Uswahiba Wa Marekani na Pakistani Umefikia Ukingoni?

AljuniorTz

JF-Expert Member
Jan 6, 2009
544
17
Wiki iliyopita Rais wa Pakistani Asif Ali Zardari, alipitisha maazimio ya kuruhusu kutumika kwa SHERIA ZA KIISLAM (SHARIAH)

Hali hiyo imepelekea mtikisiko mkubwa kwa serikali ya uongozi wa Barak Hussein Obama, na hasa upande wa kiusalama. Kubwa linalowatisha maofisa wa usalama wa Marekani ni kuwa wanahisi Pakistani inaelekea kujitangaza kuwa ni Islamic State; hivyo kuna uwezekano mkubwa ikawa ndio kambi rasmi ya Wanaharakati wa Kiislam.

Ikumbukwe kuwa Palistani wanamiliki silaha za NYUKLIA zaidi ya 100 na wanajeshi kubwa zaidi ya Marekani

Jana bibi Hilary Clinton alipigia mstari mweusi kuhusu Pakistani na kusema nchi hiyo (Pakistani)inaeleka kutii na kukubali kila linalosemwa na Wataliban ili kusitisha mapambano yao badala ya kutumia nguvu za kijeshi kuwafusha kutoka ktk maeneo wanayoyakalia.

Bibi Clinton alimaliza hotuba yake kuhusu Pakistani kwa kuwaomba Wapakistan wote DUNIANI kuzungumzia suala hilo dhidi ya SERIKALI YAO ili wasikubali kushindwa dhidi ya aliowaita ni magaidi ambao ni KITISHO KIKUBWA.


PH2009042203915.jpg

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI ALIPOKUWA AKIJIBU MASWALI MBALIMBALI, HAPO CAPITAL HILL

More Info gonga hapa : U.S. experts: Pakistan on course to become Islamist state | McClatchy

http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/content/article/2009/04http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/content/article/2009/04/22/AR2009042203913.html?hpid=topnews/22/AR2009042203913.html?hpid=topnews
 
Back
Top Bottom