Watu wengi huingia kwenye migomo mbalimbali kwa kukurupuka na matokeo yake ni kushindwa kufikia malengo yao.Watanzania wengi hasa walio kwenye ajira hutegemea mishahara na posho ambapo hawana hakiba ya kuendesha maisha yao hata kwa mwenzi mmoja.Hata huu mgomo wa walimu sidhani kama watafanikiwa kwa kiwango wanachotarajia kwani wengi hutegemea ajira tu na hawana namna ya kuenendesha maisha yao bila mshahara. Hii ndiyo maana ukifika tarehe za mwisho wa mwezi walimu hufurika kwenye mabenki ili kuchukua mishahara yao ili wasije wakaadhirika.Nashauri walimu pamoja na wafanyakazi wengine wajitahiti sana kuwa na vyanzo mbadala vya mapato ili wasitishwe na vitisho vya kuwafukuza kazi n.k. Ukiwa unategemea mshahara tu ni rahisi sana kutishwa na kama unategemea mshahara tu nashauri uwe mpole maana huna jeuri kwa mwajiri. walimu watakapofika kwenye mabenki na kukuta mishahara yao haijaingizwa nadhani kesho yake msimamo utalegea, ila wakijihadhari mapema na kuhakikisha wana vyanzo vya pesa vingine hilo halitakuwa tatizo.!!!