Utetezi wangu wa Mhe. Sophia Simba dhidi ya Ukosoaji usio wa haki

Halafu kwani usomi ni nini? Mtu unaweza ukawa msomi bila kujua kiingereza? Hapa nikiwa na maana msomi unayejua lugha moja tu, Kiswahili. Au usomi ni lazima mtu uwe unajua kiingereza tena kile kama cha Pundit....heheheh.....


Usomi siyo kujua kiingereza.Ingawa kiingereza ni lugha rasmi ya pili Tanzania lakini bado wabongo wengi tuna fikra za kitumwa kwamba anayejua kiingereza ndiye msomi na ndiyo maana hata na wao viongozi wanaona ujiko kuchomekea kiingereza kwenye mazungumzo ili waonekane wasomi na wengi wanaofanya hivyo usomi wao hua una mashaka.Ndiyo maana msomi aliyeelimika kama Dr.Migiro huwezi mkuta akafanya huu upuuzi.
 
Usomi siyo kujua kiingereza.Ingawa kiingereza ni lugha rasmi ya pili Tanzania lakini bado wabongo wengi tuna fikra za kitumwa kwamba anayejua kiingereza ndiye msomi na ndiyo maana hata na wao viongozi wanaona ujiko kuchomekea kiingereza kwenye mazungumzo ili waonekane wasomi na wengi wanaofanya hivyo usomi wao hua una mashaka.Ndiyo maana msomi aliyeelimika kama Dr.Migiro huwezi mkuta akafanya huu upuuzi.

Unajua kwa uhakika kabisa kuwa Dokta Migiro huwa hachanganyi lugha?
 
Unajua kwa uhakika kabisa kuwa Dokta Migiro huwa hachanganyi lugha?

Niliwahi kuona mara nyingi tu akihojiwa huwa anajitahidi sana kutochanganya lugha.Kama kiingereza basi ataongea kiingereza na kama kiswahili basi ataongea kiswahili.Sisemi kwamba watu hawachanganyi lugha lakini siyo kihivyo.Yaani kwa mfano mtu anashindwa kusema 'karne ya ishirini na moja' baada ya maneno 'katika hii'akasema twenty first century,mkuu huu ni ulimbukeni!
 
- Kwa kawaida huwa ninasikiliza maneno ya mwanzo tu basi katika hizi interviews za hawa wanasiasa wa bongo, lakini this one nimeisikiliza mpaka mwisho kwa sababu nilitaka kusikia anything new kuliko ninavyomfahamu waziri mwenyewe, na what she had to say kuhusu wagombea wengine wawili aliogombea nao, na the rest of the political story

- To my shock, waziri mzima wa jamhuri na mwenye elimu kubwa kama alivyodai kuwa nayo, ametumia muda karibu wote kumzungumzia mgombea mmoja tu, yaani Mama Janet, kwa nini sio the other candidate? Huyu mbona hatajwi na wala hakutajwa kabisa? WHY?

- Anaponda elimu ya mgombea mwingine kwa misingi ipi hiyo? Kwani katiba ya UWT haikutimilika kwa kiwango cha elimu ya wagombea wengine wawili? Na kama elimu kubwa ni kigezo cha uchaguzi wake kwa mawazo ya huyu waziri kwa nini hakuulizwa kuwa ni kwa nini Mwandosya na Salim wenye elimu kubwa sana, walishindwa urais na Kikwete mwenye elimu ndogo sana kulinganisha na hao wawili? Sasa kwa huu muono wake wa elimu ndogo kuwa ni sawa na kuongoza in the 60s na 70s, anapowaangalia Salim na Mwandosya, huku Kikwete akiwa ndiye rais aliyeshinda ina maana anaongoza like in the 60s na 70s?

- Sophia ameshinda uchaguzi tayari na sasa yeye ni mwenyekiti, then why worry na taarabu zote alizozitoa kwenye ile interview? I mean sijawahi kusikia mshindi wa uchaguzi akipoteza muda mrefu kuimba taarabu over mgombea aliyemshinda badala ya kutumia muda ule kuweka muongozo wa nini anategemea kukifanya, na kujaribu kuwa-win wananchi wasiomfahamu kiuongozi, lakini huyu ameongea taarabu weeee for what hasa? Hajiamini nini? Na kwa nini hajiamini hasa? Mbona interview za Obama baada ya hatujaona akiimba taarabu?

We can go on and on, kuhusu what was right na what was wrong na her ugly personal conduct kwa sababu ndio hasa sababu ya kuwepo kwetu hapa JF, na ninaomba kusema wazi kwamba hata mimi nimesikitishwa sana na the arrogance ya huyu waziri kwenye hii interview, sisi wananchi wa hili taifa sio wajinga kama hawa viongozi wanavyofikiri na ukweli ni kwamba huyu waziri aambiwe wazi kuwa anahitaji kufanya interview nyingine ili aombe radhi wananchi wote waliomsikiliza kwenye hii ya kwanza, kwa sababu imemshusha sana hadhi kuliko kumjenga na pia imetushusha hadhi wote tuliomsikiliza, kama this is all she could offer as far as kujitambulisha who she is kwa wananchi tusiomfahamu kabisa!

Sijui kilichopita huko nyuma na comments za wananchi hapa kuhusu ile interview, lakini Damn! majibu ya huyu waziri yalikuwa ni kinyume kabisa na elimu anayodai kua nayo, infact kwangu mimi inaleta maswali mazito sana kama kweli anayo hiyo elimu kwa sababu nimewahi kusikia sana kutoka kwa wanaofanya naye kazi kwa karibu kuwa huwa ana tabia za kutojiamini, as the results huwa anakuwa na ukali flani una-amount to arrogance hivi wa kujikinga asisogelewe karibu na maswali mazito, na baada ya kusikiliza hii interview ni clear kuwa critics wake wako right tena kwa 100%.

Amejaribu sana ku-raise ishus ambazo ukweli ni kwamba sio za wanawake wetu wa bongo, labda wa majuu huku akijaribu ku-promote ideas ambazo sijui ni wananchi wangapi wa Tanzania tumewahi kuzisikia zikifanyiwa kazi na UWT. What is UWT anyways? Wamewahi kufanya nini hasa kwa taifa au kwa maendeleo ya kina mama wetu? Mimi nijuavyo huu siku zote umekua umoja wa ku-hang out tu kwa kina mama wake wa viongozi na wanawake wanasiasa wa ngazi za juu tu, na sasa kuingia bungeni kwa mwenyekiti na katibu wake, pamoja na CC, lakini kwamba umewahi kumsaidia mwanamke wa kijijini? Labda zitolewe dataz tuzione kwanza.

Otherwise, tunamtakia kila na kheri Auntie Sophia, na ushindi huu ila tu cha msingi ni kwamba ni haki yetu wananchi kuuliza maswali, tena ya kila aina maana sisi wote hatuna akili moja na hatutoki kwenye njia moja ya maisha, ninaamini zipo interview zilizofanyika na viongozi wengi sana hapa ambazo Sophia anaweza akapewa kama muongozo on how to behave hapa JF, lakini never before nimewahi kusikia this kind of interview, where kiongozi ametumia muda karibu wote kuzungumzia mshindani wake badala ya UWT, tena kwa lugha chafu na dharau, kwa hili ustaarabu ni kwa huyu waziri kurudi hapa na atuombe radhi wananchi, na there is nothing personal about it ila ni kuelimishana tu! Apunguze jeuri na dharau hivi hamuoni bingwa wa dharau Mkapa alipo sasa? Hawa ndio mimi huwa ninasema wanaishia kumharibia Kikwete, maana unaishia kujiuliza anakuwaje na ukaribu na viongozi wenye this kind of Sophia's behavior?

Anajigamba amesoma, sasa kina Mwandosya watasema nini?

Sauti ya umeme, wazee wa FMES!
 
Naomba nieleweshwe;
Kitu nachoshindwa kuelewa mimi ni kwamba, ili UWT iweze kumsaidia mwanamke ni lazima awe mwanachama wa CCM. Je wanawake wengine wakipata matatizo wanasaidiwa vipi na chama (kisichokuwa cha kisiasa) katika kutatua matatizo yao? Ina maana hakuna chama/jumuia ki/nyingine yenye clout/resources kama UWT? Kwenye hii karne ya ishir...i mean twenty first century, kama ni kumuendeleza mwanamke, kwanini maendeleo yatokee kichama?

Mimi naona hii imekaa kikura zaidi ya kimaendeleo, kwahiyo siamini msomi au ambaye hajasoma ataleta mabadiliko kwa wanawake zaidi ya kutafuta kura.

Mimi kuna vitu nimependa katika interview yake, ila ningependa tumsikie Janet Kahama kwanza. Mwanakijiji, mimi nitatoa mchango kwaajili ya interview ya Janet Kahama. You need to be fair, tupatie pande mbili hata kama kashindwa. Tifananishe pointi za aliyesoma na ambaye hajasoma.

Halafu, hivi Tanzania kuna njaa gani mtu unahongwa sijui laki kadhaa kwa kura (kama ni kweli). Hiyo laki kadhaa inamsaidia nini mtu?
 
Binafsi nilifikiria mahojiano Mwanakijiji anafanya na Nasma hamisi Kidogo.....FMES analysis yako imetulia.
 
Nikiri ya kwamba nimesikitishwa na kushangazwa sana na baadhi ya ukosoaji wa Mhe. Simba kufuatia mahojiano yangu naye siku chache zilizopita. Kilichonisikitisha zaidi ni jinsi gani baadhi yetu tuna angalia vitu ambavyo si vya msingi na kuviacha vya msingi; kilichonishangaza zaidi ni jinsi gani wengine wamekuwa wa kali kiasi cha wao wenyewe kuwa kile wanachomtuhumu Mhe. Simba.. arrogance!

Katika mahojiano yangu na watu mbalimbali (kama Dr. Migiro, Dr. Salim, na wengineo) sijawahi kujaribu kumtetea mtu yeyote kwa majibu yake. Hata hivyo katika hili la Mhe. Simba nimeona kilele cha kebehi na kina cha parapanda ya unafiki wa uongo. Wengi wamemhukumu Mhe. Sofia kwa ukali ambao haukustahili na umeenda zaidi ya ukosoaji wa kumjenga mtu!

Kwa hawa nina ujumbe ufuatao: Sikiliza!

BONYEZA HAPA KUSIKILIZA

With all due respect,Mkuu...labda ungetusaidia kidogo kutupatia mifano hai ya hao (naomba kukunukuu) "wenzetu ambao wanaongalia vitu ambavyo si vya msingi na kuach avile vya msingi".Nasema hivyo kwa sababu inawezekana kabisa kwamba kile ambacho kinaonekana si cha msingi kwako ni cha msingi kwao,and vice versa.

Halafu nimesoma kule kwa Michuzi nikakutana na maoni ya mtu mmoja ambaye inaelekea anaiheshimu KHLN kama ilivyo kwa wengi wetu.Sasa wasiwasi wangu ni kwamba iwapo wewe kama KLHN utaanza kukosoa au kutetea watu unaowahoji,hadhi ya chombo hicho muhimu inaweza kuathirika.Radio Tanzania na TVT (or whatever their latest names are) ni vyombo muhimu vya habari huko nyumbani kwa vile vinawafikia wananchi wengi zaidi.Lakini wakati mwingine umuhimu wa vyombo hivyo unakuwa overshadower,or rather tarnished,na taasisi hizo mbili zinavyopenda kua-ssume role ya judge,jury and prosecutor hususan katika ulingo wa siasa.

Kwa heshima na taadhima,na kwa nia nzuri kabisa,ningekushauri wewe na KLHN mtuachie sie wasikilizaji jukumu la kukosoa au kupongeza.Najua ushauri huo unaweza kutafsiriwa kama kukunyima HAKI yako kutoa maoni (wakati KLHN ni chombo chako binafsi na una uhuru wa kukiendesha unavyotaka) lakini HAKI HUENDANA NA WAJIBU,na wajibu wa KLHN sio tu kutupatia mahojiano motomoto bali pia kutoonekana inampendelea au kumuonea mhojiwa flani (kwa kumtetea au kumpinga mhojiwa nje ya studio).

Nimalizie kwa kusema kwamba waliotoa maoni hayo ni uthibitisho kuwa wameyasikia na kuwagusa.Watendee haki kwa kuheshimu mawazo yao badala ya kuyahukumu.Hiyo ndio audiance yako!
 
Naomba nieleweshwe;
Kitu nachoshindwa kuelewa mimi ni kwamba, ili UWT iweze kumsaidia mwanamke ni lazima awe mwanachama wa CCM. Je wanawake wengine wakipata matatizo wanasaidiwa vipi na chama (kisichokuwa cha kisiasa) katika kutatua matatizo yao? Ina maana hakuna chama/jumuia ki/nyingine yenye clout/resources kama UWT? Kwenye hii karne ya ishir...i mean twenty first century, kama ni kumuendeleza mwanamke, kwanini maendeleo yatokee kichama?

Mimi naona hii imekaa kikura zaidi ya kimaendeleo, kwahiyo siamini msomi au ambaye hajasoma ataleta mabadiliko kwa wanawake zaidi ya kutafuta kura.

Mimi kuna vitu nimependa katika interview yake, ila ningependa tumsikie Janet Kahama kwanza. Mwanakijiji, mimi nitatoa mchango kwaajili ya interview ya Janet Kahama. You need to be fair, tupatie pande mbili hata kama kashindwa. Tifananishe pointi za aliyesoma na ambaye hajasoma.

Halafu, hivi Tanzania kuna njaa gani mtu unahongwa sijui laki kadhaa kwa kura (kama ni kweli). Hiyo laki kadhaa inamsaidia nini mtu?

Yaani hujui njaa iliyoko Tanzania hadi kushangaa hongo ya laki kadhaa? Puh-leeaase!!! Are you that out of touch?
 
Wana JF naona mjadala sasa unataka kuharibika kwa dataz za kudhania vile.]

Okay...

Kama sijakosea waheshimiwa wengi sana wana degrees kutoka chuo cha Washington International - I think even Sofia Simba anayo ya huko

Well,you thought wrong.Community Economic Development from New Hampshire University.
Dataz za kudhania my foot!

Midahalo between candidates...way to go.
 
Yaani hujui njaa iliyoko Tanzania hadi kushangaa hongo ya laki kadhaa? Puh-leeaase!!! Are you that out of touch?
Bongo tambarareeee wewe hujui?
Naah, actually nauliza logic yake. Labda niulize kivingine; unapiga kura kama heshima ya kuhongwa, au shukrani itakusaidia mtaji? Tena hiyo laki nimepandisha, mbona imetajwa elfu kumi tu?
Nyani, mimi nimekaa kichwa kinanigonga, najiuliza. Leo unachukua laki moja...hiyo laki moja inakufikisha wapi? Break-it down for me!
 
With all due respect,Mkuu...labda ungetusaidia kidogo kutupatia mifano hai ya hao (naomba kukunukuu) "wenzetu ambao wanaongalia vitu ambavyo si vya msingi na kuach avile vya msingi".Nasema hivyo kwa sababu inawezekana kabisa kwamba kile ambacho kinaonekana si cha msingi kwako ni cha msingi kwao,and vice versa.

Halafu nimesoma kule kwa Michuzi nikakutana na maoni ya mtu mmoja ambaye inaelekea anaiheshimu KHLN kama ilivyo kwa wengi wetu.Sasa wasiwasi wangu ni kwamba iwapo wewe kama KLHN utaanza kukosoa au kutetea watu unaowahoji,hadhi ya chombo hicho muhimu inaweza kuathirika.Radio Tanzania na TVT (or whatever their latest names are) ni vyombo muhimu vya habari huko nyumbani kwa vile vinawafikia wananchi wengi zaidi.Lakini wakati mwingine umuhimu wa vyombo hivyo unakuwa overshadower,or rather tarnished,na taasisi hizo mbili zinavyopenda kua-ssume role ya judge,jury and prosecutor hususan katika ulingo wa siasa.

Kwa heshima na taadhima,na kwa nia nzuri kabisa,ningekushauri wewe na KLHN mtuachie sie wasikilizaji jukumu la kukosoa au kupongeza.Najua ushauri huo unaweza kutafsiriwa kama kukunyima HAKI yako kutoa maoni (wakati KLHN ni chombo chako binafsi na una uhuru wa kukiendesha unavyotaka) lakini HAKI HUENDANA NA WAJIBU,na wajibu wa KLHN sio tu kutupatia mahojiano motomoto bali pia kutoonekana inampendelea au kumuonea mhojiwa flani (kwa kumtetea au kumpinga mhojiwa nje ya studio).

Nimalizie kwa kusema kwamba waliotoa maoni hayo ni uthibitisho kuwa wameyasikia na kuwagusa.Watendee haki kwa kuheshimu mawazo yao badala ya kuyahukumu.Hiyo ndio audiance yako!

Mlalahoi... kitu kimoja ambacho ni lazima kuelewa ni kuwa mimi naongozwa na falsafa tofauti kabisa; chombo cha KLHN, mwanakijiji.com au Cheche za fikra siyo vyombo vya kutoa habari tu au kuripoti matukio fulani.. vyote hivyo vinalenga katika kufanikisha mabadiliko ya kifikra. Mojawapo ya vitu hivyo ni kuchochea mijadala ya fikara.

Katika utetezi wangu wa Sofia ni baada ya kuona kuwa mjadala juu yake ulibakia on the trivials..na siyo substance ya aliyoyasema na hasa yale ya msingi. Kuna ukosoaji unaoweza kufanywa na mtu yeyote.

Lakini zaidi utaona kuwa nimesema kuwa sina kawaida ya kumtetea mtu yeyote anayekuja kwenye show yangu, sijafanya hivyo kwa muda wa kuhoji karibu watu 50 ndani ya miaka hii mitatu. Hivyo nilichofanya ni kugeuka na kuwa editorial ambapo natoa maoni yangu kama mhariri pia. Nisingetenda haki kwa dhamira yangu kukaa kimya.

Kuna mambo ya kukosoa lakini mengine ukiyaangalia katika ile hoja ya kwanza kule kwa michuzi unaweza kusikitika. Na nakuahidi haitakuwa kawaida yangu kumtetea mtu niliyemhoji.

Hata hivyo utaona kuwa katika utetezi wangu sikutetea substance ya aliyoyasema hususan wajibu wake au yaliyojiri kwenye uchaguzi wao, nimetetea kile ambacho naamini was an unfair criticism leveled against her. Msisitizo uko kwenye "unfair". Sijasema hakustahili kuwa criticized kama vile mimi mwenyewe I'm open to criticism (fair or unfair).

Otherwise, pointi zako nimezizingatia...
 
Toka lini umeanza kuwa mtetezi wa mwanawake au uanamke? Vipi vyumba vya $ 10 kwa huyo?

tangu aliyenizaa alipokuwa mwanamke, na dada zangu walipozaliwa pamoja nami, na tangu nimpendaye naye ni mwanamke!

Kuhusu hilo la $10 sina sababu ya kujaribu kujibu kwa sababu hukusoma nilichosoma uliitikia tu kihisia kama mtu mwingine alivyofanya (which I'm used to anyway).
 
Back
Top Bottom