt. Shein.

"Kwa vyovyote vile kundi hili lenye wafanyabiashara walioamua kuingia siasa kwa ajili ya maslahi yao na baadhi ya wanasiasa likiwa na mtandao mkubwa bara na visiwani, linatumia kila aina ya mikakati, mizuri au michafu kujipanga kwa ajili ya urais wa Tanzania mwaka 2015, hivyo wanawekeza katika kila fursa inayojitokeza," kilisema kimoja kati ya vyanzo vyetu.

Hata baada ya Dkt. Bilal kukosa nafasi hiyo ambayo amekuwa akiitafuta tangu mwaka 2000, kundi hilo limeelezwa kuwa lilijipanga upya na kuibua taarifa za vitisho juu ya kuwapo mgawanyiko, ili kushinikiza ateuliwe kuwa mgombea mwenza na hatimaye makamu wa rais.

Mbali ya kuwa anaelezwa kuwa mtu mwenye msimamo, Dkt. Bilal anaweza kutumika kurudisha fadhila, huku kundi hilo likifurahia uteuzi wake kwa sababu mpaka mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 70, umri ambao hautamwezesha kufikiria kupigania nafasi ya kuteuliwa mgombea urais wa CCM.

Bila ya kufafanua, moja ya chanzo chetu cha habari kutoka kambi ya kundi hilo kililiambia Majira, "nafasi hiyo itatufaa kwa mwaka 2015...

Imeelezwa kuwa mbinu ya kuhakikisha anapatikana makamu wa rais (iwapo CCM ikishinda uchaguzi) ambaye hatakuwa na ushawishi wa kuwania nafasi ya urais kupitia CCM, ilikuwa ni sababu ya kumuogopa Dkt. Ali Mohamed Shein iwapo angelibaki katika nafasi ya makamu wa rais kwa kipindi kingine.

Dkt. Shein alionekana kuwa kikwazo kwa sababu angelikuwa amekaa katika nafasi hiyo kwa miaka 15 na kumpatia uzoefu wa kutosha kuwa rais wa nchi, hivyo ikiongezewa na kitu kinachosemwa kuwa '2015 itakuwa zamu ya Zanzibar' ni wazi makundi yote yanayotarajia kusaka nafasi hiyo yasingekuwa na hoja pingamizi dhidi ya uteuzi wa Dkt. Shein.

Chanzo kingine cha habari kimelieleza Majira kuwa mkakati huo uliofanywa kwa uteuzi wa nafasi za juu unaendelea hata ngazi ya ubunge, udiwani na nafasi mbalimbali ndani ya chama ili kufungua njia ya 2015 kwa Bw. Lowassa.

CHANZO: Majira
 
Hivi kweli uraisi unachongwa kwa kiwango hicho?

Ni kwanini watu wahangaike, watumie kila mbinu ili Lowasa apate uraisi?

Kuna nini kwenye uraisi wa Lowasa? Anataka kufanya nini? Kipi anatakachofanya na ambacho hajawahi kufanya?

Nionavyo binafsi, yeye anajiandaa na makundi ya maswaiba wake wakiwa na ajenda mbili.

1. Kulipiza kisasi kwa kuwaadhibu watu wote waliohusika na kuanguka kwa Lowasa na timu yake , kwenye uongozi mbalimbali. Ni kisasi ! kisasi! kisasi!

2. Kujinufaisha kiuchumi kwa kuhodhi fursa zote za kiuchumi , kufidia fursa za kiuchumi ambazo wamepunguziwa kwa vile hawako moja kwa moja serikalini kwa muda wa miaka kama saba ijayo.

Hivyo basi, Lowasa na watu wowote wanaounga mkono azma hiyo, hayo ndiyo malengo wanayotaka kuyatekeleza na hayana mstakabali mwema kwa watanzania.

Kama watanzania tuko makini , huo ndio muhula kwa kumkataaa Lowasa na vikaragosi, swali muhimu ni kama watanzania tutakubali kuwa kondoo wa kafara wa akina Lowasa mpaka lini ? mpaka lini ?, mpaka lini?.................
 
Kumaliza haya yote tunawaomba ndugu zetu wa CHADEMA watuandalie Dr. Slaa. Tafadhali naandika thread hii nikiwa na majonzi sana na nchi yangu inako elekea. Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Africa. Soma Isaya 3- 10 utaona mpango wa Mungu katika kuikomboa Tanzania.
Amina
 
Politics!!!! Lisemwalo lipo kama halipo linakuja. Inaonekana RA na EL hawajakubali kabisa kushindwa. Wanajitahidi kumdandia mtu yeyote ili mradi wafanikishe malengo yao ya kisiasa. Lakini WATASHINDWA kwa JINA LA YESU. Hii nchi si ya kufanyia majaribio ya kiuongozi.

tunakata kiongozi mwenye maono ya kuipigisha nchi hatua kimaendeleo na si kulipiza kisasi au kujinufaisha binafsi
 
Hivi kweli uraisi unachongwa kwa kiwango hicho?

Ni kwanini watu wahangaike, watumie kila mbinu ili Lowasa apate uraisi?

Kuna nini kwenye uraisi wa Lowasa? Anataka kufanya nini? Kipi anatakachofanya na ambacho hajawahi kufanya?

Nionavyo binafsi, yeye anajiandaa na makundi ya maswaiba wake wakiwa na ajenda mbili.

1. Kulipiza kisasi kwa kuwaadhibu watu wote waliohusika na kuanguka kwa Lowasa na timu yake , kwenye uongozi mbalimbali. Ni kisasi ! kisasi! kisasi!

2. Kujinufaisha kiuchumi kwa kuhodhi fursa zote za kiuchumi , kufidia fursa za kiuchumi ambazo wamepunguziwa kwa vile hawako moja kwa moja serikalini kwa muda wa miaka kama saba ijayo.

Hivyo basi, Lowasa na watu wowote wanaounga mkono azma hiyo, hayo ndiyo malengo wanayotaka kuyatekeleza na hayana mstakabali mwema kwa watanzania.

Kama watanzania tuko makini , huo ndio muhula kwa kumkataaa Lowasa na vikaragosi, swali muhimu ni kama watanzania tutakubali kuwa kondoo wa kafara wa akina Lowasa mpaka lini ? mpaka lini ?, mpaka lini?.................


Huyu jamaa anatakiwa atundikwe anyongwe kabisa uchu wake wa madaraka utatufanya tuingie kwenye vita mtu anayesujudu mafisadi,mwivi,mroho na mwenye uchu wa kutisha wa madaraka naasiyekubali yaaishe hafaiiii hata kidogo kuwa raisi wa nchi,nchi yetu sasa ni tete kisiasa haitaki majambazi na watu wenye roho za uchu kama Lowassa anaweza akafanya kitu chochote akasababisha umwagaaji waa damu,alipoteza hadhi ilishapotea haitakaa irudi tena kamwe kamwe
 
Someni Mwanahalisi muelewe kwamba waliogaragazwa katika uchaguzi huu ni EL na RA waliokuwa wamepania kumsimika Bilal urais wa Zanzibar kwa kutumia fedha na kwa tambo wakaambulia patupu! Makamu wa Rais Bara hana nguvu zozote na Bilal akifanya mchezo kutaka kufanya atakavyo badala ya kumsikiliza Rais ataonja shubiri ya jeuri ya JK.
 
Back
Top Bottom