Utamaduni wa wahaya na kifo cha kanumba

nimejifunza kiasi kuhusu mila za kihaya.sielewi kwa nini watu wanapenda kuwasema vibaya wahaya.kwani nina rafiki yangu ameolewa na muhaya,alivyoulizwa mume wako ni kabila gani,alivyotaja muhaya,watu waliguna.yeye ni mtu wa morogoro
 
Mkuu walionitangulia wamejibu sahihi na napenda niwashukuru kwa kuweza kuuelezea ukweli halisi

Vinginevyo labda kama ni matatizo ya familia make migogoro iko popote pale lakini uhayani tunatambua kuanzia mke mpaka watoto na kila kitu kuhusu watu hawa upande wa baba ndo alfa na omega.



Mwakola waitu,(nyegela)karibu uhayani.
 
mimi navyojua kwa mila za kihaya kwasababu mimi mhaya pia, mwanamke akiolewa anakuwa part and parcel ya familia ya mwanaume hata akifa atazikwa kwa mwanaume si kwao.
Mtoto akifariki anazikwa kwenye upande wa mwananume si mwanamke.
Kuonesha msisitizo kipindi cha nyuma ilikuwa mwanaume hawezi kulala kwao mwanamke mila zilikuwa haziruhusu kabisa utaenda utembee hata kama ni saa 5 usiku itakubdi uondoke ukalale pengine.
Nakuongeza kuwa kutokana na mgogoro wa familia ulikuwepo baina ya kanumba na baba yake labda kwa kutotumia busara wameshindwa kumshirikisha baba yake kanumba kwenye huu msiba wa mwanae.
Hata mimi nilishangaa kumwona babake kanumba anahojiwa tbc anaongea mambo ambayo ni tofauti na tuliyo ambiwa na akina ray na pia hata kamati ya mazishi inasema aliyekuwa anasubiliwa ni mama hata baba hajamtaja.
sitaki judge lakini ukweli hii si mila ya wahaya huu ni mgogoro wao binafsi ambao nahisi utakuja waletea matatizo.

Wakola waitu!!!
 
nimejifunza kiasi kuhusu mila za kihaya.sielewi kwa nini watu wanapenda kuwasema vibaya wahaya.kwani nina rafiki yangu ameolewa na muhaya,alivyoulizwa mume wako ni kabila gani,alivyotaja muhaya,watu waliguna.yeye ni mtu wa morogoro

Ni mtizamo tu wa mtu binafsi dada Kisukari!
 
watani naona mmejaribu kuelezea vizuri sana tena bila hata hasira. Mimi nimeelewa lkn naona ktk huu msiba pia kuna motive ya mali za marehemu. Baba kanumba naye ameweka msiba Shinyanga hapo sasa. Refer hiyo kideo iliyotupwa humu na mdau.
 
nahisi huu msiba utazusha mgogoro mkubwa wa kifamilia. Jana nlimwona baba yake kanumba akisema inabidi maiti ya mwanaye ipelekwe shinyanga ili akakabithi jina la kanumba ambalo alirithi kwa babu yake. Lakini nahisi haitakuwa hivyo.
hapa kuna utata kweli lakini tuiachie familia.

Makabira mashuhuri hapa tz hayaishwi kusemwa jamani.
 
yakheee msituchanganye hapooo
hakuna cha mhaya, mpogoro wala mpemba hapooi, cha msingi ni kuzikwa kwa hiyo maiti tuu na kuipumzisha salama kwa amani,
na zaidi nyie kama familia ya kanumba oneni ufakhari kwa huo msiba wa ndugu yenu kuhudhuriwa na umati wa watu wengi kuliko kuupeleka mwili huko mbali, wengine hawatoafford kufika hukoo, na badala yake mumkoseshe marehemu haki zake za kuhudhuriwa kwa umati wa watu, pengine huko mazishi yake yatapata watu mia moja tuu ila kwa hapo dar umati lukuki utafurika, na kwa sie waislam twasema kuna masharifu, kwenye umati wa watu huenda wakamwombea ikapungua adhabu na huenda akawa mja wa peponi
Aamin,

For more info visit me on my blog
PEMBA N'KWETU & follow me also on twitter
Kakytee AHMED MPEMBA (@Kakytee) on Twitter
 
Kumbe frustration zinapimwa kwenye sred?

Basi hiyo ndo my very romatic language niliyoiibua uvunguni mwa moyo.

back to the topic.

Hata kama mama alikuwa wa kwanza kujulishwa, bado baba kama kapewa taarifa alitakiwa kuhudhuria tu.

Kama mzazi anaweza kuzira msiba wa mwanae inakupa idea ya aina ya mtu mwenyewe 'kisasi'

kama ana kisasi hadi cha msiba, kisasi cha kumlea kitakuwa kilikuwaje?

Kiafrika, msiba huondoa tofauti zetu hata kama ni kinafiki.

We mama mbona una frustrations sana leo? Mbona mama alipigiwa simu fasta? Kwa mtu mwenye akili baada ya msiba kutokea baba ndio anakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kwa kuwa ndio Decision maker. Huenda amewaachia wahaya wajifagilie kwanza yeye atatinga siku ya kumpumzisha. Hata namna ya kifo inareflect kuwa jamaa hakupitia malezi mazuri.

RIP The Great Kanumba, the Shinyanga boy
 
Kumbe frustration zinapimwa kwenye sred?

Basi hiyo ndo my very romatic language niliyoiibua uvunguni mwa moyo.

back to the topic.

Hata kama mama alikuwa wa kwanza kujulishwa, bado baba kama kapewa taarifa alitakiwa kuhudhuria tu.

Kama mzazi anaweza kuzira msiba wa mwanae inakupa idea ya aina ya mtu mwenyewe 'kisasi'

kama ana kisasi hadi cha msiba, kisasi cha kumlea kitakuwa kilikuwaje?

Kiafrika, msiba huondoa tofauti zetu hata kama ni kinafiki.

Safi sana kongosho bahati mbaya natumia simu ngekugongea like.
Mara nyingi nakubari sana michango yako thou sometimes .......
 
pengine marehemu kutokana na ugomvi aliokuwa nao na baba yake aliwahi kutamka kitu kwamba hata nikifa asihusishwe wala nisizikwe kwake,kama jinsi mwanamke anavyoweza pata shida na mume akaishia kusema nikifa nizikwe kwetu na ndio kitakachotekelezwa kwa hyo pengine alichagua hvyo
 
mimi nijuavyo mahali pa kuzika inategemea ndugu wa karibu wako wapi!mimi sioni kwa nini azikwe dar wakati mama yupo bukoba,wamuage tu akapumzishwe nyumbani kwa mamaye,hata angekuwa mtoto wangu ningependa 2 azikwe nilipo once in a yl i will remember my child n in his memory i wil need to do smthing like putting roses and all that just for comfort
 
Kwetu uhayani mke anaitwa 'mukyala' (meaning mgeni/aliyekuja kutembea), kwetu mwanamke akiolewa ndo imetoka hiyo kwao atakuja 'kutembea' tu. Hata iweje akifariki atazikwa kwa mmewe hata kama walishaachana.Actually zamani kwetu mke angeweza kuachika na bado mtoto atakayezaa na mwanaume mwingine atakuwa ni wa former husband (anaitwa 'omwana webisisi). The same applies kwa watoto,watoto wako kwenye himaya ya baba hata kama walizaliwa na kukulia ujombani(bunyinarumi). Ndio maana kama ingetokea Mungu hajamchukua Kanumba kikwetu kama angeamua kuoa baba yake ndiye angemuolea (okumushwelelela) nandiye angemkabidhi mkuki (sio wajomba).
Nawapa pole sana wafiwa wote,Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.
RIP Steve,tulikupenda Mungu amekupenda zaidi.

Bishanga be serious kidogo hapo kwenye red pliiiz! Na je kama mume alishaoa mke mwingine bado ex-wife atazikwa kwa ex-hubby tu???oyaaaa hizi mila zenu ngumu sana bana.
 
Nilichojifunza kwa muda niloishi hapa duniani hapa Tz watu wakioana kabila tofauti ni ngumu saaana kufuata mila za kwao. Which is safe to me. Mambo yanaendeshwa ki western zaidi na decision nyingi zinafuata convenience. Hapo ndo naona faida za kuolewa na kabila lengine kwani mila zao hawezi kuzileta ndani na mimi za kwangu zinabaki kwetu. Mfano hata mimi nikienda kwa wakwe zangu sijawahi hata siku moja kuendekeza kujifunza mila zao nachukulia kuwa wa kabila lengine kama excuse na wao wala hawa demand ni behave their way.
 
Aisee mimi nilikuwa najiuliza inakuwaje hawa wasanii wanaongelea mipango ya harusi kwa kumshirikisha mama wakati yeye amesema baba yake yupo na hawana ugomvi? Pacho mwamba alipoulizwa na ile TV ya mchangani tv mawingu kuhusu haki za Kanumba akasema mama yake ndio atachukua. Sidhani kama baba ya Kanumba ametendewa haki, hii ni kwa kuwa wanawake wakiachwa huwa wanawajaza uongo watoto kuwa baba ndiye mbaya kuficha upuuzi walioufanya ukasababisha ndoa kuvunjika. Mtoto asipochanganya na zake anaishia kumchukia au kumdharau baba yake

Usiandike pumba, kama huna la kuchangia kaa kimyaa! Kwahiyo ni wanawake tu ndio husababisha ndoa kuvunjika?!!? Una uhakika gani kama Kanumba alijazwa ujinga na mama yake(kama unavyodai)?
Tatizo la watu kama wewe huwa mnafikiri kuwa watoto hawaelewi,kwa taarifa yako kama hujui watoto wanasoma picha yote ya maugomvi yenu na wanajua fika kuchanganua nani mbaya nani mzuri hata umjaze ujinga wa aina gani!!!! Siku zote ukweli huwa unajitenga piga ua.....hata ajazwe pumba gani,kuna siku atakuja kuujua ukweli wote na ndio hapo atakapomchukia muhusika iwe mama/baba.
 
Oku mwishelelia. Wamachame wanawake ni hatari sana wanawaua wa ume zao kisa wamiliki mali kama kuna mpalestina hapa akanumba hili nimpe data za ukweli na uhalisia. Qro maa.
 
Kwetu uhayani mke anaitwa 'mukyala' (meaning mgeni/aliyekuja kutembea), kwetu mwanamke akiolewa ndo imetoka hiyo kwao atakuja 'kutembea' tu. Hata iweje akifariki atazikwa kwa mmewe hata kama walishaachana.Actually zamani kwetu mke angeweza kuachika na bado mtoto atakayezaa na mwanaume mwingine atakuwa ni wa former husband (anaitwa 'omwana webisisi). The same applies kwa watoto,watoto wako kwenye himaya ya baba hata kama walizaliwa na kukulia ujombani(bunyinarumi). Ndio maana kama ingetokea Mungu hajamchukua Kanumba kikwetu kama angeamua kuoa baba yake ndiye angemuolea (okumushwelelela) nandiye angemkabidhi mkuki (sio wajomba).
Nawapa pole sana wafiwa wote,Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.
RIP Steve,tulikupenda Mungu amekupenda zaidi.

Hii kali nimeipenda...kiafrika zaidi....natamani hizi mila zirudi tena
 
Back
Top Bottom