Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,604
- 3,163
Wana JF,
Nina leta taarifa hii kwenu ili kama kuna wahusika watasoma hapa basi wachukue hatua zinazostahili. Mchana huu nilipaki gari maeneo ya immigration karibu na jengo la UNDP la zamani. Ilinichukua kama dakika 15 kurudi na kukuta gari limefungwa chuma kwa maana ya kwamba nilipaki vibaya. Nikawauliza what is next wakaniambia lazima twende kwenye ofisi yao kule keko nikalipie faini ya Tshs. 28,000. Nikawakubalia na mmoja wao akapanda kwenye gari tukaelekea keko. Kufika Keko kwenye yadi yao story ikabadirika. Nikaambiwa inabidi nilipe hizo pesa hapo, halafu niache gari nirudi town centre kwenda kulipia faini jiji Tshs. 50,000.00. Alternatively, ili kurahisisha mambo nikaambiwa waniandikie gate pass, halafu nikalipe Tshs. 60,000 kwa mlinzi wao pale getini ili niachane nao.
Nilikuwa tayari nimechelewa kukutana na mtu na hivyo ni opt kulipia hizo Tshs. 60,000 bila risiti. Maamuzi hayo yalizingatia ukweli kwamba ningelazimika kukodi taxi kwenda ofisi za jiji mjini na kurudi na hiyo isingenigharimu chini ya Tshs. 30,000 halafu na muda ambao ningepoteza hapo njiani kwenda na kurudi Keko. Wanasema ukiisha kuja na risiti ya kulipia jiji ndipo
wanakuruhusu kuchukua gari yako.
Huu ni mpango wa makusudi kabisa wa kupata pesa za bure na kuliacha jiji bila mapato yake. Kwangu mimi yafuatayo yangeweza kufanyika kurahisisha process ya kulipia faini;
1. Waliponikamata nilikuwa hapo hapo jiji, ilikuwa ni rahisi kuniambia nilipie gharama ya jiji kwanza kabla ya kwenda huko Keko.
2. Hawa watu badala ya kumtaka mtu aliyefanya kosa kwenda kulipia sehemu mbili tofauti, pesa zote zingekuwa zinalipwa jiji kama ilivyokuwa zamani, na majembe wanapata % yao kutokana na makusanyo.
Sina uhakika kama uongozi wa jiji unaujua uozo huu unaofanywa na hawa maagenti wao. Napendekeza jiji litangaze utaratibu wa kulipia faini na kiwango kijulikane kwa kila mtu kuliko mtindo wa sasa ambapo unajikuta unalazimika kufanya wanachikitaka hawa majembe bila kujua kama hivyo ndivyo ilivyo.
Je haya yameisha mkuta mtu mwingine? Tufanyeje kukomesha tabia hii.
Tiba
Nina leta taarifa hii kwenu ili kama kuna wahusika watasoma hapa basi wachukue hatua zinazostahili. Mchana huu nilipaki gari maeneo ya immigration karibu na jengo la UNDP la zamani. Ilinichukua kama dakika 15 kurudi na kukuta gari limefungwa chuma kwa maana ya kwamba nilipaki vibaya. Nikawauliza what is next wakaniambia lazima twende kwenye ofisi yao kule keko nikalipie faini ya Tshs. 28,000. Nikawakubalia na mmoja wao akapanda kwenye gari tukaelekea keko. Kufika Keko kwenye yadi yao story ikabadirika. Nikaambiwa inabidi nilipe hizo pesa hapo, halafu niache gari nirudi town centre kwenda kulipia faini jiji Tshs. 50,000.00. Alternatively, ili kurahisisha mambo nikaambiwa waniandikie gate pass, halafu nikalipe Tshs. 60,000 kwa mlinzi wao pale getini ili niachane nao.
Nilikuwa tayari nimechelewa kukutana na mtu na hivyo ni opt kulipia hizo Tshs. 60,000 bila risiti. Maamuzi hayo yalizingatia ukweli kwamba ningelazimika kukodi taxi kwenda ofisi za jiji mjini na kurudi na hiyo isingenigharimu chini ya Tshs. 30,000 halafu na muda ambao ningepoteza hapo njiani kwenda na kurudi Keko. Wanasema ukiisha kuja na risiti ya kulipia jiji ndipo
wanakuruhusu kuchukua gari yako.
Huu ni mpango wa makusudi kabisa wa kupata pesa za bure na kuliacha jiji bila mapato yake. Kwangu mimi yafuatayo yangeweza kufanyika kurahisisha process ya kulipia faini;
1. Waliponikamata nilikuwa hapo hapo jiji, ilikuwa ni rahisi kuniambia nilipie gharama ya jiji kwanza kabla ya kwenda huko Keko.
2. Hawa watu badala ya kumtaka mtu aliyefanya kosa kwenda kulipia sehemu mbili tofauti, pesa zote zingekuwa zinalipwa jiji kama ilivyokuwa zamani, na majembe wanapata % yao kutokana na makusanyo.
Sina uhakika kama uongozi wa jiji unaujua uozo huu unaofanywa na hawa maagenti wao. Napendekeza jiji litangaze utaratibu wa kulipia faini na kiwango kijulikane kwa kila mtu kuliko mtindo wa sasa ambapo unajikuta unalazimika kufanya wanachikitaka hawa majembe bila kujua kama hivyo ndivyo ilivyo.
Je haya yameisha mkuta mtu mwingine? Tufanyeje kukomesha tabia hii.
Tiba