Utawala Bora Unapokwenda Likizo kwenye Mashirika ya Umma

Makyomwango

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
322
79
Wanabodi, tumeshuhudia na kujionea wenyewe mawaziri wakichukua maamuzi mbalimbali dhidi ya watendaji wakuu wa mashirika yaliyo chini ya wizara husika. Alianza Mwakyembe ATCL, akaja Kigoda na TBS, akafuata Profesor Mhogo na TANESCO na sasa tena Mwakyembe na Bandari.

Kwa wakati wote huo mawaziri hawa wamwkua wakichukua maamuzi mazito dhid ya watendaji wakuu huku wajumbe wa bodi wa taasis husika wakiachwa na kuendelea na majumu yao. Nijuavyo mimi, taasisi za umma hukabidhiwa kwa bodi za uongozi ambazo pamoja na mambo mengine zinatakiwa kufanya yafuatayo
  • Kutunga na kusimamia sers za taasisi
  • Kusimamia uongozi wa taaasisi na kuhakiki kuwa mipango mikakati ya taasis hizo inaandaliwa na kutekelezwa kwa ufanisi wha hali ya juu
  • Kuudhibi uongozi wa taasisi pamoja na mali za taasis
  • Kuteua watendaji wakuu wa taasis husika

Haya ni majukumu makubwa sana kwa bodi hizo na hivyo ufisadi unapotokea katika taasisi, ni wazi kuwa wajumbe wa bodi hizo wanakuwa hawajatekekeleza majukumu yao ipasavyo. Naamini kwamba kama tungekuwa na wajumbe wa bodi za uongozi wazalendo, walio makini na wenye uchungu na taasis hizo kamwe ufisida usingejipenyeza kwenye taasisi.

My Take
Kuchukua maamuzi magumu dhidi ya watendaji wakuu wa taasisi zilizovulunda na kuwaacha wajumbe wa bodi za uongozi kuendelea na majukumu yao waliyoyashindwa kuyatekeleza ni kuendeleza uozo ndani ya taasisi husika. Ni vyema bodi hizo zikavunjwa na ikiwezekana sheria zinazounda taasis hizo zirekebibishwe ili wajumbe wa bodi hizo nao waweze kuwajibishwa taasisi zao zinapovurunda.
 
Naamini uko sahihi kwa kiasi fulani.

Kwani wajumbe wa bodi husika wanapatikanaje? Taasisi nyingi za umma watendaji wakuu wana uwezo wa kushawishi nani ateuliwe kuwa mjumbe wa bodi. Bila shaka watapendelea wanaolinda maslahi yao.

Watu wameachwa wafanye wanavyotaka, hakuna anayejali!Hii ndio dhana ya shamba la bibi.,

Wakuu wa taasisi wanafanya wanavyotaka, hakuna anayefuatilia. Wanaiba, wanakula na kuvimbiwa! Hawana aibu wala hawajali. Dhaifu, hamuumi kwani naye ameamua kufanya biashara ukubwani, nao wanajua.

JF inatusaidia sana, pamoja na taasisi hizo ulizotaja, zipo nyingine nyingi tu,mfano Chuo Kikuu Huria, nitakuja na thread yake jamvini.Prof. Mbwete ameigeuza kama ofisi yake binafsi.Anakula mpaka anatapikia humo. Ameiga za Vasco, kila siku safari nje ya Nchi. Hata za binafsi anataka alipiwe na chuo. Aibu, anatumia staff wamjazie maiimprest yake ya wizi. Analazimisha mambo na ubadhirifu mkubwa wa mali na fedha, ukabila, kugawa vyeo na kulazimisha nafasi kinyume na utaratibu, na mengi mengine. Chuo hakisongi, staff wako hoi, idadi ya wanafunzi inazidi kupungua.

Mawaziri kibinafsi, wameona bora waonekane japo wamechulua hatua. Though, wanachofanya ni juhudi zao binafsi na sio uongozi wa pamoja! Dhaifu haumizi kichwa na nini:israel: kinachoendelea. Wakati mwingine nasikitika na kujiuliza iwapo kweli anajua anatakiwa afanye nini kama Rais! Pity!

Pro. Muhongo, anajitahidi, sana. Ushauri wangu kaza buti. Wananchi wanaelewa mazingira yako magumu ya kazi. Akikuvalisha spidi gavana, ni bora urudi chuoni ukafundishe.
 
Back
Top Bottom