Utabiri wa REDET na Uchaguzi Tanzania...

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,844
...Asilimia 75.4 ya wahojiwa wote walisema wangempigia kura mgombea urais wa CCM ili awe Rais.

...Kuhusu uchaguzi wa wabunge, CCM bado iliongoza kwa wingi wa idadi ya wahojiwa. Asilimia 69.6 ya wahojiwa walisema kwamba wangemchagua mgombea wa CCM ili awe mbunge wa jimbo lao.

...ni muhimu kutambua kwamba maoni ya wananchi kuhusu chaguo lao la vyama na wagombea yanaweza kubadilika kutokana na kampeni za uchaguzi zinazoendelea, pamoja na elimu ya uraia inayotolewa na vyombo mbalimbali. Pia, inategemewa kwamba matokeo haya yatatoa changamoto kwa vyama vya siasa na wagombea kujaribu kuboresha mikakati yao ya kampeni ili kuweza kushinda katika uchaguzi mkuu ujao. -REDET, September, 2005

KURA YA MAONI NAMBA 10:SEPTEMBA 2005
MAONI YA WANANCHI KUHUSU UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 2005
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]CCM [/FONT][/FONT]
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]75.4% [/FONT][/FONT]
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman](979) [/FONT][/FONT]
source; http://www.redet.udsm.ac.tz/documents_storage/2008-3-28-13-23-32_opinion poll sept2005 swahili.pdf

NA MATOKEO KAMILI YA URAISI 2005 YALIKUWA HIVI;

Jakaya Kikwete
Chama Cha Mapinduzi
9,102,951
80.28%

...Swali la kujiuliza ni je? Vyama vya Upinzani vimejiwekea mikakati gani kwa chaguzi za 2010-2015 kama kweli wanataka kuleta mabadiliko ya utawala wa Tanzania kuanzia kwa wabunge na wawakilishi,...maana kwenye uraisi hakuna matumaini kwa sasa!

Ushindi wa asilimia zaidi ya 51 tu ya wabunge wakitoka CCM tayari bunge litakuwa limeelemewa na Chama Tawala...
 
Hilo la CCM kushinda hai hitaji kura za maoni kujua. Tanzania ina chama kimoja ambacho ndicho "hegemony" na vingine vina kua. Mpaka tuta kapo kua na vyama vingine ukiacha CCM vyenye uwezo wa kushinda basi kura za maoni kama hizi ndipo zitakua na maana.
 
Hilo la CCM kushinda hai hitaji kura za maoni kujua. Tanzania ina chama kimoja ambacho ndicho "hegemony" na vingine vina kua. Mpaka tuta kapo kua na vyama vingine ukiacha CCM vyenye uwezo wa kushinda basi kura za maoni kama hizi ndipo zitakua na maana.


Pamoja na utu uzima wa CCM hakika wakiingia ulingoni bila mabavu ya FFU , NEC kuwasaidia na wizi wa kura wanaweza kushangazwa kabisa . Redet wanajua hili miaka hii si ya mwaka 2005. CCM imejionea uchaguzi wa mitaa .Wameshinda sana ila hawawezi kutamba wanajua mbinu zao chafu na zina mwisho .
 
Hilo la CCM kushinda hai hitaji kura za maoni kujua. Tanzania ina chama kimoja ambacho ndicho "hegemony" na vingine vina kua. Mpaka tuta kapo kua na vyama vingine ukiacha CCM vyenye uwezo wa kushinda basi kura za maoni kama hizi ndipo zitakua na maana.

Yaani! nilitaka kuandika maelezo ambayo yanashabihiana sana na yako ;). Wa kulaumiwa katika hali hii pia ni vyama vya upinzani. Pamoja na kupewa mawazo ya bure na Watanzania juu ya umuhimu wa kuungana na kuunda chama kimoja chenye nguvu ili waking'oe chama cha mafisai madarakani bado wameweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa.

Wameshashindwa chaguzi tatu sasa za tangu tuingie katika mfumo wa vyama vingi, pamoja na kuwa kunakuwa na zengwe la wizi wa kura, vitisho na vipigo toka kwa matawi ya CCM aka vyombo vya dola, lakini hawakai chini wakatafakari wafanye nini. Labda baada ya kushindwa katika chaguzi 20 au zaidi za vyama vingi ndiyo wataona umuhimu wa kuyafanyia kazi mapendekezo ya Watanzania kuhusu umuhimu wa kuungana.
 
Yaani! nilitaka kuandika maelezo ambayo yanashabihiana sana na yako ;). Wa kulaumiwa katika hali hii pia ni vyama vya upinzani. Pamoja na kupewa mawazo ya bure na Watanzania juu ya umuhimu wa kuungana na kuunda chama kimoja chenye nguvu ili waking'oe chama cha mafisai madarakani bado wameweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa.

Wameshashindwa chaguzi tatu sasa za tangu tuingie katika mfumo wa vyama vingi, pamoja na kuwa kunakuwa na zengwe la wizi wa kura, vitisho na vipigo toka kwa matawi ya CCM aka vyombo vya dola, lakini hawakai chini wakatafakari wafanye nini. Labda baada ya kushindwa katika chaguzi 20 au zaidi za vyama vingi ndiyo wataona umuhimu wa kuyafanyia kazi mapendekezo ya Watanzania kuhusu umuhimu wa kuungana.
kwani wakiungana ndio watashinda bana!...vyama uchara vitajiondokea taratibu kwenye whole formula..kitu muhimu hapa ni civil education mfano..kudai katiba mpaya, tume huru ya uchaguzi kwa kutumia civil forums kama NGO, CBOna vyama vya upinzani
 
Kuunganba nadhani ni jambo jema ila si suluhisho.Mtaungana lakini watu hawaamini katika Muungano itakuwa ni bure .Elimu ya Uraia kwanza itawale kote na watu waelewe klwamba Upinzani na wapinzani ni Watanzania na si zaidi ya hapo . Hili ndilo muhimu na si kuunganisha vyama .Unawezaje kuwaamini CUF ukawaweka sawa na Chadema ? Jamani kuna ugumu hapo
 
Hilo la CCM kushinda hai hitaji kura za maoni kujua. Tanzania ina chama kimoja ambacho ndicho "hegemony" na vingine vina kua. Mpaka tuta kapo kua na vyama vingine ukiacha CCM vyenye uwezo wa kushinda basi kura za maoni kama hizi ndipo zitakua na maana.

...mkuu, mwenzako sina mashaka na ushindi wa CUF Zanzibar.

Anyway,...ina maana wananchi hawana imani na vyama (vilivyopo) vya upinzani kwakuwa bado vichanga/vinakua na ndio maana 'tukubaliane' na hali ngumu zilizopo au?

Bila vyama hivi 'vichanga' kupewa nafasi kwenye ngazi za chini mpaka Ubunge na uwakilishi, kweli tutaweza kuvipima uwezo wao?

Ndio kusema Imani ya wananchi hasa asilimia 60-approx (ya wapiga kura) waliopo vijijini waendelee na imani hiyo hiyo tu kwamba maendeleo bila serikali ya CCM hayapo?

Sijui wenye mawazo ya Upinzani wanayaonaje maoni haya, au nao ndio wameshakata tamaa kama wewe :)
 
kwani wakiungana ndio watashinda bana!...vyama uchara vitajiondokea taratibu kwenye whole formula..kitu muhimu hapa ni civil education mfano..kudai katiba mpaya, tume huru ya uchaguzi kwa kutumia civil forums kama NGO, CBOna vyama vya upinzani

Well said

Mwakani utashangaa Chadema na wenzao wanaingia kwenye uchaguzi huku katiba haijabadilika na tume ya uchaguzi siyo huru,

wakati mwingine huwa nashangaa credibility za hivi vyama, unaingia kwenye ulingo ili hali unajua utashindwa , kama si kutaka ruzuku ni nini?
 
kwani wakiungana ndio watashinda bana!...vyama uchara vitajiondokea taratibu kwenye whole formula..kitu muhimu hapa ni civil education mfano..kudai katiba mpaya, tume huru ya uchaguzi kwa kutumia civil forums kama NGO, CBOna vyama vya upinzani

...hayo ya katiba mpya na tume huru si yanapitishwa kwanza bungeni? sasa imagine zaidi ya 51% wataopiga kura ya kupinga ni wabunge wa CCM!...

mabadiliko yanatakiwa yaanzie bungeni kwanza...
Vyama vya Upinzani vielekeze nguvu kwenye kutwaa majimbo ya CCm kwanza ili kuupa nguvu upinzani Bungeni...

Urahisi wa hili ni kumsimamisha mbunge mmoja wa upinzani anayekubalika na wananchi wa jimbo husika, badala ya wanavyofanya sasa kila chama kumsimamisha mgombea wake kupambana na mgombea wa CCM... watashindwa tu!

wengine sijui ni hii Ruzuku inawasumbua?...:mad:
 
Yaani! nilitaka kuandika maelezo ambayo yanashabihiana sana na yako ;). Wa kulaumiwa katika hali hii pia ni vyama vya upinzani. Pamoja na kupewa mawazo ya bure na Watanzania juu ya umuhimu wa kuungana na kuunda chama kimoja chenye nguvu ili waking'oe chama cha mafisai madarakani bado wameweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa.

Wameshashindwa chaguzi tatu sasa za tangu tuingie katika mfumo wa vyama vingi, pamoja na kuwa kunakuwa na zengwe la wizi wa kura, vitisho na vipigo toka kwa matawi ya CCM aka vyombo vya dola, lakini hawakai chini wakatafakari wafanye nini. Labda baada ya kushindwa katika chaguzi 20 au zaidi za vyama vingi ndiyo wataona umuhimu wa kuyafanyia kazi mapendekezo ya Watanzania kuhusu umuhimu wa kuungana.

...Mkubwa,

apart from CHADEMA, CUF na TLP kwa wapinzani sioni chama kingine kinachopiga kelele hadharani kwa sasa kupingana na CCM.

Zitapofikia siku za chaguzi, vyama vyote vilivyolala utaona vinaibuka kama uyoga eti navyo vinakimbilia Ruzuku tayari kwa uchaguzi. Kama sio kuharibiana Kura ni nini?

Kuna mambo mengine wala hayana haja ya kusubiri chaguzi 20 kuyabaini kwamba uchaguzi unahujumiwa kwa makusudi na hivyo vyama pandikizi sababu tu 'penye udhia inapenyezwa rupia!'...

Wakemewe wenye vyama hivyo, na wananchi tujitokeze kuvipinga na kuvikataa hadharani! mfano; (matokeo yao hawa, eti walishindana na CCM kiti cha uraisi!)...


Democratic Party -Kura 31,083
0.27%

PPT Maendeleo -Kura 18,783
0.17%

National League for Democracy -Kura 21,574
0.19%

Demokrasia Makini -Kura 17,070
0.15%

Sauti ya Umma -Kura 16,414
0.14%

Kama hayo yangekuwa matokeo ya darasani si wangekuwa wesharudishwa makwao hao? Wanatuletea utani wakati sisi wananchi tunaendelea kuteseka na matatizo lukuki nchini!
 
Kuunganba nadhani ni jambo jema ila si suluhisho.Mtaungana lakini watu hawaamini katika Muungano itakuwa ni bure .Elimu ya Uraia kwanza itawale kote na watu waelewe klwamba Upinzani na wapinzani ni Watanzania na si zaidi ya hapo . Hili ndilo muhimu na si kuunganisha vyama .Unawezaje kuwaamini CUF ukawaweka sawa na Chadema ? Jamani kuna ugumu hapo
Mkuu wangu hakuna ugumu kabisa ktk kuunganisha Chadema na CUF isipokuwa wote wameingizwa mjini na UDINI.
 
Mkuu wangu hakuna ugumu kabisa ktk kuunganisha Chadema na CUF isipokuwa wote wameingizwa mjini na UDINI.

...ubaya wenyewe huyo anayewaingiza mjini wanamjua na itikadi yake, sema wamemfumbia macho!...

Tatizo kubwa lipo kwa CUF, Kila wakijaribu kujitoa kwenye rangi ya udini, wanapakwa rangi ya Upemba... Mpaka hapo watapoweza kujinasua kwenye rangi hizi ndipo 'Kinyonga' atapojulikana...
kinyume na hapo Ushindi wao utaendelea kuishia Chumbe! Inashangaza chama hiki chenye wasomi kushindwa kuzuia 'propaganda' chafu hizi kiasi kwamba 'majority' wanaamini kweli CUF ni HIZBU!

Ama kwa CHADEMA nawasifu kuweza kujinasua kwenye dhana enzi zile za Ukabila hususan Uchagga, mpaka sasa wanajionyesha sura ya utaifa zaidi...

Vyama hivi vikiamua kuungana kiukweli, watamshinda adui anayewapaka rangi kwa propaganda za Ukabila, i.e walivyotaka kuwatumia watu wa Musoma dhidi ya Kilimanjaro hususan kwenye zengwe la Mar Chacha Wangwe nk...

UMOJA NI NGUVU, ...Upinzani hawajalijua hilo (?)
 
...mkuu, mwenzako sina mashaka na ushindi wa CUF Zanzibar.

Anyway,...ina maana wananchi hawana imani na vyama (vilivyopo) vya upinzani kwakuwa bado vichanga/vinakua na ndio maana 'tukubaliane' na hali ngumu zilizopo au?

Bila vyama hivi 'vichanga' kupewa nafasi kwenye ngazi za chini mpaka Ubunge na uwakilishi, kweli tutaweza kuvipima uwezo wao?

Ndio kusema Imani ya wananchi hasa asilimia 60-approx (ya wapiga kura) waliopo vijijini waendelee na imani hiyo hiyo tu kwamba maendeleo bila serikali ya CCM hayapo?

Sijui wenye mawazo ya Upinzani wanayaonaje maoni haya, au nao ndio wameshakata tamaa kama wewe :)

Mkuu kwanza hizo kura za maoni za REDET siziamini sana mpaka hapo nita kapo jua size ya sample ilikua ni ngapi, maswali gani yaliulizwa na ni watu wapi haswa wameulzwa.

Mimi nadhani vyama vya upinzani lazima vijijengee jina haswa in rural areas ambapo ndiyo asilimia kubwa ya wapiga kura wapo. Kama umegundua kelele nyingi za ufisadi nk zina toka kutoka population za mijini ambapo wana access na habari mbali mbali. Hivi haujiulizi kwa nini watu wana piga kelele lakini bado CCM inashinda? Kwa sababu sisi tunaopiga kelele tuna represent asilimia ndogo sana ya wapiga kura wote.

Sawa labda CCM ina fanya faulo za hapa na pale lakini siamini kabisa kwamba kuna chama cha upinzani kina uwezo wa kuchukua idadi kubwa ya wabunge na uraisi. Kwa huko Z'bar sijui....
 
kwani wakiungana ndio watashinda bana!...vyama uchara vitajiondokea taratibu kwenye whole formula..kitu muhimu hapa ni civil education mfano..kudai katiba mpaya, tume huru ya uchaguzi kwa kutumia civil forums kama NGO, CBOna vyama vya upinzani

Na hilo jukumu la kutoa civil education ni la nani kama siyo vyama vya upinzani? Tuwe wakweli bwana nani atampa advantage mpinzani wake? CCM na serikali yake lazima inajua kuwa civil education will work against them so usi tegemee hata siku moja wao wataipa kipaumblele.
 
Mkuu kwanza hizo kura za maoni za REDET siziamini sana mpaka hapo nita kapo jua size ya sample ilikua ni ngapi, maswali gani yaliulizwa na ni watu wapi haswa wameulzwa.

Mimi nadhani vyama vya upinzani lazima vijijengee jina haswa in rural areas ambapo ndiyo asilimia kubwa ya wapiga kura wapo. Kama umegundua kelele nyingi za ufisadi nk zina toka kutoka population za mijini ambapo wana access na habari mbali mbali. Hivi haujiulizi kwa nini watu wana piga kelele lakini bado CCM inashinda? Kwa sababu sisi tunaopiga kelele tuna represent asilimia ndogo sana ya wapiga kura wote.

...kwa mujibu wa hiyo link wanasema hivi;

2.0 Mfumo wa Ukusanyaji Maoni
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]Sampuli ilichaguliwa kufuata muundo wa kiutawala yaani mikoa, wilaya, kata na vijiji au mitaa. Kwa kutumia njia ya sampuli nasibu (random sampling) sampuli ilichaguliwa ili kujumuisha watu wa sifa na aina mbalimbali. Katika kila mkoa, wilaya moja ilichaguliwa. Jumla ya watu 50 walichaguliwa katika kila wilaya. Ili kuweza kupata wahojiwa (respondents), orodha ya kata, vijiji, mitaa, na wakaazi zilitumika katika mchakato mzima wa kupata sampuli. Orodha za wakaazi katika kijiji au mtaa zilipatikana kutoka kwa viongozi wa serikali za mitaa.1 Wahojiwa wote ilibidi wawe wale tu waliokuwa na umri wa miaka 18 na zaidi. Sampuli hii inajumuisha idadi inayolingana ya wanaume na wanawake. Pia, wahojiwa walichaguliwa kufuatia mgawanyo wa idadi ya watu hapa nchini, asilimia 60 ya vijiji na mitaa ilichaguliwa kutoka mazingira ya shamba (rural areas) na asilimia 40 kutoka katika mazingira ya mjini (urban areas). [/FONT]

[FONT=Times New Roman,Times New Roman]1 [/FONT]
[/FONT][FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]Katika maeneo ambayo orodha hizi hazikuwepo, watafiti waliweza kuziandaa wakisimamiwa na viongozi wa serikali za mitaa na watafiti wakuu wa REDET. [/FONT]
[/FONT]
2
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]Maswali yalikuwa ni mafupi, yaliyohitaji majibu bayana kuhusu matakwa ya wapiga kura katika uchaguzi mkuu ujao. Pia kulikuwa na maswali yahusuyo mchakato wa uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya siasa na matatizo nyeti ambayo wapiga kura wangependa serikali ijayo iyatilie mkazo.2 Kama ilivyo desturi katika tafiti za REDET, watafiti wasaidizi walisimamiwa na maprofesa na wahadhiri waandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. [/FONT]
[/FONT]

...Sawa labda CCM ina fanya faulo za hapa na pale lakini siamini kabisa kwamba kuna chama cha upinzani kina uwezo wa kuchukua idadi kubwa ya wabunge na uraisi. Kwa huko Z'bar sijui....

...Mkubwa, huko Zanzibar hasa Pemba CCM wanapelekeshwa mchakamchaka kila chaguzi! Kukubalika kwa Upinzani hakutokani na Uwezo pekee wa kushinda, ni pamoja na kukubalika vilevile...

Kwa mfano, jiulize kwanini katika wilaya ya Temeke tu hapa Dar CCM inapelekeshwa mchakamchaka iwapo (CCM) wanakila uwezo wa kushinda -wakitaka! ...si kuwajengea tu mabarabara, maji, umeme wa uhakika nk 'labda' wananchi watawakubali?...
 
...kwa mujibu wa hiyo link wanasema hivi;


O.k thanks for these details mkuu.



...Mkubwa, huko Zanzibar hasa Pemba CCM wanapelekeshwa mchakamchaka kila chaguzi! Kukubalika kwa Upinzani hakutokani na Uwezo pekee wa kushinda, ni pamoja na kukubalika vilevile...

Kwa mfano, jiulize kwanini katika wilaya ya Temeke tu hapa Dar CCM inapelekeshwa mchakamchaka iwapo (CCM) wanakila uwezo wa kushinda -wakitaka! ...si kuwajengea tu mabarabara, maji, umeme wa uhakika nk 'labda' wananchi watawakubali?...

Mkuu CCM kushinda mimi nime maanisha kushinda kiujumla kama kuwa na majority bungeni na kushinda uraisi. Siku maanisha hata kidogo kuwa watashinda kila jimbo.....that's impossible. Hilo swala la barabara, maji nk nakubaliana na wewe but I seriously doubt it kwamba upinzani ungeingia wangeweza pia kufanya yote hayo. Anyway ni mtazamo tu tuendelee kujadiliana.
 
Jamani,

Mimi nimepata funzo kutoka kwenye uchaguzi wa vitongoji/mitaa; sikuwa nawasikia CHADEMA, CUF etc... In fact akina CHADEMA walikuwa busy na kujitafutia masifa binafsi! Kama walivyo vinara wawili wanaopenda majisifaaaa.... yet hawakisaidii chama.
 
Mkuu CCM kushinda mimi nime maanisha kushinda kiujumla kama kuwa na majority bungeni na kushinda uraisi. Siku maanisha hata kidogo kuwa watashinda kila jimbo.....that's impossible. Hilo swala la barabara, maji nk nakubaliana na wewe but I seriously doubt it kwamba upinzani ungeingia wangeweza pia kufanya yote hayo. Anyway ni mtazamo tu tuendelee kujadiliana.

...hawataweza kufanya yote lakini angalau wanaweza kutoa changamoto yafanyike angalau nusu ya haya...


Ufisadi kwenye ununuzi wa Radar, Umeme wa Richmond, Mkataba wa Mgodi wa Buzwagi, Tuhuma za EPA,... na mengineyo yameibuliwa machoni mwa watanzania kwa juhudi binafsi za wabunge wa Upinzani.


Tatizo lililopo sasa, baada ya kuibuliwa hayo hatua gani zinachukuliwa kwa wahusika? kwa walio wepesi kusahau, kuna maneno 'matamu-matamu' yalitamkwa;

"...Serikali ya Awamu ya Nne itaendeleza vita dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi, tena kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Serikali ya Awamu ya Nne itatimiza ipasavyo wajibu wake wa utawala na maendeleo, na itaendesha dola kwa misingi ya utawala bora na uwajibikaji; utawala wa sheria unaoheshimu na kulinda haki za binadamu;" -JK

“...Nitawapa utumishi makini na uliotukuka.” -EL

"...natangaza uongozi wa Bunge wa 'kasi na viwango’ (Speed & Standards), " -S6

Rais aliyedai anawafahamu wala rushwa imekuwaje tena anadai apewe majina?

source; http://www.chadema.or.tz/makala/makala.php?id=125
 
Well said

Mwakani utashangaa Chadema na wenzao wanaingia kwenye uchaguzi huku katiba haijabadilika na tume ya uchaguzi siyo huru,

wakati mwingine huwa nashangaa credibility za hivi vyama, unaingia kwenye ulingo ili hali unajua utashindwa , kama si kutaka ruzuku ni nini?

CCM kamwe hawawezi kubadilisha katiba au kuweka tume ya uchaguzi iliyo huru kwa hiari yao. Hawako civilized kiasi hicho. Lakini yapo mambo mawili ambayo yatawezesha hayo kufanikiwa. Moja, ni kuingia kwenye uchaguzi hivyo hivyo na kupambana nao kwa muda mrefu, kujijenga na hatimaye kuwa na viti vingi bungeni. Halafu kujenga hoja bungeni mpaka wabunge wa CCM wenye hekima kuiunga mkono hiyo hoja, tupate kura za kutosha, katiba ibadilishwe. Au wafadhili kuwalazimisha kuwa na uchaguzi uliyo huru kama tulivyolazimishwa kuachana na siasa za chama kimoja na kuwa na siasa za vyama vingi. Sasa hatuwezi kukaa na kusubiri wafadhili, inabidi tupambane nao hivyo hivyo. Juhudi zikionekana, wafadhili wakaingilia, mchakato utaharakishwa.


Na hilo jukumu la kutoa civil education ni la nani kama siyo vyama vya upinzani? Tuwe wakweli bwana nani atampa advantage mpinzani wake? CCM na serikali yake lazima inajua kuwa civil education will work against them so usi tegemee hata siku moja wao wataipa kipaumblele.

Jukumu la kutoa civil education ni LAKO, langu, la mashule yetu, asasi za kijamii, TAMWA, HAkielimu, madhehebu ya dini, vyama vya wafanyakazi, kwa ujumla ni letu sote wenye uchungu na nchi hii. Vyama vya siasa vitoe hiyo elimu kwa uwezo upi? Inahitajika pesa, itoke wapi?

.
 
Back
Top Bottom