Mjenda Chilo
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 1,467
- 513
Wanaforum, watu wameshamwaga mboga sasa wakati wa kumwaga ugali ugali umefika. Kama tujuavyo Hosea ameahidi Chenge kupelekwa mahakamani baada ya DPP kukamilisha mchakato wa file. sipati picha jinsi kesi hii itakavyokuwa rahisi kwa Chenge. Yaani kwa TZ yetu ya leo, mtu ambaye amekuwa Mwanasheria mkuu wa serikali na Waziri kwa miaka lukuki yet ni kati ya wasomi wachache wa sheria wa kwanza akashindwa kujustify jinsi alivyopata hiyo hela kabilioni moja na ushee tu, mbona nachoka! Huyu jamaa kwa hesabu za karibu makusanyo yake ya posho halali ambazo kwa serikali yetu double payments zimekithiri ni ngumu sana kumbana. Fikiria Waziri akienda Mwanza kikazi si anapewa allowances, anazitumia wapi? wakati kila kitu anaandaliwa? Billion moja kwa waaziri bongo ni hela ndogo saana, na ndo maana Chenge alisema ni visenti tu, hiyo ni kweli kabisa, kama kuna mtu anadata za kupinga hili aweke mezani. Hapa hamna kesi yeyote, wasiwasi wangu labda ni umri tu ndo utamnyima fursa ya kurudi kwenye chart. Nafikiri pindi itakapofika wakati wa chenge wa kutoa ushahidi ndo tutajua kwanini watu wanauana kugombea ubunge na kuteuliwa uwaziri na inawezekana baada ya hapo wote tukaenda vijijini kwetu kuanza kuangalia jinsi gani ya kujiunga na ujasiriamali ulipao kupita maelezo. Mtaniambia.