Njoka Ereguu
JF-Expert Member
- Apr 7, 2012
- 821
- 335
Hivi watu wanataka kujua alikopelekwa Dkt. Ulimboka ili iweje? wale ambao yeye anataka wajuwe yuko wapi wanajua. Ingekuwa vyema kama tungekuwa tunaomba kufahamishwa anavyoendelea na siyo kuja na taarifa zenye vichwa vya habari kama hii. Tunajua fika kilichomtokea na hivyo ili kuendelea kumlida wasije mmalizia ni lazima anakotibiwa kuwe siri sasa kutaka kujua anatibiwa wapi sijui inakuja vipi. Wote tunafahamu anatibiwa na tunamwombea kwa Mungu apone haraka, hatuhitaji kujua anatibiwa wapi, tuanhitaji kumwona akiwa na nguvu na ari mpya katika kutekeleza majuku yake.