Utabiri wa REDET na Uchaguzi Tanzania...

Mkuu wangu hakuna ugumu kabisa ktk kuunganisha Chadema na CUF isipokuwa wote wameingizwa mjini na UDINI.

Hii sio kweli. Nimeshakaa mara kadhaa na viongozi wa vyama vya upinzani tukijaribu kuunganisha nguvu wakati wa uchaguzi ili tuwe na mgombea mmoja wa upinzani. Nina diriki kusema ukindoa CUF vyama vingine vyote vya upinzani ni mapandikizi au viongozi wao wa juu ni vibaraka vya CCM. Kwa namna moja au ingine huwa wanafadhiliwa au wanawezeshwa na CCM kwa vile wanatumia hivi vyama kama miradi ya kutafutia pesa. Tatizo la CUF ni kwamba uongozi wao wa juu una concentrate kwenye siasa za zanzibar tu. Hawako tayari ku compromise chochote when it comes to mainland politics. Na hii ndio sababu waliamua kumweka Lwakatare pembeni ambaye alikuwa anawasumbua na kelele zake za Ubara. Naomba ujiulize ni kwanini wabunge wa CUF na CHADEMA wanashirikiana vizuri sana bungeni ilhali viongozi wa CUF kila siku wako kwenye majukwaa wakiiponda CHADEMA? Wabunge wa CUF macho yao yako Dodoma, viongozi wa CUF macho yao yako Pemba na Unguja.

.
 
Hii sio kweli. Nimeshakaa mara kadhaa na viongozi wa vyama vya upinzani tukijaribu kuunganisha nguvu wakati wa uchaguzi ili tuwe na mgombea mmoja wa upinzani. Nina diriki kusema ukindoa CUF vyama vingine vyote vya upinzani ni mapandikizi au viongozi wao wa juu ni vibaraka vya CCM. Kwa namna moja au ingine huwa wanafadhiliwa au wanawezeshwa na CCM kwa vile wanatumia hivi vyama kama miradi ya kutafutia pesa. Tatizo la CUF ni kwamba uongozi wao wa juu una concentrate kwenye siasa za zanzibar tu. Hawako tayari ku compromise chochote when it comes to mainland politics. Na hii ndio sababu waliamua kumweka Lwakatare pembeni ambaye alikuwa anawasumbua na kelele zake za Ubara. Naomba ujiulize ni kwanini wabunge wa CUF na CHADEMA wanashirikiana vizuri sana bungeni ilhali viongozi wa CUF kila siku wako kwenye majukwaa wakiiponda CHADEMA? Wabunge wa CUF macho yao yako Dodoma, viongozi wa CUF macho yao yako Pemba na Unguja.

.

...ni dhahiri haya yanaonyesha udhaifu wa Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa chama hicho ambao pia ni wagombea wa viti vya urais kupitia chama hicho...

Bila muungano wa CHADEMA na CUF upinzani hauna nguvu isipokuwa kwa wabunge mmoja mmoja,...

Haya, tunaotaka maendeleo ya kweli tutaendelea kuwasubiri wenye nia ya kweli!...

...CCM nako vipi, hakuna tena wale kina G-55, CCM 'asilia', nk ambao wanaweza kuwachallenge hawa CCM 'Mtandao?'
 
Tatizo kubwa TANZANIA ni tume huru na vyombo vya dola, unajua vijana wengi waliopo jeshini bado hawajajua kuwa wapo pale kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania na sio CCM na makada wao. Wao wanajua pale wapo kwa sababu ya CCM, they are indefinitely wrong, mimi nafikiri watu tunapokuwa watumishi wa Umma tujaribu kutune mindsets zetu upya.Tupo kwenye utumishi kwa ajili ya Watanzania na sio CCM, watu waelewe kuwa CCM imepewa tu dhamana ya kuongoza na wao muda wao ukiisha chama kingine kitachukua hatamu. Sasa hapa huwa najiuliza hivi chama kingine kikachukua hatamu hao wanajeshi watakubali kweli kukitumikia-----si tutarudi kwenye maisha ya Mugabe na kwenye falsafa ya akili MGANDO.

Halafu vyama vya upinzani vijue kuwa mafanikio hayaji tu kwenye silver plates yenyewe, lazima uitafute, so to what i believe they were supposed to put lots of hursals to CCM na serikali yake kwa ajili ya kupata tume huru ya uchaguzi, wasibaki tu kila mara kulalamika kuibiwa kura. lazima vyama vikae na kuplan kuhusu kesho, lakini wao uchaguzi ukiisha na mambo yote yanaisha siku hiyo, hizo ni akili mgando.
 
Mbu,
Jamani hivi mpaka leo hamjabaini ukweli kwamba hii Redet ni chama kingine cha siasa? Shida ni kwamba Redet ni invisible political party ambayo ni arm of sisi m. na inatumika kupiga propaganda kwa mlango wa nyuma.
Mbona sijawahi kusikia wakifanya utafiti wa jinsi sisi m. inavyovuruga uchaguzi? Au mbona hawajawahi kusemea kama uchaguzi una uhalali au la?!

Sikilizeni ukweli ni kwamba si kweli kwamba sisi m inashinda kila mahali. Hapana, maana baada ya uchaguzi huu uliopita ambao mimi nimeuita wa kijinga sana katika thread fulani, nimegundua mengi sana.
Kwanza viongozi wa serikali wanajihusisha kuvuruga uchaguzi na kuhakikisha kwa namna yoyote sisi m. inashinda.

Wakati wa uchaguzi wa mitaa kwa mfano kuna mtaa mmoja ambao baada ya kugundua sisi m wameshindwa walijaribu kuleta sanduku lingine la ziada lililokuwa na kura zilizokwisha kupigwa ili lichanganywe na yale mengine. Kama si juhudi za wananchi kuingilia kati na kulikamata, hadithi ingekuwa nyingine. Lakini maswali yangu ni kwamba je hilo sanduku la ziada lilipatikana vipi? kama si kupatikana kutoka katika uongozi wa halmashauri ya wilaya lilipatikana vipi?

Jambo lingine lililonishangaza ni kwamba pamoja na OCD wa wilaya ile kuitwa baada ya vurugu ya wananchi kutokana na kutaka kuuvuruga kwa makusudi uchaguzi na yeye kugundua kuwa sanduku hilo lilikuwa la forgery na kwamba lisichanganywe na mengine wakati wa kuhesabiwa kura, bado hakuwachukulia hatua wale wote waliohusika. Kwa ajili ya kuwapoza wananchi waliokuwa wamejawa jaziba aliamua liwekwe pembeni na story ikaishia hapo kana kwamba hilo si kosa.

Ilifikia mahali sisi m walikuwa radhi watangaze kuwa mshindi ni sisi m ingawa si kweli wakiamini mambo yatakwenda kwenye rufani itakayochukua muda mrefu na ikiwezekana watamalizana na wahusika mahakamani. Kama si wananchi kuja juu kwa hasira maana walikuwa hawamtaki huyo sisi m na kutishia kuchoma moto jengo na waliomo, hadithi ingekuwa nyingine.
Sasa basi, huo ushindi wanaolilia kila siku kushinda si ndio huu?
si kweli na sintaamini kwamba ni kweli kwamba chaguzi zote sisi m ushinda. La hasha bali zingine nyingi zina hadithi kama hii.

Nilijiuliza swali jingine ambalo lilinishangaza. Kwenye vituo vyote vya kupigia kura katika halmashauri ya wilaya nilikopigia kula walikuwa wamebandika majina ya wagombea ndani ya chumba cha kupigia kura ili mtu binafsi achague kutoka katika majina hayo na kuandika katika karatasi ya kupigia kura mwenyekiti na wajumbe awatakao. Nilitegemea mpangilio wa majina ungekuwa katika alphabetical order. Badala yake majina yalikuwa yameandikwa randomly lakini ya sisi m yakiwa ndio yametangulia juu na ya vyama vingine vya siasa yakiwa chini. Je hii ilifanywa makusudi au bahati mbaya? na mbona ilikuwa ni kwa vituo vyote?

Alafu kwa ujinga kama huu utasikia watu wazima bila hata haya wanatamba kwa ushindi wa kishindo! Ni aibu tupu!

Mwisho wa yote ninaamini kama sisi m wataendelea hivi siku moja si ajabu nchi ikawa kama ilivyokuwa Kenya. Hakuna lisilowezekana.
Na kwa sababu hiyo nabaki nikiamini si kuungana vyama wala nini kitasaidia demokrasia yetu bali siku tukidai tume huru, tena wananchi wakidai na si vyama vikidai, hapo ndipo tutaona mchuano wa kweli. Bila hivyo hadithi itaendelea kuwa hivyo mwaka hadi mwaka na mwisho BALAA LITAZALISHWA.
 
kwani wakiungana ndio watashinda bana!...vyama uchara vitajiondokea taratibu kwenye whole formula..kitu muhimu hapa ni civil education mfano..kudai katiba mpaya, tume huru ya uchaguzi kwa kutumia civil forums kama NGO, CBOna vyama vya upinzani

Siku zote naamini "Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu". Ukifuatilia katika uchaguzi uliopita kama CHADEMA na CUF wangekuwa ni chama kimoja basi idadi yao ya Wabunge ingekuwa kubwa kuliko ilivyo sasa maana kuna majimbi mengi jumla ya kura walizopata ilikuwa ni kubwa ukilinganisha na zile za chama cha mafisadi. Kwa mfano CCM walikuwa na kura 5, CHADEMA 4 na CUF 3 kama ingekuwa ni chama kimoja basi jimbo kama hilo lisingekuwa mikononi mwa CCM.

Pia wapiga kura wako wanapokushauri umuhimu wa kuungana basi ni lazima mfanye hivyo vinginevyo wataona hamjali ushauri wao na hivyo wengi wao kuamua kutopiga kura kwa kuwa wanajua CCM itashinda tena

Mwaka jana Waziri Mkuu wa Kenya Odinga aliwaambia viongozi wa upinzani kama wanataka kuiondoa CCM madarakani ni lazima kuungana vinginevyo itakuwa si rahisi.

Ni aibu kubwa kwa nchi yetu kuendelea kukichagua CCM pamoja na matatizo chungu nzima ndani ya chama hicho na ndani ya Serikali ambayo pia imeindwa na CCM. Nchi nyingine katika hali kama hii CCM ingeshindwa vibaya sana katika uchaguzi ujao lakini kwa Tanzania CCM wataiba kura, watatumia vyombo vya dola kuwatisha na hata kuwapiga viongozi na wanachama vya upinzani. Watatoa hongo ya pesa, fulana, magodoro, chakula n.k. ili kuwaghilibu Watanzania wenye upeo finyu wa kufikiri ili wawapigie tena kura CCM.
 
...Mkubwa,

apart from CHADEMA, CUF na TLP kwa wapinzani sioni chama kingine kinachopiga kelele hadharani kwa sasa kupingana na CCM.

Zitapofikia siku za chaguzi, vyama vyote vilivyolala utaona vinaibuka kama uyoga eti navyo vinakimbilia Ruzuku tayari kwa uchaguzi. Kama sio kuharibiana Kura ni nini?

Kuna mambo mengine wala hayana haja ya kusubiri chaguzi 20 kuyabaini kwamba uchaguzi unahujumiwa kwa makusudi na hivyo vyama pandikizi sababu tu 'penye udhia inapenyezwa rupia!'...

Wakemewe wenye vyama hivyo, na wananchi tujitokeze kuvipinga na kuvikataa hadharani! mfano; (matokeo yao hawa, eti walishindana na CCM kiti cha uraisi!)...


Democratic Party -Kura 31,083
0.27%

PPT Maendeleo -Kura 18,783
0.17%

National League for Democracy -Kura 21,574
0.19%

Demokrasia Makini -Kura 17,070
0.15%

Sauti ya Umma -Kura 16,414
0.14%

Kama hayo yangekuwa matokeo ya darasani si wangekuwa wesharudishwa makwao hao? Wanatuletea utani wakati sisi wananchi tunaendelea kuteseka na matatizo lukuki nchini!

Mkuu nami ninaposema waungane sina maana ya utitiri wa vyama vyote vinavyojiita ni vya siasa bali ni hivyo vitatu labda na NCCR. Kingine kama wanaona mazingira ya uchaguzi kama vile kunyanyaswa na vyombo vya dola, wakuu wa mikoa au hata Wilaya wakapti wa kampeni basi wasusie uchaguzi ili kushinikiza kuwepo na mabadaliko ya kweli ambayo yatavipa nafasi kubwa vyama vya upinzani kupata ushindi kwa maeneo mbali mbali. Hao tume ya uchaguzi wanaona ufujaji mkubwa wa sheria za uchaguzi unaofanywa na CCM lakini hawatii neno bali hufumbia macho uchafu wote huo kutokana na tume hiyo kutokuwa huru.

Umefiak wakati wa kukaa chini na kutafakari, je katika mazingira tuliyonayo kuna haja ya kushiriki katika uchaguzi!? Kwa maoni yangu jibu ni hapana hivyo cha kufanya ni kuishinikiza Serikali kuwepo na mabadiliko ya kweli na tume huru ya uchaguzi ambayo itaweza kukemea chama chochote kile ambacho kitavuruga au kukiuka sheria za uchaguzi. Vinginevyo kushiriki katika chaguzi kila baada ya miaka mitano na baada ya uchaguzi kulalamika malalamiko yale yale kwamba tume ya uchaguzi si huru, vyombo vya dola vilitunyanyasa ni uhayawani.
 
Mbu,
Jamani hivi mpaka leo hamjabaini ukweli kwamba hii Redet ni chama kingine cha siasa? Shida ni kwamba Redet ni invisible political party ambayo ni arm of sisi m. na inatumika kupiga propaganda kwa mlango wa nyuma.

...mnh, Mchukia Fisadi kama REDET ni kweli 2nd arm ya CCM na utabiri wao ulikuwa sahihi miezi miezi mitatu kabla ya uchaguzi ule wa 2005, WANATISHA!

Wao walitabiri mgombea wa CCM kupata kura wastani 75.4%, takwimu sahihi JK alipata kura 80.28%...Ndio kusema uchaguzi haukuwa huru au? Sidhani watanzania 9.m Waliopiga kura, waliyumbishwa na 'propaganda' za REDET.

Kama unakumbuka Blog ya Habari Tanzania nayo ilikuwa na 'kura' zake za maoni... unakumbuka utuletee takwimu zao?
Wakituletea 'tabiri' zao za 2010, nitawatilia shaka na huo mkono wa pili wa CCM , lakini sitokuwa na shaka dira ya wapiga kura!


KURA YA MAONI NAMBA 10:SEPTEMBA 2005
MAONI YA WANANCHI KUHUSU UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 2005
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]CCM [/FONT][/FONT]
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]75.4% [/FONT][/FONT]
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman](979) [/FONT][/FONT]
source; http://www.redet.udsm.ac.tz/documents_storage/2008-3-28-13-23-32_opinion poll sept2005 swahili.pdf

NA MATOKEO KAMILI YA URAISI 2005 YALIKUWA HIVI;

Jakaya Kikwete
Chama Cha Mapinduzi
9,102,951
80.28%
 
ni kweli REDET inaonekana ni progapanda za wana Si Si emu kwa mlango wa nyuma, lakini hii sio issue sana, kwani siasa ni propaganda, akipiga proganda nawe unakuja na propanda kali zaidi ili mwananchi mwenyewe achague, jamani mwenye kumbukumbu sahihi atusaidie- kwa Afrika yote nchi ambazo bado zina chama tawala kama CCM ni ngapi ukitoa Tz na SA?, hii statistics inafaa sana kwa propaganda!
 
Back
Top Bottom