Utekelezaji wa mapendekezo ya Richmond hakuna lolote

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?
 
Itakuwa vizuri kama utatolewa muhtasari wa alichokisema au ikiwezekana basi ije copy ya hicho alichokisema.Vinginevyo uchangiaji(hasa kwa 'sisi' ambao hatujamsikia) itakuwa ni bendera fata upepo.
 
waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?

Kasema nini hasa? weka hata summary of what he has said......! vinginevyo hatutakusoma vilivyo!
 
Yeah ni vizuri na sisi ambao tupo mbali na radio kwa leo tupate alichokisema japo kwa ufupi.Kwaiyo Hosea na Mwanyika bado wanaendelea kupiga mzigo au????
 
waziri mkuu katoa taarifa bungeni sasa hivi kila kitu ni siasa na michakato inaendelea... hili ndio tunalotitaka?

Taifa la michakato, mchakato wa richmond, mchakato wa vitambulisho vya taifa, mchakato wa kumpata mwekezaji wa ATCL, mchakato wa TAZARA, mchakato wa kujua waliofuja richmond, mchakato wa JF ni kina nani, mchakato wa ...................
 
hamu yetu kubwa ilikuwa ni hatma ya maofisa wa serikali walituhumiwa katika ripoti. yeye kasema wameshapeleka maelezo yao na yanafanyiwa kazi na atakae patikakana na hatia atachukuliwa hatua za kinidhamu. mpaka sasa walikuwa wanafanya nini? tunachotaka ni utekelezaji na sio taratibu
 
Mkuu nadhani ni vyema tukafahamu kwa ufupi tuu amesema nini. ila katika hali ya kawaida nadhani tusitegemee makubwa maana hata Bible inasema kama ufalme utajifitini wenyewe basi ufalme umekwisha anguka.(weak). Tutegemee kuona porojo zilezile na kama hali ya kisiasa itaruhusu(political advantage), japo vikesi viwili vitatu hivi kuwazima watanzania.......
 
Hivi kuna mtu alitarajia kusikia jambo lolote la kushtua kuhusiana na Richmond tena? Igizo hili lilimalizika rasmi Gire alipofikishwa Kisutu, subiri igizo jingine
 
Nahofia kusema kuwa viongozi wetu wanataka kucheza mchezo wa kisiasa katika issues muhimu. Wanataka kuvuta miguu mpaka mwakani (karibu na uchaguzi), halafu waanze kutumia mambo haya kuonyesha wanafanya jambo. Wakishachaguliwa wanayaweka kando tena. Nadhani wanacheza na wananchi.

Haiwezekani serikali uchukue muda mrefu kiasi hicho kwa mambo yaliyo bayana kiasi hicho. Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa ni pamoja na walau kusimamisha/kufukuza kazi viongozi wote walitajwa katika sakata hilo na ambao wako katika utumishi wa umma. Maana hadi sasa hakuna hatua hata moja iliyochukuliwa tangu mambo haya yaamuliwe na Bunge mwaka mmoja uliopita. Kama yapo naomba kufahamishwa.

Wasitumie mambo haya kisiasa, hayatawafaa hata kidogo. Nadhani hawajui tu kuchelewa kwao kutawanyima kura nyingi sana mwakani. Hata kama wataanza kuonyesha kuanza kuchukua hatua wakati huo wa kuomba kura.

Tume zilizoundwa zimefanya kazi kwa ukamilifu na kwa muda mfupi kuliko serikali ambayo ina rasilimali za aina zote zinazohitajika kukamilisha mambo haya. Je, wanataka tuamini kuwa Tume zinaweza kazi kuliko Serikali? Nadhani waanze kutupa matumaini kuwa kuchaguliwa kwao hakukuwa kwa makosa.
 
Hivi kuna mtu alitarajia kusikia jambo lolote la kushtua kuhusiana na Richmond tena? Igizo hili lilimalizika rasmi Gire alipofikishwa Kisutu, subiri igizo jingine

you're right dude, Pinda amesema uchunguzi bado unaendelea...
 
Nahofia kusema kuwa viongozi wetu wanataka kucheza mchezo wa kisiasa katika issues muhimu. Wanataka kuvuta miguu mpaka mwakani (karibu na uchaguzi), halafu waanze kutumia mambo haya kuonyesha wanafanya jambo. Wakishachaguliwa wanayaweka kando tena. Nadhani wanacheza na wananchi.

Haiwezekani serikali uchukue muda mrefu kiasi hicho kwa mambo yaliyo bayana kiasi hicho. Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa ni pamoja na walau kusimamisha/kufukuza kazi viongozi wote walitajwa katika sakata hilo na ambao wako katika utumishi wa umma. Maana hadi sasa hakuna hatua hata moja iliyochukuliwa tangu mambo haya yaamuliwe na Bunge mwaka mmoja uliopita. Kama yapo naomba kufahamishwa.

Wasitumie mambo haya kisiasa, hayatawafaa hata kidogo. Nadhani hawajui tu kuchelewa kwao kutawanyima kura nyingi sana mwakani. Hata kama wataanza kuonyesha kuanza kuchukua hatua wakati huo wa kuomba kura.

Tume zilizoundwa zimefanya kazi kwa ukamilifu na kwa muda mfupi kuliko serikali ambayo ina rasilimali za aina zote zinazohitajika kukamilisha mambo haya. Je, wanataka tuamini kuwa Tume zinaweza kazi kuliko Serikali? Nadhani waanze kutupa matumaini kuwa kuchaguliwa kwao hakukuwa kwa makosa.

Narejea mahojiano aliyowahi kufanya Mwanakijiji na Dr. Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond. Nakumbuka akijibu swali kuhusu utekelezaji wa maazimio yaliyopitishwa na bunge, aliomba watu wasubiri ripoti ya serikali bungeni tarehe 6/2/2009.

Hii tarehe imepita na inaonekana serikali haikuweza kuleta ripoti inayojibu maswali kama ilivyotarajiwa. Kuna wengine tumekuwa "very cynical" kuhusu nia ya kweli ya serikali ya kushughulikia kashfa ya Richmond. Wengine tumeiita ripoti ya Dr. Mwakyembe kama aina ya usanii lakini kuna watu wamekuwa wepesi kutunyooshea vidole.

Kwa sasa ni dhahiri serikali imeonyesha ujeuri katika kuyadharau maazimio ya bunge na kuyapuuza. Natoa wito kwa Dr. Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond, kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuiwajibisha serikali kwa kitendo cha kulidhalilisha bunge.
 
Richmond: Serikali yasema Mwanyika, Hosea wanaweza kushtakiwa
Na Leon Bahati, Dodoma

SERIKALI imesema kuna uwezekano wa kuwafikisha mahakamani Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea ikibainika kuwa walikosea wakati wa kupitisha zabuni tata ya umeme wa dharura iliyoipa ushindi kamapuni ya Richmond.

Akitoa kauli ya serikali juu ya utekelezaji wa maazimio ya bunge kuhusiana na kashfa ya Richmond Development LLC, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema kuwa uchunguzi bado unaendelea dhidi ya vigogo hao.

“Kwa sasa kazi hiyo inayoendelea ni vyombo vya dola kufanya uchunguzi zaidi, ili kuona kama kuna makosa yoyote ya jinai yaliyotendwa,” alisema Pinda.

Alisema kuwa ripoti ya uchunguzi huo ndiyo itakayoipa serikali dira ya hatua za kuchukua, kama vile kupelekwa mahakamani au hatua za kinidhamu.

Mbali na vigogo hao wawili, Pinda aliwataja wengine ambao wapo kwenye uchunguzi kuwa ni Wakili wa Serikali, Donlad Chidowu na wajumbe wa kamati za wataalamu na majadiliano, ambazo inawahusisha maofisa waandamizi wapatao 12 kutoka wizara na taasisi za umma.

Alifafanua kwamba, taarifa ambazo vyombo hivyo vya dola inazifanyia kazi ni uchunguzi uliofanywa na mamlaka za nidhamu baada ya kuchambua maelezo ya mtumishi mmoja mmoja.

Hatua hiyo ya serikali inatokana na maazimio ya kikao cha bunge mwaka jana, kilichoitaka serikali kuwachukulia hatua watumishi wote waliohusika katika mchakato wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyoipa ushindi kampuni tata ya Richmond.

Katika hatua nyingine, Pinda alisema serikali ipo njia panda kutokana na mikataba mingi ambayo imeivunja na ambayo iko katika taratibu za kuvunjwa.

Pamoja na mkataba kati ya Shirika la Umma Tanzania (Tanesco) na Aggreko na Richmond ambao ulirithiwa na Dowans kuvunjwa, Pinda alisema kuwa wamefungua kesi mahakama za kimataifa pamoja na Mahakama Kuu ya Tanzania.

Pinda alifahamisha kuwa, mkataba wake na Kampuni ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL) pia ulikuwa kwenye mchakato wa kuvunjwa, lakini imeshindikana kutokana na wanahisa wake kufungua kesi mahakamani.

Hata hivyo, Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliikosoa kauli hiyo ya serikali kwa maelezo kwamba, haikuainisha kiasi cha tozo, ambacho kampuni ya Richmond na Dowans ilitakiwa kulipa kutokana na kuchelewesha kuzalisha umeme katika siku zilizokubaliwa.

Akisoma taarifa ya kamati, Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa (CCM) alikosoa mtindo wa serikali wa kuwaacha watumishi wa umma wanaotuhumiwa kuendelea na nyadhifa zao wakati wakichunguzwa, akidai kuwa ni rahisi kuingilia uchunguzi.

“Kamati inatoa maoni kwamba, uwajibishwaji wa watumishi hao upewe kipaumbele,” alisema Marombwa na kupendekeza kuwa zitumike taratibu za kuwasimamisha, kupewa likizo maalumu ama kuhamishwa ili kuepuka kuingilia uchunguzi.

Mwaka jana bunge liliagiza serikali kuwachukulia hatua zinazostahili Mwanyika na Hosea kutokana na kuifanya serikali iingie mkataba na kampuni tata ya Richmond pamoja na Takukuru kuusafisha mchakato uliowezesha kupatikana kwa kampuni hiyo, lakini baadaye kamati ya bunge ilibaini kuwa, ulikuwa na kasoro nyingi na kumfanya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu.
 
hi guys... kama ntapata ripoti ya jaji mark bomani kuhusu madini itakua ni kitu kizuri kwa kuanzia kulitathmini bunge lililopita na utekelezaji wake.. kwa yeyote mwenye copy ya ile ripoti i would appreciate kama ataipost humu
 
Back
Top Bottom