Utafiti: Waislam walisusia sensa kwa asilimia 60%

Mimi ningaliiona sensa ya maana kama serikali inatumia raslimali zake kuinua uchumi na hali duni ya watanzania. Unaspend hela nyingi kuhesabu watu wakati shule hazina hata madawati? Unamhesabu mtu leo kesho anakufa kwa kukosa dawa ya kutuliza maumivu? Wamama wanaenda kujifungua wanalundikana kama ng'ombe kwenye chumba kimoja bila vitanda wala huduma muhimu? Kama huwezi kumhudumia hata mjamzito unamhesabu nani?
Kwenda kuwahesabu watanzania ni usanii mtupu. Kwanza serikali ishughulikie mahitaji muhimu kama elimu, mahospitali, barabara hadi vijijini then ituhesabu. Watanzania tumekata tamaa kwani viongozi wanajilundikia mali huku sisi tukifa duni. Unamhesabuje mwananchi ambae hutibiwi hospitali moja nae? Ni kwa nini wasiwahesabu wale wanaopokea matibabu India tukajua ni kiasi gani cha kodi kinahitajika kwa mwaka ili tujikunje kufanikisha matibabu hayo?
Sensa ya kitanzania ni kama mtu anasesabu tu mbuzi. Haina manufaa yeyote kwa raia wake. Kama mtu anagoma kuhesabiwa ni sawa kabisa na ni haki yake. Tuache unafiki na tuambiane ukweli. Wanaonufaika na uchumi wa Tanzania sii watanzania hata kidogo.
Kama serikali inafanya kazi ya serikali basi ikiita watu kuhesabiwa wataenda tena bila ubishi wowote, ila kama ni huu usanii na unafiki wa kujinufaisha binafsi na familia zenu wengi watawagomea. Tunahitaji serikali itakayoweka system in order ili mtoto akizaliwa ajulikane amezaliwa. Mtu akifa ajulikane amekufa na sii ujinga wa kusukumana na watu eti unawahesabu huku huwahudumii hata katika mahitaji ya msingi.
Jengeni shule bora, hospitali za maana na njia bora za usafiri kwanza. Wapeni wanetu elimu bora. Jengeni vyuo bora na sii kuwakimbiza watoto wenu kusoma nje kwa garama ya mashule yetu. Rudisheni kwanza usafiri wa reli ili wananchi wasafirishe mazao na bidhaa zao bila usumbufu wa kulipia malori ya ridhimoja na vituo vyake vya mafuta.
Acheni unafiki. Hii serikali haina lolote la maana hata kama tungalihesabiwa wote kabisa. Sensa itajikamilisha yenyewe kama serikali inaihudumia jamii iliyoiweka madarakani. Bila hivyo hata tungalijipanga wote kwenye mstari na kuhesabiwa kwaq pamoja ni bure.

ndio maana tunasema mliotishia kugomea sensa hamjielewi mnagomea kwa sababu gani haswa!!
 
Inafahamika kuwa zaidi ya 90% ya wakazi wa Zanzibar ni waislamu na kwamba sensa ni kwa manufaa yao, sasa nini kinapelekea wao kugomea sensa:
  1. Ni kuonyesha mshikamano na wenzao wa Bara?
  2. Ni kukosa kujitambua?
  3. Ni kuonyesha upinzani wao kwa serikali ya Rais Shein?
  4. Ni kwa viongozi wao kujitafutia umaarufu na kutaka kutambuliwa? au
  5. Ni kutojua umuhimu wa sensa?
Maoni yangu: Nadhani hapa kuna ajenda ya siri ambayo intelijensia ya serikali inatakiwa kutafuta majibu.
 
Mkuu hii sensa ni zoezi ambalo limeshindwa sana, maana haikuwa na haja ya kubandika vipeperushi wala kujificha. makarani wa sensa walitoweka wenyewe na kaya nyingi tu hazijaesabiwa hata kama umeacha mlango wa nyumba yako wazi, hakuna atakayekuja kukuhesabu. lakini tutaambiwa zoezi limekamilika kwa kishindo cha 99.99%
 
Uchunguzi wakawaida utagundua idadi kubwa ya waliokosoa serekali kutaka kipengele cha dini ktk sensa ni wasomi wa kiislam waliopitia vyuo vikuu vya taifa ambao wanaujua mfumo mzima wa serekali unavyoendeshwa na athari yake kwa taifa.
ndio wasomi walioibua athari ya MOU kwa taifa.
. Lkn pia inaonyesha idadi kubwa ya jamii ya kiislam wamesusia sensa ingawa liziutumika nguvu na wengine kuhesabiwa kwa mtutu wa bunduki wakiwa wameelekezewa.
kipindi kirefu nilipokuwa nasikiliza redio za kiislam hakuna hata redio moja iliowahi kuhamasisha sensa tofaut na redio za Umma kama TBC, redio Uhuru, redio one , Redio Free Africa na Clouds fm, times na nyengine.
lkn hata redio za waumini wa kikiristo kama redio Tumaini na Wapo redio zilikuwa zinatoa matangazo ya sensa kila wakati.
chakushangaza hata redio Qurani inayomilikiwa na BAKWATA nayo haikuwahi kutoa tangazo lolote la sensa huku redio Kheir, redio imaan wao wakiwaweka masheikh wanaopinga SENSA, Redio Nuur,redio Adhana nazo Zikipiga qasida wala hujui kama kuna sensa
.
hata hao masheikh na watu wa Takwimu ambao wakihamasisha sensa wakitumia TBC au redio one na sio kwenye vyombo vya habari vya madhehebu ya kiislam ambapo jamii kubwa ya kiislam ndio inasikiliza.
huu ni ushahidi kwamba waislam walilazimishwa tu, na wengi wanapendekeza uchaguzi 2015 serekali itumie nguvu kwa wale wote wanaokataa kumchagua Mbunge au rais wa nchi kwa manufaa ya taifa kama ilivyosensa

Kwa maana hiyo idadi itakayopatikana ni ya wakristo na wapagani? Mtaumia myoyo sana, wakristo hawana haja ya kujua idadi yao maana wanachokifikiria na mipango yao ni zaidi ya sensa kwa asilimia 10000%. Nakushauri kwa siri uingie kwenye makanisa usikilize agenda zao. Ni nadra sana kuzungumzia ishu za watu wengine au dini za watu, zaidi ya kuwafundisha waumini kumjua Mungu na kubuni miradi na huduma mbalimbali za kimwili na za kiroho. Kujua idadi sio jambo la maana kwao japo zikiwepo zitawasaidia kujenga mashule yenye tija, vyuo vikukuu, vituo vya watoto n.k na vyote hivyo havina ubaguzi wa nani apewe huduma au asipewe maana kwao wameshavuka ishu kama hizo
 
Kulikuwa na Umuhimu kwa vyombo vya Dini kuitangaza sensa,.Kwani hata kwenye maandiko,.[ BIBLE] inashuhudia kuwapo kwa sensa na YESU pia alisafiri na wazazi wake lengo ikiwa ni kwenda kuhesabiwa. [http://wiki.answers.com/Q/Why_did_Mary_and_Joseph_travel_to_Bethlehem].
katika UISLAMU pia inafahamika kwamba uhesabiwa [ census] na analysis za Kidemographic ni SUNNAH [Qastalani, Irshad al-Sari]
. vile vile katika Hadith inasomeka, The taking of a census itself does not lift blessings, because it is for a religiously-sanctioned communal benefit. [al-Asqalani, Fath al Bari Sharh Sahih al-Bukhari] .
Yapo mapokeo ya Hadith yanayopatikana kutoka kwa Bukhari na Muslim yakiwa na maneno tofauti, ambapo Hudhayfa (Allah be pleased with him) alisema:Tulikuwa na MTUME wa MWENYEZI MUNGU (peace and blessings of Allah be upon him) ambaye alituambia , nihesabieni ni watu wangapi wana imani ya Kiislamu.' [http://seekersguidance.org/ans-blog/2011/08/25/why-was-the-census-ordered-in-the-time-of-the-prophet-and-the-companions/]
Sasa Kama vitabu vya Dini vimezungumzia UMUHIMU WA SENSA kiasi hicho HIVI hawa waliOkataa kuhesabiwa ni WAISLAMU KWELI???ama kweli sio kila ALIYESOMA AMEELIMIKA nashangaa.,..Poleni Sana kwa kujua kitu ambacho hamkijui
 
TUANZISHE TENA KIJIJI CHA NGENGEMKENI MITO MINGI
Kwa kuwa umenihakikishia kuwa waliogomea sensa ni wasomi, nachelea kusema kwamba tuanzishe tena kijiji cha Ngengemkeni Mitomingi. Wale wasomi waliosoma kitabu cha penzi kitovu cha uzembe, wanajua maudhui ya kitabu hicho, moja ya maudhui ni ya wananch wa kijiji hicho kugomea sensa wakidai kuwa anayehesabu watu anataka kuwaroga. Nachelea tena kusema kwamba, hata waislam waliogomea sensa sababu yao ni ile ile, kwamba wakihesabiwa bila kuwepo na kipengere cha dini basi wanarogwa kimaendeleo.
Binafsi, sikuona haja ya vyombo vya habari vya kidini kulazimika kuitangaza sensa, kwani sensa ni zoezi la Kitaifa, si la kidini, ila kama chombo cha dini kitatangaza, sawa tu, kisipotangaza, sawa pia.
Binafsi, hainishtui eti wasomo nao wamegomea sensa, wala isikupe moyo na kuona kuwa kuna usahihi,"kusoma si kuelimika" na ktk karne hii, Tanzania kuna wasomi wengi wenye ugonjwa ktk kupambanua masuala yahusuyo dini na mustakabali wa Taifa.Nachelea tena kusema wasomi wa namna hiyo wana ugonjwa mbaya sanausio na tiba rahisi, na mara nyingi ukiwapima wana uwezo mdogo hata ktk Taaluma walizozisomea, bila kujali kiwango cha Taaluma walizonazo. Natambua kwamba wapo wenye kiwango cha juu cha Taaluma zao, na hao ukiwasikia wanashindwa kupambanua masuala hayo, wanafanya maksudi kwa maslahi ya kisiasa.
MWISHO. Serikali ilitakiwa kuwakusanya wote waliogomea sensa na kuwalundika ktk kijiji maalum kitakachopewa jina la Ngengemkeni Mito Mingi, kwa makumbusho ya kihistoria.

du kumbe hata madaktari na walimu waliogoma hawajaelimika? Mh basi tanzania hakuna msomi.
 
Mimi niligoma kuhesabiwa (japokuwa sikutanganza) lakini si kwa sababu ya kipengee cha dini (mimi si muumini wa Kiislamau wala wa Kikristu, ninajiweka katika kundi la Wajadi) bali ni kwa sababu naiona sensa ya Bongo kama usanii tu nami sitaki kuwa sehemu ya usanii huo. Ninaomba unipe sababu mbili kuu kwa nini nisigome kuhesabiwa!
Mwaka 2002 nilihesabiwa mimi na familia yangu lakini nikipita mitaani ninakuta watoto wa shule za msingi wamekalia mawe darasani kama si kukaa sakafuni huku wakiwa wamerundikana katika chumba kimoja cha darasa kama maguni ya maharakwe kwenye Fuso! Nikipita vijijini akina mama na wasichana wadogo bado wanatembea maili zaidi ya sita kutafuta maji ya kunywa na kupikia! Leo hii watawala wetu wanatuhamasisha kuhesabaiwa kwa madai kuwa sensa inawasaidia kupanga maendeleo!! Mimi ninafikiri hata Masheikh waliogomea sensa kwa msingi wa dini wamedhihirisha welewa wa hali ya juu wa uchambuzi wa masuala ya kidunia zaidi ya nyie mnaotaka kuhesabiwa tu bila kujua kwa nini mnahesabiwa alimradi amesema Rais kama kama sio Rahisi.

Mwaka 2002 kulikuwa na barabara zenye lami ngapi?
mwaka 2002 kulikuwa na vituo vya afya vingapi?
Mwaka 2002 kulikuwa na vyuo vikuu vingapi?
Sitaki kuamini kuwa hali tuliyokuwa nayo toka TANU ndiyo hii na kuwa sehemu tuliyokuwepo mwaka 2000 ndiyo tulipo leo. Nchi hii imejaa watu walalamishi wasio na shukrani wasiojua kuwa hii ni nchi ambayo bado inaendelea na inachangamoto nyingi. Nawapa pole viongozi wa Afrika maana kuongoza watu katika nchi hizi ni presha.
 
na uchaguzi mkuu wasusie kwa 80%.

sasa hapo ndio umetuthibitishia kuwa waislamu wamegoma kwa asilimia 60??? Mbona ni porojo tupu? Grea thinker wa siku hizi noma!!!

acha porojo na majungu ,kama mmefanya utafiti na kugundua mpo asilimia sitini mliogomea sensa mbona miaka yote mmeshidwa kujijua mko wangapi.

ushahidi wa mazingira unaonyesha, sio asilimia 60% bali waislamu wamegomea sensa kwa 100%. Wengi hawakuandikishwa, na wachahche walio andikishwa, wameandikishwa baada ya vitisho vya raisi wao, jeshi lapolisi lilivyo tumika na waandishi wa habari walivyo jidharau baada ya tukio hili.
 
Back
Top Bottom