Tufanye mathalan ulipata nafasi ya kwenda kujiendeleza kimasomo nchi za magharibi katika kutafuta shahada ya uzamivu, muda wa shahada ni miaka 4... shule yako hiyo haikuruhusu kurudi nyumbani bongo mara kwa mara kutokana na kukaba na pia gharama kali ya usafiri wa anga , mdogo wako wa kiume anayekufata anaishi mji mmoja na unaoishi wewe na mkeo, unapoondoka unamsisitiza asiache kuitembelea familia yako na kuijulia hali, wewe umeoa na una watoto watatu na mkeo wakati unaondoka, na mdogo wako nae ana mke na watoto....
Baada ya miaka 2 unabahatika kurudi likizo nyumbani na kukuta mkeo ni mja mzito wa miezi 7 au 8, unambana hasa akueleze ni mimba ya nani, mwishoni anakuambia ni ya mdogo wako na anaomba msamaha kwa kuwa alipitiwa na shetani, na umbali ulichangia kumtia majaribuni.....
katika hali hiyo, Ingelikuwa ni wewe ungechukua uamuzi gani?
Baada ya miaka 2 unabahatika kurudi likizo nyumbani na kukuta mkeo ni mja mzito wa miezi 7 au 8, unambana hasa akueleze ni mimba ya nani, mwishoni anakuambia ni ya mdogo wako na anaomba msamaha kwa kuwa alipitiwa na shetani, na umbali ulichangia kumtia majaribuni.....
katika hali hiyo, Ingelikuwa ni wewe ungechukua uamuzi gani?