waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?
waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?
Hivi kuna mtu alitarajia kusikia jambo lolote la kushtua kuhusiana na Richmond tena? Igizo hili lilimalizika rasmi Gire alipofikishwa Kisutu, subiri igizo jingine
Nahofia kusema kuwa viongozi wetu wanataka kucheza mchezo wa kisiasa katika issues muhimu. Wanataka kuvuta miguu mpaka mwakani (karibu na uchaguzi), halafu waanze kutumia mambo haya kuonyesha wanafanya jambo. Wakishachaguliwa wanayaweka kando tena. Nadhani wanacheza na wananchi.
Haiwezekani serikali uchukue muda mrefu kiasi hicho kwa mambo yaliyo bayana kiasi hicho. Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa ni pamoja na walau kusimamisha/kufukuza kazi viongozi wote walitajwa katika sakata hilo na ambao wako katika utumishi wa umma. Maana hadi sasa hakuna hatua hata moja iliyochukuliwa tangu mambo haya yaamuliwe na Bunge mwaka mmoja uliopita. Kama yapo naomba kufahamishwa.
Wasitumie mambo haya kisiasa, hayatawafaa hata kidogo. Nadhani hawajui tu kuchelewa kwao kutawanyima kura nyingi sana mwakani. Hata kama wataanza kuonyesha kuanza kuchukua hatua wakati huo wa kuomba kura.
Tume zilizoundwa zimefanya kazi kwa ukamilifu na kwa muda mfupi kuliko serikali ambayo ina rasilimali za aina zote zinazohitajika kukamilisha mambo haya. Je, wanataka tuamini kuwa Tume zinaweza kazi kuliko Serikali? Nadhani waanze kutupa matumaini kuwa kuchaguliwa kwao hakukuwa kwa makosa.
waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?