Usimfanye mkeo raha akazitafute nje ya ndoa!

Mmmh ntajuaje mie...labda kwasababu kule ukijitahidi UNATUNZWA!

mmmh.....kula na kulipa ndo mtindo wa kisasa,
asante, nimeipata hiyo!!!
lakini nilidhani nyumbani ndo kuna malipo mengi zaidi kuliko ya nje.............................
 
mmmh.....kula na kulipa ndo mtindo wa kisasa,
asante, nimeipata hiyo!!!
lakini nilidhani nyumbani ndo kuna malipo mengi zaidi kuliko ya nje.............................

Ingekua hivyo basi maujuzi yote yangebaki kwaajili ya mhusika/mstahili mkuu.
 
Ingekua hivyo basi maujuzi yote yangebaki kwaajili ya mhusika/mstahili mkuu.

kwahiyo hapa Lizzy tukubaliane kuwa,
wanando wanapeana uvivu katika kutimiza majukumu yao ya kimsingi,
matokeo yake hasira wanaziamishia nje.....................
 
..mkuu sasa kama tunaufuata huo ufundi kwa mahawala tufanyaje?

Hapo kwenye rangi hapo. Mnapaswa kuwapa maufundi wake zenu wa ndoa sio mahawara, vinginevyo ndo hivyo tena mkeo atatoka nje. Utajisikiaje mkeo akitoka nje kwa sababu wewe uliachakumfundisha au kusema unachokifurahia ili yeye akifanye!
 
Heshima kwenu wakuu,
Mimi naamini wanawake wengi ni waaminifu na ni wavumilivu sana katika ndoa, sio rahisi sana mwanamke kutoka nje bila sababu ya msingi, na ukiona katoka ujue basi uvumilivu umemshinda.

Ukweli uko hivi, Wanaume wengi wanamtumia mwanamke kama sehemu ya kujifurahisha bila kujua kua wanawake nao wanahitaji kufurahi. Wanaume wengi wakiwa kwenye ule mchezo wa kufurahisha hawajibidishi wala hawajali kuona wenza wao wanaridhika, wanachoangalia ne wenyewe kujiridhisha na baada ya hapo wanakugeuzia mgongo na kuchapa usingizi. Mwanamke atahangaika usiku kucha na mchana kutwa maana haja yake haikutimia(hakutosheka), hii hali ikijirudia mara kwa mara mwanamke uvumilivu unamwishia na haoni haja hata ya kukutana na mmewe maana anaona hana maslahi yoyote kwa kukutana kwao.
Hili linapelekea wanawake wengi kutokua na hamu na kale kamchezo na baada ya mda hamu inapokuwepo anatafuta mtu hata kama ni mara moja kwa mwezi lakini amfikishe.

Ombi langu kwa Wanaume:
Jiulize ni kwa nini mkeo hataki/hajisikii kufanya tendo la ndoa. Je juzi na jana ulimfikisha. kama sio jirekebishe.
Wanawake wanajua wazi kua sio siku zote Mme anaweza kumfikisha na yuko tayari kuvumilia hilo, ila inapokua too much na mme haoneshi bidii yoyote basi Mwanamke anatoka.

Nawakilisha...
 
hivyo vitu adimu kuvipata huko nyumbani kwetu,
ndio haswa inabidi tuvibainishe ili hawa wake zetu,
kama ni mapungufu waliyonayo basi wayarekebishe.....................

Watajuaje kama wana mapungufu kama haujasema??
 
Heshima kwenu wakuu,
Mimi naamini wanawake wengi ni waaminifu na ni wavumilivu sana katika ndoa, sio rahisi sana mwanamke kutoka nje bila sababu ya msingi, na ukiona katoka ujue basi uvumilivu umemshinda.

Ukweli uko hivi, Wanaume wengi wanamtumia mwanamke kama sehemu ya kujifurahisha bila kujua kua wanawake nao wanahitaji kufurahi. Wanaume wengi wakiwa kwenye ule mchezo wa kufurahisha hawajibidishi wala hawajali kuona wenza wao wanaridhika, wanachoangalia ne wenyewe kujiridhisha na baada ya hapo wanakugeuzia mgongo na kuchapa usingizi. Mwanamke atahangaika usiku kucha na mchana kutwa maana haja yake haikutimia(hakutosheka), hii hali ikijirudia mara kwa mara mwanamke uvumilivu unamwishia na haoni haja hata ya kukutana na mmewe maana anaona hana maslahi yoyote kwa kukutana kwao.
Hili linapelekea wanawake wengi kutokua na hamu na kale kamchezo na baada ya mda hamu inapokuwepo anatafuta mtu hata kama ni mara moja kwa mwezi lakini amfikishe.

Ombi langu kwa Wanaume:
Jiulize ni kwa nini mkeo hataki/hajisikii kufanya tendo la ndoa. Je juzi na jana ulimfikisha. kama sio jirekebishe.
Wanawake wanajua wazi kua sio siku zote Mme anaweza kumfikisha na yuko tayari kuvumilia hilo, ila inapokua too much na mme haoneshi bidii yoyote basi Mwanamke anatoka.

Nawakilisha...
Aya yako ya kwanza inapotosha sana!!
 
Hapo kwenye rangi hapo. Mnapaswa kuwapa maufundi wake zenu wa ndoa sio mahawara, vinginevyo ndo hivyo tena mkeo atatoka nje. Utajisikiaje mkeo akitoka nje kwa sababu wewe uliachakumfundisha au kusema unachokifurahia ili yeye akifanye!

labda safina cha kujiuliza hapa ni kwamba,
kwani hayo maufundi mke hawezi kuyaanzisha yeye,
kiasi kwamba mume akapagawa na kuhairisha mipango yake ya nje?
 
una maanisha nini Lizzy?

Maana yake ni kwamba anahalalisha kutoka nje ya ndoa upande wa wanawake kwa kisingizio kwamba hua lazima wawe na sababu....utadhani kuna mtu anaekubaligi kaosa bila kusingizia mtu/kitu kingine kua chanzo.
 
..........hii ilikuwa ni kauli ya Kungwi mmoja maarafu,
mjini DSM;alikuwa akimfunda binti na kisha akawageukia na akina baba/wanaume,

Akazidi kusema......................

''Nawaambia akina baba/wanaume mkome kuwafanya wake zenu,
kuwa dada zenu, utundu na ufundi wote mwaupeleka kwa mahawala,
matokeo yake wake zenu wanaanza kutoka nje ya ndoa.''

Akazidi kusema...........................

''Wewe mume usimwonee huruma punda kwani kupigwa bakora,
ndiyo furaha yake, kama gari kanyaga mpaka chini,
hakuna aliyewahi kutoboa eksileta kwa kukanyaga mafuta.''

Wapendwa wanajamii wenzangu, habari ndo hiyo,
sijui nyie mwasemaje?
Mie nilibaki natikisa kichwa tu!!!!!!!!!!!!!!!!
MBARIKIWE SANA!!!!!

Huyo Kungwi, mbona tena kapita mipaka!, yeye aliitwa afunze Binti, mbona aongeza na mafunzo/maonyo kwa Waume???.

Na jee hao Waume walikuwa wafanya nini hapo kwenye unyago/Kitchen party??,

Mambo mengine jamani!!!!!!
 
Sasa Shantel, binafsi sijakataa hilo,
ila hebu nisaidie hapo kwani ufundi unatakiwa uonyeshwe
na baba/wanaume tu?
Nimeongelea wababa sababu ndio wamebanwa kwenye hii thread umenielewa mkuu? maujuzi mke atampa nani sasa wakati anaiona mara moja kwa mwezi na siku akiipata anakuwa na maswali mengi kichwani hii inapunguza usanifu wa kujishughulisha umenipata bacha!
 
..mkuu sasa kama tunaufuata huo ufundi kwa mahawala tufanyaje?
Msijisahau kwamba wenzenu wako home na wanawatemea nyie tu muwape hizo raha sasa kama unakuwa bize nje unadhani utapaa muda wa kumuwazia wa ndani?
 
..........hii ilikuwa ni kauli ya Kungwi mmoja maarafu,
mjini DSM;alikuwa akimfunda binti na kisha akawageukia na akina baba/wanaume,

Akazidi kusema......................

''Nawaambia akina baba/wanaume mkome kuwafanya wake zenu,
kuwa dada zenu, utundu na ufundi wote mwaupeleka kwa mahawala,
matokeo yake wake zenu wanaanza kutoka nje ya ndoa.''

Akazidi kusema...........................

''Wewe mume usimwonee huruma punda kwani kupigwa bakora,
ndiyo furaha yake, kama gari kanyaga mpaka chini,
hakuna aliyewahi kutoboa eksileta kwa kukanyaga mafuta.''

Wapendwa wanajamii wenzangu, habari ndo hiyo,
sijui nyie mwasemaje?
Mie nilibaki natikisa kichwa tu!!!!!!!!!!!!!!!!
MBARIKIWE SANA!!!!!

Sasa kama gari haina mafuta utajikanyagia tu?
 
Huyo Kungwi, mbona tena kapita mipaka!, yeye aliitwa afunze Binti, mbona aongeza na mafunzo/maonyo kwa Waume???.

Na jee hao Waume walikuwa wafanya nini hapo kwenye unyago/Kitchen party??,

Mambo mengine jamani!!!!!!

chiko,unajua kungwi aliyasema haya maneno,
kama kauli ya kuwaasa wanaume popote pale walipo,
wamsikie na wajirekebishe..............................................
 
Yipeeee acha awaambie hao wababa wakware, hivi mnapopeleka ujuzi wote nje mnataka wake zenu waonyeshwe na nani huo ujuzi?
au utakuta mtu kwa mkewe mstaarabu akienda nje ndio anaonyesha uchakaramu wake, nani kawaambia wake hawapendi waume machakaramu


ivi BB, pale juu kwen post ya Shantel, umegonga senks, ina maana umekubaliana na mawazo yake yote ama baadhi.:ranger:
 
Back
Top Bottom