Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
- Thread starter
- #221
Yote ni feki kuanzia unywele hadi unyayo. Nyumba hadi mwanamke aliyekuwa naye vyote feki tu.
Aisee wewe ni mzuri, naomba nisifie uumbaji wa Muumbaji
Yote ni feki kuanzia unywele hadi unyayo. Nyumba hadi mwanamke aliyekuwa naye vyote feki tu.
Suala la msingi hapa ni kufuatilia kujua kwa nini gari alilokuwa nalo namba zake ni batili, kwa maana kuwa namba hiyo hiyo inatumiwa na gari la mtu mwingine. Hali hii imeshamiri sana hasa katika mkoa wa Mbeya.
Sioni tatizo kwa yeye kuwa na nyumba za gorofa. Hivi ni kweli kuwa na gari tatu, nne tano au kumi ni utajiri? Hii ndiyo tafsiri ya utajiri kwa Tanzania? hizo nyumba hata tathmini hazifanyiwa kuweza kuestablish value zake lakini tunarukia tu huyu ni tajiri. Gari kuu kuu zinauzwa kwa fedha kidogo sana.
Umeeleza vizuri kuwa ana malozi ya mizigo yanayofanya biashara na bado unauliza hizo fedha amepata wapi? Tusitishe watu kuwa waoga wa kujiletea maendeleao kwa kigezo kuwa mishahara yao haiendani na mali walizo nazo. Si wote wameanza kazi wakiwa hawana kitu. Usimjaji mtu kwa kujiangalia wewe unapoanzia, kila moja ameanzia katika ngazi tofauti. Wapo walioanza kazi zao wakiwa na biashara tayari.
Haya mambo ni ya kawaida sana kwa polisi. Kuna mjomba wangu mmoja aliwahi kuuziwa gari na watu fulani kule Moshi na alipouliza wapi kadi ya gari aliambiwa tunakutuma Dar ukamuone IGP fulani enzi hizo(jina nalihifadhi)atakupatia hiyo kadi basi huyo mjoma akaja akafikia kwangu.
Asubuhi akaniomba nimpeleke kwa huyo IGP, baada ya kuingia ofisini kwake alijitambulisha na akapokelewa kwa furaha sana na chai juu,akaandikiwa kiji-note aende kwa mkuu wa trafiki na vehicle inspector ambapo alipewa kibali cha usajili.
Tukaondoka hapo ofisini na baada ya siku chache mjomba wangu akapata kadi akasafiri zake kwenda Moshi. Hadi hivi leo ile gari ambayo ilikuwa mpya anayo na huwa anakuja nayo hapa Dar bila tatizo.
Hiyo ndiyo Tanzania jamani, mjenga nchi ndio mbomoa nchi.[/jadchiko
haya mambo ni ya kawaida sana kwa polisi. Kuna mjomba wangu mmoja aliwahi kuuziwa gari na watu fulani kule moshi na alipouliza wapi kadi ya gari aliambiwa tunakutuma dar ukamuone igp fulani enzi hizo(jina nalihifadhi)atakupatia hiyo kadi basi huyo mjoma akaja akafikia kwangu.
Asubuhi akaniomba nimpeleke kwa huyo igp, baada ya kuingia ofisini kwake alijitambulisha na akapokelewa kwa furaha sana na chai juu,akaandikiwa kiji-note aende kwa mkuu wa trafiki na vehicle inspector ambapo alipewa kibali cha usajili.
Tukaondoka hapo ofisini na baada ya siku chache mjomba wangu akapata kadi akasafiri zake kwenda moshi. Hadi hivi leo ile gari ambayo ilikuwa mpya anayo na huwa anakuja nayo hapa dar bila tatizo.
Hiyo ndiyo tanzania jamani, mjenga nchi ndio mbomoa nchi.
Mbona tumali twenyewe tudogo? Kaulizie mali za kamanda mstaafu SHIMBONI au wasiliana na Invisible akupe diteili uzimie!
Yah,huyu Mzee alipambana sana, he deserved hivo vitu, familia yake haijaviendeleza kuna mashamba yake Geita na kiwanja Mwanza hakijajengwa mpaka leoumesema kweli kabisa kuwa mfanyakazi wa serikali au kuajiria kusiwe kigezo cha mtu kuchindwa kujitafutia maendeleo yake nakubaliana nawe kabisa sio kila mtu kwa sababu yuko serikalini basi umjudge kutokana na kipato chake wapo waliopata pesa au kufanya biashara kabla ya kupata kazi na walipo pata kazi hawakuacha kufanya biashara tusikimbilie kumtupia mtu lawama ati jambazi or kala rushwa hii sio sawa