Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Tanzania Daima
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeweza kutawala taifa letu kwa muda huu mrefu na chaweza kuendelea kutawala kwa muda mrefu baadaye kwa kile ambacho nakitambulisha kwenu kuwa ni uchakachuaji wa demokrasia. Ndugu zangu, ninapozungumzia uchakachuaji wa demokrasia ninazungumzia mjumuisho wa taratibu, mikakati, mbinu, sheria, mipango na mfumo mzima ambapo kanuni za demokrasia zimechanganywa na kuharibiwa na kanuni za utawala wa kibabe, kimabavu au wa kiimla (kidikteta).
Demokrasia imechakachuliwa pale ambapo vitu ambavyo ni kinyume na demokrasia vimeingizwa ndani yake na kupitishwa kwa furaha kuwa ni demokrasia alimradi nchi inakwenda.
Wazo hili la kuchakachuliwa kwa demokrasia ni rahisi kuelewa kama utachukua muda kuelewa mojawapo ya mambo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa muda mefu kuhusu suala la mafuta ya magari kuchanganywa na mafuta ya taa au vitu vingine ili kuweza kuyapa wingi usiostahili ilikuweza kusababisha faida zaidi kwa wamiliki wa vituo vya mafuta.
Demokrasia nayo imechakachuliwa ili hatimaye kuongeza faida za haraka haraka kwa chama tawala. Mambo haya yamefanywa kwa makusudi na mtu yeyote anaweza kuyaona kwa urahisi endapo ayatasogelea akiwa na fikra huru na zilizo wazi.
Nitatoa mifano michache ili muweze kuona kuwa Tanzania hatuna demokrasia halisi bali tunayo ile iliyoingizwa kanuni za utawala wa kidikteta au wa kibabe.
Kwa muda mrefu tumekuwa tukililia uwepo wa tume huru ya uchaguzi. Na kwa muda mrefu serikali ya CCM imekataa kuweka utaratibu wa kuunda tume huru ya uchaguzi hasa kwa upande wa bara.
Matokeo yake ni kuwa tume ipo ya uchaguzi lakini haina uhuru ule tunaouhitaji kwenye demokrasia yaani kuanzia kuundwa kwake, ufanyaji kazi wake, bajeti yake n.k
Au tuangalie uundwaji wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Ukiangalia kwa haraka haraka unaweza kudhania kuwa ni ofisi huru lakini nayo ukiiangalia kwa karibu utaona kuwa nayo imechakachuliwa kwa kuingizwa vitu ambavyo ni kinyume na demokrasia. Kwa mfano, Mbunge wa CCM (chama tawala) ambaye ni waziri anayeshughulikia masuala ya kisiasa ana kauli katika masuala ya usajili wa vyama na utendaji wa sheria za gharama ya uchaguzi yeye akiwa ni mtu ambaye anaweza kuamua kiasi gani kitumike kwenye jimbo gani!
Au nitoe mfano mwingine ambao nina uhakika watu wengi hawaufahamu. Sheria ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura yanampa nguvu rais kuzuia gazeti au chombo chochote cha habari kuandika au kufanya kazi zake kwa sababu ya hali ya hatari ambayo yeye ndiye mtu pekee anayeweza kuitangaza.
Kwa mujibu wa sheria hiyo rais ana uwezo wa kidikteta siyo katika kuzuia tu hata kutaifisha mara moja vyombo hivyo.
Mfano mzuri wa jambo hili lilitokea Kenya ambapo wakati wa machafuko yaliyofuatia uchaguzi mkuu, Rais wa Kenya akitumia sheria kama ya kwetu aliweza kuzuia vyombo vya habari kutangaza kilichokuwa kinatokea wakati ule.
Sasa, mtu ambaye hana uwezo mzuri wa kufikiri japo anaweza kuwa ameenda shule na kuhitimua atasema kuwa hilo ni jambo zuri kwa sababu hatutaki vyombo vya habari vichochee watu kwa kutangaza yanayoendelea nchini wakati wa hali ya hatari.
Kwa maneno mengine, sheria yetu inataka wananchi waweke imani yao kwa asilimia mia moja kwenye mikono ya rais kuwa hatofanya jambo lolote baya na kuwa wananchi wasitake kujua serikali yao inafanya nini wakati kama huo.
Kidemokrasia hii ni sheria mbaya na ni kweli ni ya hatari wakati wa hali ya hatari. Ni mbaya kwa sababu demokrasia inataka wananchi wajue kile ambacho serikali yao inafanya wakati wote. Na hakuna wakati muhimu kwa wananchi kujua kile kinachofanywa kwa jina lao kama wakati wa hatari. Wakati wowote ule watawala wanaweza kufanya mambo kwa siri kwa kisingizio kuwa ni kwa ajili ya usalama wa taifa au kwa sababu ya hali ya hatari basi watawala wanakuwa hatimaye wamejipatia leseni ya kufanya lolote walipendalo kwani hakuna chombo kinachoweza kuandika habari hizo.
Wakati watawala wanaruhusiwa kufanya mambo wayatakayo wakiwa wanakingwa na tangazo la hali ya hatari historia imekuja kugundua mauaji yaliyofanywa na tawala mbalimbali katika majaribio ya kuzima ukimya.
Mfano mzuri ni tawala za Serbia wakati wa kuvunjika iliyokuwa Yugoslavia. Lakini ukweli ni kuwa demokrasia inahitaji vyombo huru zaidi vya habari wakati wa hali ya hatari kuliko wakati mwingine wowote.
Kwa sababu endapo katika wakati wa hatari hatuwezi kujua watawala wetu wanafanya nini itakuwaje wakati ambapo si wa hatari?
Demokrasia imechakachuliwa vile vile katika mojawapo ya mambo ya ajabu kabisa kuwahi kutokea nchini. Wakati CCM inaamini kabisa kuwa ipo haki ya msingi kwa mtu kuchagua na kuchaguliwa wameona kuwa mtu asiye mwanachama wa chama cha siasa anaweza kupiga kura kumchagua mtu mwingine lakini hawezi kufanya hivyo kwa yeye mwenyewe kuchaguliwa bila kuwa na chama cha siasa.
Yaani, wanaamini mtu asiye na chama ana akili na utimamu wa kuweza kuchagua na uchaguzi wake kuheshimiwa lakini linapokuja suala la yeye mwenyewe kuchaguliwa au kugombea tunaambiwa kuwa Watanzania hawana akili nzuri ya kuweza kutambua nani anawafaa au kujua mgombea mzuri hata asiye na chama! Huku ni kuchakachukuliwa kwa demokrasia.
Naweza kutolea mifano ya Bunge, Mahakama, Polisi, Usalama wa Taifa n.k katika kila sehemu nikaonesha pasipo jitihada kubwa ni jinsi gani kanuni za demokrasia zimechakachuliwa na kutufanya tuchanganyikiwe kama ndio demokrasia yenyewe au mfanano wake tu.
Fikiria wakati tunaaminishwa kuwa mahakama yetu iko huru ukweli ni kuwa ni huru kwa kadiri ya kwamba rais ameona ni huru, uteuzi wa majaji wake haufanyiwi usaili na wawakilishi wa wananchi na sote tunatakiwa tuamini tu kuwa rais anatuchaguliwa majaji wazuri!
Demokrasia imechakachuliwa nchini kiasi kwamba kama tungekuwa na uthubutu na ukali kama wa Wanyarwanda tungewarudishia demokrasia yao kwani haitufai.
Kama vile mafuta yanavyochakachuliwa na kusababisha matatizo kwenye magari (hata ya Ikulu!) ndivyo hivyo hivyo demokrasia inapochakachuliwa husababisha matatizo kwa watawala, naam hata Ikulu!
Wito wangu ni kuwa kama taifa tuna uamuzi wa kuamua kufanya kazi kwa kutumia demokrasia iliyochakachuliwa au kuanza kuisafisha na kukataa ili hatimaye tuwe na demokrasia ya kweli isiyo na nyongeza ya kanuni haramu za utawala wa kifisadi, kidikteta au kibabe.
Kwa vile tunafikiri (kwa ujumla wetu) kuwa demokrasia iliyochakachuliwa itafutikisha tunavyokwenda kama tunavyoamini kuwa mafuta yaliyochakachuliwa yanaweza kutufaa siku moja tutajikuta tunalipa gharama kubwa kwa sababu demokrasia hata siku moja haifanyi kazi inapochakachuliwa na inaweza kwenda tu kwa kiasi fulani lakini itafika mahali itakwama.
Siku itakapokwama ndipo tutajua kwanini mafuta yaliyochakachuliwa hayafai kwenye mashine kama vile demokrasia ilivyochakachuliwa haifai kwenye utawala. Hapo ndipo tutajua kuwa CCM inastahili lawama zote kama vile wamiliki wa vituo vinavyohusika na kuchakachua maisha.
Lakini yawezekana kama vile wachakachuaji mafuta hawapati adhabu kali ndivyo hivyo hivyo CCM hawaadhibiwi kwa sababu hatuoni hatari ya demokrasia isiyo demokrasia. Lakini tukitaka twaweza kuwaadhibu kama vile tunavyofanya haraka na hasira kuwaadhibu wenye vituo vya mafuta yaliyochakachuliwa.
La kwanza hata hivyo ni kuamini kuwa ninachosema ni kweli.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeweza kutawala taifa letu kwa muda huu mrefu na chaweza kuendelea kutawala kwa muda mrefu baadaye kwa kile ambacho nakitambulisha kwenu kuwa ni uchakachuaji wa demokrasia. Ndugu zangu, ninapozungumzia uchakachuaji wa demokrasia ninazungumzia mjumuisho wa taratibu, mikakati, mbinu, sheria, mipango na mfumo mzima ambapo kanuni za demokrasia zimechanganywa na kuharibiwa na kanuni za utawala wa kibabe, kimabavu au wa kiimla (kidikteta).
Demokrasia imechakachuliwa pale ambapo vitu ambavyo ni kinyume na demokrasia vimeingizwa ndani yake na kupitishwa kwa furaha kuwa ni demokrasia alimradi nchi inakwenda.
Wazo hili la kuchakachuliwa kwa demokrasia ni rahisi kuelewa kama utachukua muda kuelewa mojawapo ya mambo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa muda mefu kuhusu suala la mafuta ya magari kuchanganywa na mafuta ya taa au vitu vingine ili kuweza kuyapa wingi usiostahili ilikuweza kusababisha faida zaidi kwa wamiliki wa vituo vya mafuta.
Demokrasia nayo imechakachuliwa ili hatimaye kuongeza faida za haraka haraka kwa chama tawala. Mambo haya yamefanywa kwa makusudi na mtu yeyote anaweza kuyaona kwa urahisi endapo ayatasogelea akiwa na fikra huru na zilizo wazi.
Nitatoa mifano michache ili muweze kuona kuwa Tanzania hatuna demokrasia halisi bali tunayo ile iliyoingizwa kanuni za utawala wa kidikteta au wa kibabe.
Kwa muda mrefu tumekuwa tukililia uwepo wa tume huru ya uchaguzi. Na kwa muda mrefu serikali ya CCM imekataa kuweka utaratibu wa kuunda tume huru ya uchaguzi hasa kwa upande wa bara.
Matokeo yake ni kuwa tume ipo ya uchaguzi lakini haina uhuru ule tunaouhitaji kwenye demokrasia yaani kuanzia kuundwa kwake, ufanyaji kazi wake, bajeti yake n.k
Au tuangalie uundwaji wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Ukiangalia kwa haraka haraka unaweza kudhania kuwa ni ofisi huru lakini nayo ukiiangalia kwa karibu utaona kuwa nayo imechakachuliwa kwa kuingizwa vitu ambavyo ni kinyume na demokrasia. Kwa mfano, Mbunge wa CCM (chama tawala) ambaye ni waziri anayeshughulikia masuala ya kisiasa ana kauli katika masuala ya usajili wa vyama na utendaji wa sheria za gharama ya uchaguzi yeye akiwa ni mtu ambaye anaweza kuamua kiasi gani kitumike kwenye jimbo gani!
Au nitoe mfano mwingine ambao nina uhakika watu wengi hawaufahamu. Sheria ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura yanampa nguvu rais kuzuia gazeti au chombo chochote cha habari kuandika au kufanya kazi zake kwa sababu ya hali ya hatari ambayo yeye ndiye mtu pekee anayeweza kuitangaza.
Kwa mujibu wa sheria hiyo rais ana uwezo wa kidikteta siyo katika kuzuia tu hata kutaifisha mara moja vyombo hivyo.
Mfano mzuri wa jambo hili lilitokea Kenya ambapo wakati wa machafuko yaliyofuatia uchaguzi mkuu, Rais wa Kenya akitumia sheria kama ya kwetu aliweza kuzuia vyombo vya habari kutangaza kilichokuwa kinatokea wakati ule.
Sasa, mtu ambaye hana uwezo mzuri wa kufikiri japo anaweza kuwa ameenda shule na kuhitimua atasema kuwa hilo ni jambo zuri kwa sababu hatutaki vyombo vya habari vichochee watu kwa kutangaza yanayoendelea nchini wakati wa hali ya hatari.
Kwa maneno mengine, sheria yetu inataka wananchi waweke imani yao kwa asilimia mia moja kwenye mikono ya rais kuwa hatofanya jambo lolote baya na kuwa wananchi wasitake kujua serikali yao inafanya nini wakati kama huo.
Kidemokrasia hii ni sheria mbaya na ni kweli ni ya hatari wakati wa hali ya hatari. Ni mbaya kwa sababu demokrasia inataka wananchi wajue kile ambacho serikali yao inafanya wakati wote. Na hakuna wakati muhimu kwa wananchi kujua kile kinachofanywa kwa jina lao kama wakati wa hatari. Wakati wowote ule watawala wanaweza kufanya mambo kwa siri kwa kisingizio kuwa ni kwa ajili ya usalama wa taifa au kwa sababu ya hali ya hatari basi watawala wanakuwa hatimaye wamejipatia leseni ya kufanya lolote walipendalo kwani hakuna chombo kinachoweza kuandika habari hizo.
Wakati watawala wanaruhusiwa kufanya mambo wayatakayo wakiwa wanakingwa na tangazo la hali ya hatari historia imekuja kugundua mauaji yaliyofanywa na tawala mbalimbali katika majaribio ya kuzima ukimya.
Mfano mzuri ni tawala za Serbia wakati wa kuvunjika iliyokuwa Yugoslavia. Lakini ukweli ni kuwa demokrasia inahitaji vyombo huru zaidi vya habari wakati wa hali ya hatari kuliko wakati mwingine wowote.
Kwa sababu endapo katika wakati wa hatari hatuwezi kujua watawala wetu wanafanya nini itakuwaje wakati ambapo si wa hatari?
Demokrasia imechakachuliwa vile vile katika mojawapo ya mambo ya ajabu kabisa kuwahi kutokea nchini. Wakati CCM inaamini kabisa kuwa ipo haki ya msingi kwa mtu kuchagua na kuchaguliwa wameona kuwa mtu asiye mwanachama wa chama cha siasa anaweza kupiga kura kumchagua mtu mwingine lakini hawezi kufanya hivyo kwa yeye mwenyewe kuchaguliwa bila kuwa na chama cha siasa.
Yaani, wanaamini mtu asiye na chama ana akili na utimamu wa kuweza kuchagua na uchaguzi wake kuheshimiwa lakini linapokuja suala la yeye mwenyewe kuchaguliwa au kugombea tunaambiwa kuwa Watanzania hawana akili nzuri ya kuweza kutambua nani anawafaa au kujua mgombea mzuri hata asiye na chama! Huku ni kuchakachukuliwa kwa demokrasia.
Naweza kutolea mifano ya Bunge, Mahakama, Polisi, Usalama wa Taifa n.k katika kila sehemu nikaonesha pasipo jitihada kubwa ni jinsi gani kanuni za demokrasia zimechakachuliwa na kutufanya tuchanganyikiwe kama ndio demokrasia yenyewe au mfanano wake tu.
Fikiria wakati tunaaminishwa kuwa mahakama yetu iko huru ukweli ni kuwa ni huru kwa kadiri ya kwamba rais ameona ni huru, uteuzi wa majaji wake haufanyiwi usaili na wawakilishi wa wananchi na sote tunatakiwa tuamini tu kuwa rais anatuchaguliwa majaji wazuri!
Demokrasia imechakachuliwa nchini kiasi kwamba kama tungekuwa na uthubutu na ukali kama wa Wanyarwanda tungewarudishia demokrasia yao kwani haitufai.
Kama vile mafuta yanavyochakachuliwa na kusababisha matatizo kwenye magari (hata ya Ikulu!) ndivyo hivyo hivyo demokrasia inapochakachuliwa husababisha matatizo kwa watawala, naam hata Ikulu!
Wito wangu ni kuwa kama taifa tuna uamuzi wa kuamua kufanya kazi kwa kutumia demokrasia iliyochakachuliwa au kuanza kuisafisha na kukataa ili hatimaye tuwe na demokrasia ya kweli isiyo na nyongeza ya kanuni haramu za utawala wa kifisadi, kidikteta au kibabe.
Kwa vile tunafikiri (kwa ujumla wetu) kuwa demokrasia iliyochakachuliwa itafutikisha tunavyokwenda kama tunavyoamini kuwa mafuta yaliyochakachuliwa yanaweza kutufaa siku moja tutajikuta tunalipa gharama kubwa kwa sababu demokrasia hata siku moja haifanyi kazi inapochakachuliwa na inaweza kwenda tu kwa kiasi fulani lakini itafika mahali itakwama.
Siku itakapokwama ndipo tutajua kwanini mafuta yaliyochakachuliwa hayafai kwenye mashine kama vile demokrasia ilivyochakachuliwa haifai kwenye utawala. Hapo ndipo tutajua kuwa CCM inastahili lawama zote kama vile wamiliki wa vituo vinavyohusika na kuchakachua maisha.
Lakini yawezekana kama vile wachakachuaji mafuta hawapati adhabu kali ndivyo hivyo hivyo CCM hawaadhibiwi kwa sababu hatuoni hatari ya demokrasia isiyo demokrasia. Lakini tukitaka twaweza kuwaadhibu kama vile tunavyofanya haraka na hasira kuwaadhibu wenye vituo vya mafuta yaliyochakachuliwa.
La kwanza hata hivyo ni kuamini kuwa ninachosema ni kweli.