(UTAFANYAJE?) Ukigundua mwenza wako ni mshirikina

Kama ninao uthibitisho ya kuwa ni mchawi na yeye mwenyewe kakiri, hapa hakuna kupenda tena namtema na akinitishia namfungulia kesi

The WitchCraft Act Chapter 18 ya mwaka 2002 Ibara ya 5(1) na 5(2) inataja adhabu zao vizuri kabisa


nilikuwa sijui kama hiyo sheria ipo na ukimfungulia mashitaka inabidi uhakikishe afungwa milele lah sivyo akitoka ama zako ama zake

 
ndoa ya kikristo, ndoa ya kikristo. Toa maandiko yanayofanya ndoa ya kikristo isivunjike. Huwezi ukageuza dunia kuwa jehanamu ya mateso kwa mwenzio kwa sababu tu eti umefunga ndoa ya kikristo, Yesu mwenyewe aliyafukuza na kuyakemea mapepo, sasa wewe unashauri mtu aendelee kuyakumbatia na kumlisha mchawi simply because ni ndoa ya kikristo? Ni Kristo gani huyo unayemzungumzia hapa?

ALincon kaenda mitini
 
ndoa ya kikristo, ndoa ya kikristo. Toa maandiko yanayofanya ndoa ya kikristo isivunjike. Huwezi ukageuza dunia kuwa jehanamu ya mateso kwa mwenzio kwa sababu tu eti umefunga ndoa ya kikristo, Yesu mwenyewe aliyafukuza na kuyakemea mapepo, sasa wewe unashauri mtu aendelee kuyakumbatia na kumlisha mchawi simply because ni ndoa ya kikristo? Ni Kristo gani huyo unayemzungumzia hapa?

Soma Mathayo 19:3-12. Hayo ni moja ya majaribu wala hapaswi kuyakimbia. Hivyo ni vita vya kiroho havipiganwi kwa mwili. Wewe u'mtakatifu' kiasi gani hata ujitenge na mchawi iwapo Yesu mwenyewe alikaa na wachafu zaidi ya huyo? Msaidie ili naye amjue Yesu kama wewe ni mkristo!
 
Wapo wanaume wachawi pia,nakushauri zungumza nae,mshauri aachane na huo uchawi then nenda nae kwa Gwajima au Kakobe,wanajua namna ya kushughulikia haya masuala......Huo ni utumwa mkubwa sana na pengine hata wewe unakugharimu au utakugharimu wewe na watoto.
Act quickly,akikataa,though ni ngumu but sikushauri uendelee nae,na wala usiwaweke wanao karibu yake,hakuna nguvu zaidi ya ile ya Mungu,usiogope,jipe moyo mkuu utayashinda!kila la kheri!
 
Soma Mathayo 19:3-12. Hayo ni moja ya majaribu wala hapaswi kuyakimbia. Hivyo ni vita vya kiroho havipiganwi kwa mwili. Wewe u'mtakatifu' kiasi gani hata ujitenge na mchawi iwapo Yesu mwenyewe alikaa na wachafu zaidi ya huyo? Msaidie ili naye amjue Yesu kama wewe ni mkristo!

Hebu mwambie huyu jamaa naona kama sio vile nae walewale
 
Kama ndoa ilifungwa kwa misingi ya dini ya kikristo huwezi kumuacha, huo mzigo ni wako na kwa ushauri tu unapaswa umuombee Mungu ampe macho ya rohoni ili aweze kujionea uchafu wake. Bila shaka ataumia akigundua kuwa uchawi hauna thamani aliyoina na hivyo ataacha. Huna haja ya kumpiga, kumuacha wala kumburuza kwenda kokote! Maombi yatafanya kazi popote atakapokuwa.

Haleluya, ubarikiwe!
 
Kama ndoa ilifungwa kwa misingi ya dini ya kikristo huwezi kumuacha, huo mzigo ni wako na kwa ushauri tu unapaswa umuombee Mungu ampe macho ya rohoni ili aweze kujionea uchafu wake. Bila shaka ataumia akigundua kuwa uchawi hauna thamani aliyoina na hivyo ataacha. Huna haja ya kumpiga, kumuacha wala kumburuza kwenda kokote! Maombi yatafanya kazi popote atakapokuwa.

Haleluya, ubarikiwe!
 
wanajf ikitokea mmeoana then ukagundua mwenzio ni mshirikina/mchawi utafanyaje? na anao siku nyingi ila hukujua baada ya kupata habari ukamuuliza akakuambia ni kweli yeye ni mchawi na hawezi kuacha na wewe unampenda ila hupendi uchawi!
na kama anajikinga je... asidhuriwe na wabaya ake?
 
Kama ninao uthibitisho ya kuwa ni mchawi na yeye mwenyewe kakiri, hapa hakuna kupenda tena namtema na akinitishia namfungulia kesi

The WitchCraft Act Chapter 18 ya mwaka 2002 Ibara ya 5(1) na 5(2) inataja adhabu zao vizuri kabisa

heee! Serikali si haiamini uchawi sasa imekuwaje tena kuna hiyo act!
 
Itakubidi tu uombe mungu, hasi na hasi havivutani. Ukiona mwenzio ni wa shetani we nenda kwa mungu tu, ndo utapata msaada.
 
Piga chini maana kama alishakula nyama za wenzake na yake italiwa, sasa unaweza ukapoteza watoto kwa upuuzi wake.
 
Back
Top Bottom