Jamani hodi humu jamvini!
Huenda swala hili limeshaongelewa huko nyuma ... mimi sijui maana mie ni mgeni. Lakini ni katika kutafuta ufahamu. Je UTANI kati ya makabila ulitokana na nini? Japo dhana hii ina mwelekeo wa kizamani / wa kale ukizingatia juhudi zilizofanyika na zinazoendelea kufanyika kuelekea kwenye utaifa ikiwa ni pamoja na ndoa za watu wanaotoka makabila tofauti , lakini haimaanishi kutotafuta jinsi jamii tofauti zilivyoweza kupatana na kuishi katika msingi na mifumo fulani fulani. Hivyo kwa sasa tuongelee utani kati ya makabila. Je ulitokana na nini? Haya makundi yalichaguana vipi kuwa watani? Je hii ni dhana ya huku kwetu Tanzania tu au na kwingineko ipo?
Huenda swala hili limeshaongelewa huko nyuma ... mimi sijui maana mie ni mgeni. Lakini ni katika kutafuta ufahamu. Je UTANI kati ya makabila ulitokana na nini? Japo dhana hii ina mwelekeo wa kizamani / wa kale ukizingatia juhudi zilizofanyika na zinazoendelea kufanyika kuelekea kwenye utaifa ikiwa ni pamoja na ndoa za watu wanaotoka makabila tofauti , lakini haimaanishi kutotafuta jinsi jamii tofauti zilivyoweza kupatana na kuishi katika msingi na mifumo fulani fulani. Hivyo kwa sasa tuongelee utani kati ya makabila. Je ulitokana na nini? Haya makundi yalichaguana vipi kuwa watani? Je hii ni dhana ya huku kwetu Tanzania tu au na kwingineko ipo?