Utafanyaje?

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,025
Wewe ndo msanii,uko busy stage una perform,unaimba kwa hisia mpaka unafumba macho,lakini baadaye unagundua kuwa mashabiki wako busy na mambo yao tofauti na wengine wanachapa usingizi.Yes,watu wametoa viingilio vyao na ndo hao wamelala wakati we unajitahidi kuwaburudisha,utachukua uamuzi gani?
 
Ni kuendelea kuwaburudisha tu, hata kama wanaendelea na mambo yao!
 
Kazi waliyokupa fanya mpaka iishe kwa sababu viingilio vyao ni gharama ya kukuweka wewe pale uwaburudishe.Waliolala wamekolea na burudani.Wenye mambo mengine inawezekana umewakuna sana wanasemezana wenyewe.Wewe chapa kazi mwanangu kwa kupata bahati ya hiyo ajira.Usichezee ajira chezea pesa baada ya kazi.Heshimu wateja kwani wao ndio mfalme wewe mtendaji.
 
Take it as a challenge

Kajifunze how to control the crowd like Busta Ryhmes.
 
Unajua hata home team inakuwa tipped ku perform fresh kwa sababu ya cheerings from the home fans,hawa mashabiki wanaboa bwana.
 
kwa sababu wameshalipa kiingilio, na uhakika wa kulipwa upo.......!
waaache walale mpaka wakorome na kuota. Coz cdhan kama waweza wacheer pipo like hao.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom