Utapeli mkubwa DSM: Beware

Katikomile

JF-Expert Member
Jul 12, 2007
471
74
Jamani Kuna utapeli mpya umezagaa katika jiji la Dar Es Salaam. Ambapo unaweza kupokea simu kutoka kwa mtu ambaye hukueleza data zote zinazoonyesha anakufahamu kweli kweli (including habari za ndugu zako, mahusiano yako na watu kadhaa, shule ulizosomea kama ni nje au seminar workshops etc). Kisha hujieleza kuwa anafanya Mashirika ya Kimataifa na kwamba ana deal. Kwa hiyo hukupa business proposal eti Shirika analofanyia (mfano UNHCR) wana vyakula vvinavyohitaji madawa kuvihifadhi ili visiharibike.

Aidha, husema maboss wake ni wazungu wapo Uganda, Kenya ama Sudan. Pia husema kuwa aliyekuwa anawa-supply madawa ameenda Marekani, Uingereza. Kwa hukuomba umpigie ili akupe details. Ukipiga simu hiyo itakuwa inaingia kwenye voice mail etc. Ukiwa-contact watakwambia subiri watafute mtu mwingine aliyekuwa anafanya shughuli hizo na yule wa Mwanzo. Baadaye watakutumia namba ya huyo mtu na kukutaka uje Dar kufuatilia deal hilo.

Wakati wote huo watasema fedha za kununua dawa hizo zipo. Hivyo watakwambia uwasiliane na contact person Dar ES Salaam ili akupatie sample uzipeleke airport (JKNIA). Sample ya chupa mbili za dawa inaweza kuwa $ 10,000 mpaka 12,000. Kama umeshaingizwa mjini (mfano 100 pcs @ $6,000 = $ 600,000 hukifikiria wewe hutanunua kwa $500,000) unaweza kuhaha kulipia $ 10,000 kwa ajili ya samples ukijua uta-win maisha baada ya kukamilisha deal.

Cha kushangaza watu hawa matapeli ukishalipa dola hizo say 10,000 unachukua sample ambazo ni kanyaboya (Uhuni mtupu hamna kitu). Ukitaka proof nenda Oysterbay Police utakuta machupa kibao ya aina hiyo ambayo watazania kibao wameshalizwa michuzi yao. Kwani ukiachana na huyo anayekupa sample ukifika airport humkuti mtu na simu zote zinakuwa hazipatikani.

Jamani kama kuna watanzania mnafikiri kuwa unaweza kuvuna bila kupanda acheni hizo. Ushahidi jamaa yangu ilibaki kidogo aliwe mchuzi wake machale yakamcheza akachukua askari kanzu pale O-bay polisi. Wakamkamata huyo kijana mmoja hapo MLIMANI CITY. Aliwekwa ndani kwa masaa na baadae nafikiri polisi nao walimtoka michuzi wakamuachia na kumwambia jamaa yangu hana kesi kwani alikuwa hajaibiwa. Naamini kuna watanzania kibao wameshalizwa.


Please if possible share this information.
 
Hao watu washawaliza wengi na hata majuzi tulitaka kuwakamata mitaa ya Sinza wakakimbia!

Mimi nimerecord hadi sauti yao! But if it is a police case ni rahisi kuwakamata through serial number za simu-handset. (baada ya registration ya simcard itakuwa rahisi through mobile number). Chukua simu yako, piga *#06# utaona serial number ya handset yako, hii ndo police wanatumia kuwapata wahalifu wasio wajanja, mhalifu mjanja atatumia call box ama simu yake then anaitupa, ama atatuma msg (ukituma msg kwenye mtambo wa simu serial number hai-display, ndo maana ilikuwa vigumu ku-trace wabaya wa Mwandishi Kubenea!).

Wahalifu wengi wanajisahau wanapiga simu then wanabadilisha simcard wakifikiri huwezi kuwapata! Atabadili line ya Tigo, Zain, Voda ama Zantel, lakini simu ni ile ile. Kama unakumbuka wezi wa CRDB Azikiwe, na NBC moshi walikamatwa kwa staili hii, baada ya waalifu kutupa simcard na polisi kuikota.

Kawaida polisi wanatumia serial number na kuangalia watu unaowapigia mara kwa mara, say mkeo/mmeo ama mtu yeyote wa karibu, then from there upelelezi unaanza!

Wanawatapeli wengi hawa watu hasa wakitegemea kwamba December ni mwisho wao baada ya simcard registration!

POLICE WAKIWA SERIOUS WANAWAKAMATA!
 
wakale wapi wakati maisha bora hayaonekani hadi sasa? Hichi ndicho kilichobaki katika jamii yetu, so we need to be aware about them
 
Kuna rafiki yangu mmoja (binti) wamempiga milioni moja na laki tisa.. alisubiri hapo Airport mpaka amekoma hakuna cha mzungu kutokea wala nini... na hela yenyewe alikua amekopa.
 
Kuna rafiki yangu mmoja (binti) wamempiga milioni moja na laki tisa.. alisubiri hapo Airport mpaka amekoma hakuna cha mzungu kutokea wala nini... na hela yenyewe alikua amekopa.

Bora hiyo 1.9m, mi jamaa yangu alikopa Dola 4,000 na zikapotea hivi hivi!
 
Sisi tumelizwa 1,300,000/= kwa njia hiyo hiyo uliyoelezea Mjasiliamali. Tena siyo waswahili kama unavyodhani kwani rugha wanayoongea ni kiingereza ambao ni watu weupe tena waliyoenda shule.
 
Kinachoshangaza ni kuwa hawa jamaa wanapata wapi hizi taarifa maana kwa mujibu wa wadau waliolizwa ni kuwa wanakutajia mpaka namba ya nyumba unayoishi na ikiwezekana mpaka kodi unayolipa na TV uliyonayo kama ni Samsung ama Hitachi bila kusahau birthday ya mdogo wako aliye boarding.... Kwa Dar es salaam huu ni zaidi ya utapeli.

Kinachonishangaza ni kuwa kesi kama hizi zimeripotiwa nyingi tu hapo central na inawezekana baadhi ya watuhumiwa wanafahamika lakini bado huu mchezo unaendelea.Mpaka siku akilizwa waziri ama mbunge ndio watashtuka.
 
Kaaazi kweli kweli kwa wale wasiopenda kufanya kazi bali kufikiria tu michongo.
 
Kinachonishangaza ni kuwa kesi kama hizi zimeripotiwa nyingi tu hapo central na inawezekana baadhi ya watuhumiwa wanafahamika lakini bado huu mchezo unaendelea.Mpaka siku akilizwa waziri ama mbunge ndio watashtuka.

Mbona majuzi tu nasikia alitaka kulizwa mtoto wa mkuu wa Kaya, Ridhiwani Kikwete, ngoma ikaisha kinamna pale Oysterbay police!
 
Kinachoshangaza ni kuwa hawa jamaa wanapata wapi hizi taarifa maana kwa mujibu wa wadau waliolizwa ni kuwa wanakutajia mpaka namba ya nyumba unayoishi na ikiwezekana mpaka kodi unayolipa na TV uliyonayo kama ni Samsung ama Hitachi bila kusahau birthday ya mdogo wako aliye boarding.... Kwa Dar es salaam huu ni zaidi ya utapeli.

Kinachonishangaza ni kuwa kesi kama hizi zimeripotiwa nyingi tu hapo central na inawezekana baadhi ya watuhumiwa wanafahamika lakini bado huu mchezo unaendelea.Mpaka siku akilizwa waziri ama mbunge ndio watashtuka.

Na ndio maana wanawapata wengi kirahisi! Kukufuatilia mbona IZE tu! wanatumia watu wako wa karibu, ndugu yako awe mdogo wako mfanyakazi ama popote wanapoweza kupata info zako! Anayetoa info ama nae akuwa part ya deal ama bila kujua!
 
deal yoyote inayolipa zaidi ya mara mbii ya fedha uliyoinvest ni WIZI, UTAPELI ama HARAMU. ukiona pesa nyingi zinajipanga mbele yako ujue umekaribia kupoteza fedha nyiingi. think twice mtu anakupa deal kama hiyo wakati wewe hufanyi biashara kama hizo, labda na wewe utapeli na UFISADI ndiyo zako. chunga sana usije ukakopa kwa mshkaji eti kuna bonge la deal!! utauza mpaka makochi
 
Dah mm kuna kakaangu kaingizwa mjini juzi juzi hapa yaani walimtoa Mbeya wakaja kumtapeli Bagamoyo $25,000 hivi hivi ili fika kipindi jamaa wanamkamua anaishiwa anarudi tena Mbeya kukopa mke wake anamzuia lakini wapi anasema kuna bonge la dili mm mara ya mwisho nilimwona Sinza nikataka kumwokoa kwa kumpigia cmu akiwa na hayo matapeli jamaa alikana kama yupo Sinza dah nilichoka sana wakati namwona kabisa ana katisha barabara baada ya masaa 4 kupita ananipigia cmu ndio nilikuwa mm.
 
Sure rafiki yangu kapigwa lk tisa akaja kunikopa laki saba ndo nikamshtua ni utapeli,akagoma akawaomba wawasiliane nae end of month atawalipa,ameenda airport ni michupa feke kuanzia saa saba mchana till kumi na moja jioni ndo anamini ameshaliwa ndogo!!
 
maisha magumu mkuu ndio maana watu wanabuni mbinu za kujiongezea kipato, na kama utagundua hawawaibii walala hoi, so sio mbaya wanagawana uamskini, ilaa tuwe makini na hizo njia mpya za utapeli
 
Back
Top Bottom