Elections 2010 Utafiti wa TCIB: Dk. Slaa aongoza

AK-47

JF-Expert Member
Nov 12, 2009
1,373
199
Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Tanzania Citizen's Information Bureau (TCIB) na kutolewa leo umeonyesha Dk Slaa anaongoza kwa asilimia 45, JK asilimia 41,Prof. Lipumba asilimia 10, Hashim Rungwe 2, Peter Mziray 1 na Mutamwega 1.


Utafiti huu umefanyika kwenye mikoa 15 iliyochaguliwa kwa njia ya kinasibu (random sampling ) na kwenye jimbo moja katika kila mkoa wananchi kati ya 60 na 100 walihojiwa. Utafiti umefanywa ndani ya mwezi huu na kutolewa leo Jijini Dar es Salaam.

 
Last edited by a moderator:
Nina hard copy tu nimeipata kwa mtu sina soft copy
 
akija mwingine kufanya utafiti atasema dr.slaa 65% kikwete 20%.........nk........iko wazi na kila mtz hamtaki kikwete isipokuwa mafisadi,na familia yake kwani hata marafiki zake wamemtosa sasa.......DR.SLAA 4CHANGE!
 

clip_image002.jpg
Kutoka kushoto ni Mhadhini kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Uchumi Dr.Vicent Leyaro akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Courtyard juu ya utafiti wa (TCIB) akiwa na mwakilishi wa Mkurugenzi wa (TCIB) Bw. Steven Msechu.

Na.Mwandishi wetu.

Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kutoa utafiti wa taarifa mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha wananchi maamuzi kwa uelewa la Tanzania Citizens Information Bureau (TCIB) limetoa taarifa ya matokeo ya utafiti wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais 2010.

Akizungumza na waadishi wa habari Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es salaam idara ya Uchumi Dr. Vicent Leyaro amesma malengo ya TCIB ni kutoa msukumo kwa wananchi kushiriki katika harakati za kulinda na kendeleza misingi ya Demokrasia, Kutoa fursa kwa wananchi katika kutoa maoni yao juu ya mambo mbalimbali katika maisha na kujenga uwezo wa wananchi kwa njia ya tafiti na elimu katika nyanja za serikali, siasa, Mambo ya Kimataifa, ulinzi, elimu na maadili.

Aidha Dr. Vicent Leyaro amesema washiriki katika kura hii ya maoni ni 3047 wenye wasifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto chini ya darasa la saba, elimu ya sekondari na elimu iliyo juu ya sekondari ambapo katika utafiti huo silimia kubwa ya vijana wamonekana kuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Wllbrod Slaa na asilimia kubwa ya wazee wameonyesha kumuunga mkono mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Amesema Dr. Willbod Slaa ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa ya Kilimanjaro 71%, Arusha 60.4%, Manyara79.8%, Iringa58.2% na Dar es salaam 42% ambapo Jakaya Kikwete ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa Dodoma 59.3%, Morogoro 56%, Mbeya50%, Rukwa54.3% na Ruvuma 55%.

Akihitimisha wakati akijibu maswali kwaa waandishi wa habari Dr. Vicent Reyaro amesema utafiti haukuangalia wala kupendelea sehemu ambazo mtu anapendwa sana kuliko sehemu nyingine na uchambuzi wa matokea kimkoa yanaonyesha kuwa wagombea wawili Jakaya Kikwete na Dr. Willbrod Slaa wanachuana vikali baadhi ya mikoa na mikoa mingine kufanya vibaya.

Hata hivyo utafiti huu wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais hauukufanyika kwa upande wa Zanzibar japokuwa wananchi wa Zanzibar wanashiriki katika kupiga kura ya kuchagua rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 
MO-BLOG.jpg


Kutoka kushoto ni Mhadhini kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Uchumi Dr.Vicent Leyaro akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Courtyard juu ya utafiti wa (TCIB) akiwa na mwakilishi wa Mkurugenzi wa (TCIB) Bw. Steven Msechu.


Na Mwandishi wetu

Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kutoa utafiti wa taarifa mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha wananchi maamuzi kwa uelewa la Tanzania Citizens Information Bureau (TCIB) limetoa taarifa ya matokeo ya utafiti wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais 2010.

Akizungumza na waadishi wa habari Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es salaam idara ya Uchumi Dr. Vicent Leyaro amesma malengo ya TCIB ni kutoa msukumo kwa wananchi kushiriki katika harakati za kulinda na kendeleza misingi ya Demokrasia, Kutoa fursa kwa wananchi katika kutoa maoni yao juu ya mambo mbalimbali katika maisha na kujenga uwezo wa wananchi kwa njia ya tafiti na elimu katika nyanja za serikali, siasa, Mambo ya Kimataifa, ulinzi, elimu na maadili.

Aidha Dr. Vicent Leyaro amesema washiriki katika kura hii ya maoni ni 3047 wenye wasifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto chini ya darasa la saba, elimu ya sekondari na elimu iliyo juu ya sekondari ambapo katika utafiti huo silimia kubwa ya vijana wamonekana kuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Wllbrod Slaa na asilimia kubwa ya wazee wameonyesha kumuunga mkono mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Amesema Dr. Willbod Slaa ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa ya Kilimanjaro 71%, Arusha 60.4%, Manyara79.8%, Iringa58.2% na Dar es salaam 42% ambapo Jakaya Kikwete ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa Dodoma 59.3%, Morogoro 56%, Mbeya50%, Rukwa 54.3% na Ruvuma 55%.

Akihitimisha wakati akijibu maswali kwaa waandishi wa habari Dr. Vicent Reyaro amesema utafiti haukuangalia wala kupendelea sehemu ambazo mtu anapendwa sana kuliko sehemu nyingine na uchambuzi wa matokea kimkoa yanaonyesha kuwa wagombea wawili Jakaya Kikwete na Dr. Willbrod Slaa wanachuana vikali baadhi ya mikoa na mikoa mingine kufanya vibaya.

Hata hivyo utafiti huu wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais hauukufanyika kwa upande wa Zanzibar japokuwa wananchi wa Zanzibar wanashiriki katika kupiga kura ya kuchagua rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Chanzo:
Changamoto
 
wangetoa matokeo ya jumla nchi nzima au walau kwa mikoa waliofanyia utafiti ili kutoa taswira kama walivyofanya wenzao wa:

  • redet
  • synovate
  • mwanahalisi
  • jamiiforums
  • dailynews
 
Huu utafiti nao ni dhaifu sawa tu na ule wa Benson Bana. Watoto chini ya darasa la saba wanapiga kura? Na bado hajatuambia hao wa shule ya msingi ni wangapi, tusishangae kusikia ni 50% of the sample! Kumbe Benson Bana hayuko peke yake!
 
Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Tanzania Citizen's Information Bureau (TCIB) na kutolewa leo umeonyesha Dk Slaa anaongoza kwa asilimia 45, JK asilimia 41,Prof. Lipumba asilimia 10, Hashim Rungwe 2, Peter Mziray 1 na Mutamwega 1.


Utafiti huu umefanyika kwenye mikoa 15 iliyochaguliwa kwa njia ya kinasibu (random sampling ) na kwenye jimbo moja katika kila mkoa wananchi kati ya 60 na 100 walihojiwa. Utafiti umefanywa ndani ya mwezi huu na kutolewa leo Jijini Dar es Salaam.
Thanks
 
Nadhani taasisi hii utafiti wake unaweza ku-reflect kaukweli fulani kuliko wale Sinto-vote na Redirty ambao inaonyesha kabisa kuwa kuna biaseness na kuingiliwa kiana fulani na Serikali. Hata tofauti baina ya wagombea watatu Dk Slaa, Kikwete, na Prof Lipumba si mkubwa sana na hiyo ni hali halisi hata katika mahudhurio ya watu kwenye kampeni za Dk Slaa na Kikwete.

Utafiti huu nauamini zaidi. Viva TICB!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom