Viongozi wastaafu na walioko hapa nchini wamekuwa matajiri ghafla mno. mathalan, wanamiliki viwanda vikubwa vya sukari,mashirika ya ndege, mabenki, mahoteli, majengo makubwa ya ghorofa nk. Ukichunguza sana utajiri wao utaona umepatikana kutokana na mojawapo ya vianzo hivi vya kifisadi:
- Ten au twenty percent kutoka kwenye mikataba ya madini na uwekezaji na uuzaji mashirika na makampuni ya umma.
- Fedha za EPA na Income Suport
- Michango ya wahindi kukisaidia chama (CCM) kwenye kampeni za uchaguzi nk
- Ufisadi kwenye fedha za miradi mbali mbali ya maendeleo ndani ya Halmashauri za miji.mfano,ujenzi wa barabara,shule, hospitali nk.
- Rushwa kubwa kubwa na ndogo ndogo huko TRA kwa wafanyakazi wa TRA.
- Biashara ya madawa ya kulevya, biashara hii inaendeshwa na viongozi waliomo serikalini na katika chama tawala.
- Safari za nje kwa viongozi wa serikali
- Posho mbali mbali za vikao
- Ufisadi kwenye zabuni mbali mbali za miradi na matumizi ya serikali.