MCHUNGAJI Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapile Babu Ambi (pichani), anaendelea kusakamwa na wagonjwa wanaodai hawakuponyeshwa na dawa yake, wapo walioweka nia ya kumburuza mahakamani lakini mpya ni pendekezo la kumfilisi.
Madai hayo yanakuja wakati ambao Babu Ambi ameukata, ameshakamilisha ujenzi wa nyumba yake ya kisasa kijijini Samunge, pia anamiliki magari mawili ya bei mbaya, Toyota Land Cruiser (pick-up) na Isuzu (pick-up).
Babu Ambi, ameshahama nyumba chakavu aliyokuwa anaishi zamani na sasa anaendesha maisha yake kwenye mpya ya kisasa ambayo kwa Samunge, inaonekana ni kama Ikulu kwa jinsi inavyomeremeta.
Wakati Babu alizoea kukanyaga vumbi kwenye nyumba yake ya awali ya udongo, yenye chumba kimoja cha kulala, hivi sasa anatembea juu ya sakafu iliyotandikwa vigae (tiles) kila eneo.
Nyumba ya Babu, pia ina kila kitu ambacho hustahili kuwemo kwenye nyumba ya kisasa yenye hadhi ya mtu mwenye fedha, vile vile ina umeme wa mionzi ya jua na maji ya uhakika.
Wanamwonea wivu babu wa watu bure, kama mumeshindwa kuwaburuza mahakamani na kuwafilisi mafisadi waliokula mabilioni ya wapiga kura kwanini mmufilisi babu ambaye yeye kachukuwa 500/= tu?
Hata na mimi nashindwa kujua madai yako ya msingi ni nini? lakini pia ni hospitali ngapi walishakwenda wakatibiowa bila kupona na je walienda kuwadai madaktari gharama za matibabau?
Amewadanganya wabunge na mawaziri huyu babu inaonyesha ni mjasiriamali mzuri hakuchukua kitu kitu kikubwa ili wasishituke.