UTAFITI: 'Message' ni adui wa Elimu pia...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Ni utafiti wangu binafsi.Hapa ni sehemu ya kwanza kuuwakilisha.Ni hivi:ujumbe mfupi wa maneno wa simu za viganjani almaarufu kama 'sms' kwa kiasi kikubwa unachangia kudumaza elimu Tanzania. Hii ni kwasababu,wanafunzi wa Shule na Vyuo ambao hutumia simu za vikanjani kwa kutuma ujumbe,hulemazwa na uandishi wa kifupikifupi katika ujumbe na kujikuta wakiandika kifupi hata kwenye mitihani yao.

Katika utafiti huu,nilifanya mahojiano na maafisa mbalimbali wa Baraza la Taifa la Mitihani,Walimu na Wahadhiri pamoja na Wanafunzi wenyewe. Hoja ya msingi ni juu ya jinsi majibu ya mitihani yanavyoathiriwa na uandishi wa sms. Wengi wa Maafisa,Walimu na Wahadhiri wamekiri kuwepo na kukua kwa tatizo hilo na kudai kuwa majibu ya wanafunzi na wanavyuo hayaeleweki kwa kuwa yanaandikwa 'kihuni'. Wakatoa mfano wa sentensi kama 'Tanzania is a democratic country' ambapo wanafunzi huandika 'Tz z a dmcrtic cntry'.

Wanafunzi nao wamekiri kwa wingi wao kuwa sms hulemaza na kuwaharibia majibu katika mitihani waifanyayo. Wanafunzi hao wakawaasa wenzao na wengine kujenga utaratibu wa kuandika kwa kirefu sms zao ili wasije kulemaa katika uandishi hata wa mambo muhimu ya kimtihani.

Katika utafiti huo,nimewahoji Maafisa 11,Walimu 20,Wahadhiri 20 na Wanafunzi wa Shule na Vyuo 45. Niliuanza 2011 na kuukamilisha 2012. Nitauweka katika mtindo wa ripoti hivi karibuni. Asanteni Wakuu...
 
Hahhaa binafsi huwa naandika kwa urefu

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
hao wanafunzi ndio waleeeeeeeeee...... Walio maliza darasa wakiwa hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu
 
Ni utafiti wangu binafsi.Hapa ni sehemu ya kwanza kuuwakilisha.Ni hivi:ujumbe mfupi wa maneno wa simu za viganjani almaarufu kama 'sms' kwa kiasi kikubwa unachangia kudumaza elimu Tanzania. Hii ni kwasababu,wanafunzi wa Shule na Vyuo ambao hutumia simu za vikanjani kwa kutuma ujumbe,hulemazwa na uandishi wa kifupikifupi katika ujumbe na kujikuta wakiandika kifupi hata kwenye mitihani yao.

Katika utafiti huu,nilifanya mahojiano na maafisa mbalimbali wa Baraza la Taifa la Mitihani,Walimu na Wahadhiri pamoja na Wanafunzi wenyewe. Hoja ya msingi ni juu ya jinsi majibu ya mitihani yanavyoathiriwa na uandishi wa sms. Wengi wa Maafisa,Walimu na Wahadhiri wamekiri kuwepo na kukua kwa tatizo hilo na kudai kuwa majibu ya wanafunzi na wanavyuo hayaeleweki kwa kuwa yanaandikwa 'kihuni'. Wakatoa mfano wa sentensi kama 'Tanzania is a democratic country' ambapo wanafunzi huandika 'Tz z a dmcrtic cntry'.

Wanafunzi nao wamekiri kwa wingi wao kuwa sms hulemaza na kuwaharibia majibu katika mitihani waifanyayo. Wanafunzi hao wakawaasa wenzao na wengine kujenga utaratibu wa kuandika kwa kirefu sms zao ili wasije kulemaa katika uandishi hata wa mambo muhimu ya kimtihani.

Katika utafiti huo,nimewahoji Maafisa 11,Walimu 20,Wahadhiri 20 na Wanafunzi wa Shule na Vyuo 45. Niliuanza 2011 na kuukamilisha 2012. Nitauweka katika mtindo wa ripoti hivi karibuni. Asanteni Wakuu...

Huyo Mwanafunzi atakayejibu kifupi kwenye mtihani basi atakuwa zumburkuku na anajitakia mwenyewe kufeli
 
Hilo ni tatizo kweli,huwa uandishi wa namna ile unanikera sana
 
Ngoja nisubiri hiyo ripoti yako ya utafiti ndio ntapata pa kuanza kuchangia
 
Huyo Mwanafunzi atakayejibu kifupi kwenye mtihani basi atakuwa zumburkuku na anajitakia mwenyewe kufeli

hlo tatzo la walimu. Kam tulikuwa tunafundishwa usiandke kfup cha katika 'ktk' sembuse madudu ya kujitungia ya is 'z'. Namuunga mkono mdau hapo juu.
 
Ni adui mkubwa sana katika elimu, maana kushindwa mitihani ni sawa na umbali wa nusu nukta
 
...hii yote ilianza na suala zima la kuandika kifupi ili kukwepa "multiple in one" msg maana yakizidi na hela inazidi kukatwa. mpk makampuni ya simu yalipokuja na mapromotion ya extreme sijui cheka na jiachie it was already too late, watu wako addicted na cutting words short. dah safari ya elimu bora, tunaenda mbele tunarudi nyuma

on the other hand, mbona hata sisi katika uandishi wetu huwa tunafupisha kama tunaandika kitu casual mfano sms, fb au tunapopost kitu hapa JF, ila tunapokuwa tunaandika vitu formal huku makazini kwetu huwa tunajisahau? I hope no. mara nyingine ni hawa vijana kujiendekeza tu!
 
Hata mimi naamini kabisa! Hata huku JF kuna wanafunzi na wahitimu wa Vyuo Vikuu wengi wanaandika kihuni kabisa. Wakikumbushwa kurekebisha lugha wanakuwa wakali ile mbaya.
 
Back
Top Bottom