Ni bora jamii iweze kutafakari kwa kina na upeo mkubwa kwamba ivi nani hasa anapaswa kuliongoza Taifa. Swala la msingi hapa ni kumtafakari kiongozi ambae anaweza kujinadi hadharani kwa ushahidi wa wazi kuwa amelifanyia nini Taifa aliloliongoza. Vilevile kiongozi anaejinadi kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kuliongoza taifa kwa kuahidi mambo kadhaa, swala la msingi hapa la kujiuliza , je ana mikakati gani inayoweza kutekelezeka na yenye uhalisia atatumia kufikia malengo yake katika kuleta maendeleo ya kweli ndani ya jamii husika.