DEVINE
JF-Expert Member
- Mar 11, 2011
- 536
- 86
Jana kuna mchungaji mmoja katika mahubiri yake huwa anachangamsha sana waumini wake,kwa mfano utakuta katikati ya mahubiri utasikia "..Muambie jirani yako..Yesu anakupenda!" basi kwa furaha na mbwembwe kila mtu atamuambia jirani yake,kisha mchungaji anasema "pokea upendo wa bwanaa!"..Sasa jana mchungaji alikuwa anahubiri kuhusu wanawake wasiopata watoto,sasa katikati ya mahubiri akasema "...Muambie jirani yako,mwaka huu utapata mimba!" bila kujali watu wamekaa na nani jirani wengi tulikaa kimya kwani unakuta umekaa na mwanaume mwenzio.Mara ikasikika tu mtu kapigwa kofi huko nyuma alafu mtoto akaanza kulia ile tunageuka tunakutana na baba akimwambia mwanae wa kiume "..Ukome!".Watu wote kanisani mbavu hatuna kwa kicheko.