Usichukulie poa,laif samtaimz inaboa!

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,385
Wanangu!
Msione humu rodi majita wanakatiza wako smati nini wanasmaili, ukimsalimiamwana anakwambia poa tu, hizi buku, buku mbili nini sio tatizo kumkuta kwa mama nanii anapiga mbili, umeona?

Sio kwamba huyu jamaa fresh ile kiukweli, ..kajaribu tu kukopu na hii laifu lakini kiukweli kabisa mwanangu mwenyewe, laifu mizinguo!
...amini usiamini...

Watu wameamua tu, kuchukulia poa maana hata ukisema unanyongea nini unakuwa mtu wa filingi deile, sana sana utaishia kudedi bila sababu ya msingi ujue? Watu wanaamka tu wanakuta mwana wa zamaaaaani keshaaga, wanaaza kuleta zile za marehemu hakuugua kumbe mwanangu ushasafa sana maisha haya.

Halafu kitu kingine kuna wana wanajisahau kabisa maisha yaha ujue, kuna taimu inafika, mwana anahisi kabisa kwamba keshamaliza mchezo kumbe bwana dunia hii hakuna kumaliza, kama kujifunza basi deile mwanangu topikimpya zinaibuka,mtu unadedi huku unajifunza maisha haya mchizi wangu hujaishtukia hiyo?

Asa kuna mwanangu mmoja mitaa ya Tabata unaambiwa imemkuta ishu hiyo kilaakijaribu kusovu, inamzingua, haya mambo yetu ya malavidavi na mademu zetu unaambiwa, inabidi kama tupunguze spidi hivi vinginevyo mtu unaweza kujikuta umerudi skwea wani.

Sasa mchizi unaambiwa sio kwamba ni suala la demu tu, waifu kabisa unaambiwa kazingua, kamuacha mchizi nje wakati mwana alikuwa keshamaliza kila kitu, ana mjengo wake, mkoko nini, na bado biznes mbili tatu zinamsukuma katika suala zima la kukamatia deile bredi, sasa hivi mwanetu hana kitu.
Unajua ikoje?

Mchizi kaoa kabisa demu unaambiwa na wana watoto nini, ..laifu inasonga,na katika laifu ya mtu na waifu wake si unajua mizingulizi haikosekani?

Wahenga unawakumbuka? Basi jamaa wale wanakwambia huwezi kula muwa bila kukuta fundo, kwa hiyo jamaa wakakuta fundo, ...wakazinguana!

Kila walipojaribu kusovu unaambiwa maza anaonekana kama hamaindi hivi kurudisha moyo kwa mwana, akawa anaonekana kama anataka kufunga pazia lenyewe, apewe mauhuru nini asonge, lakini mwana akawa kila akimaindi madogo nini pale homu kusavaivu bila maza ingekuwa mizinguo, akawa kama anagoma hivi kutoa divosi yenyewe.
Unaona mwanangu?

Maza kuona mchizi kagomakuachia uhuru nini, akasonga fronti unaambiwa, mahakamani nini, akaipeleka ishu nzima nzima kwa bwana Pilato, pilato akaichekiiiiiii akaona hata hapa huyu maza kama kashakuwa na msimamo wake hivi, hata mwana akifosi amani itakuwa haipo homu, akawa kama anataka kuitenganisha hivi ndoa, basi akaamuru talaka itoke.

..dizaini kama talaka ilitoka, maza akasepa!
Kumbe bwana maza kashakula mchongo longtaimu kuhusiana na mjengo na kila kitu, hati si mtu mzima alimkabidhi waifu ndio atunze? Kaenda tu kujiandikisha kama kauziwa nini, akajihamishia mazaga yoye yakawa kwa jina lake, halafu akayapigilia bei kwa mbali kudadadeki.

Mchizi siku hiyo karilaksi siting rumu anakulakitu cha TV, wanaingia majita wanampa zipi ujue?
"Mwana eeh, inabidi kama mwezi ujao hivi usepe, sababu, mwenye nyumba anataka kuhamia".
Pata picha ingekuwa wewe mwanangu ungedataje?

Mwana alidata ujue akaanza kuhamaki, sikaja dokyumentsi unaambiwa mwanzomwisho zinamsapoti mnunuzi, mwenyewe akaanza kuhaha alipoenda kwenye kabati akakuta kweupe, maza kumbe alishasonga nazo fronti longtaimu ujue?Dah...

Sasa hivi mwana karudi mwanzoni tu kama anaanza upya laifu, watoto hawana pa kuishi, yaani laifu imekuwa kama inaanza tena hivi wakati mwana alishajitosheleza kwa kila kitu ujue? Mademu zetu hawa unaambiwa, wa kuwaangalia sana ujue hawa la sivyo wanaweza kutupeleka ambako siko ujue?

Mi naishia hapa wanangu, tutachekiana au sio?
Wanlav!
 
hahaha,wanlav bingwa! uko kijiwe cha wapi nije nigongee manake nna mzuka na cha ngaramtoni ile mbaya yake, na leo niko alosto ile mbaya. usinione nasmaili nini, ila kiukweli mambo ndivyosivyo. usintenge basi bingwa,ama sio! manake wan'dei yes nikizamia meli nikaibukia abrodi ntakukumbuka masela wangu
 
hahaha,wanlav bingwa! uko kijiwe cha wapi nije nigongee manake nna mzuka na cha ngaramtoni ile mbaya yake, na leo niko alosto ile mbaya. usinione nasmaili nini, ila kiukweli mambo ndivyosivyo. usintenge basi bingwa,ama sio! manake wan'dei yes nikizamia meli nikaibukia abrodi ntakukumbuka masela wangu
hahahaha!! bingwa uskonde..ngoja kidogo nitakushtua si unajua wana wa kitaa nini sku hizi wanamind mtu ukiwa new pale kijiwe?..kuna soo ilitokea si unajua nini aliibuka mwana kijiwe nini tukamwagiana mastori kibao .uyu mwana akadai kuwa alikuwa mbele kitambooo. kumbe yule mwana alikuwa njagu.si unajua balaa lake?akaenda akawatonya wenzake basi ikabidi tuwaachie chenji pale na kijiwe tukakiua , sema haina majotrooooooo,
one day nini nitaku alert.
 
tehe tehe tehe

Siku hz naona umeamua kuja na stori za kitaa...lol wape hi masela mwana.. One love 4reva...
 
msiwamaindi wala nini, si unajua njaa town haichagui sura bingwa? sasa si unajua mzuka hausubiri wala nini, na unajua tena washkaji zako wakiona shori na kigiza kishatua basi inakuwa kelele miingi,wasije wakakumaindi nini na kukutenga wakidhani ww sio mgumu. basi nistue mapema bingwa manake na mi giza nini inakuwa soo si unaelewa wangu? poa basi bestee, mi nakuskizia utanstua, niko humu leo kutwa nzima napunguza maisha!

hahahaha!! bingwa uskonde..ngoja kidogo nitakushtua si unajua wana wa kitaa nini sku hizi wanamind mtu ukiwa new pale kijiwe?..kuna soo ilitokea si unajua nini aliibuka mwana kijiwe nini tukamwagiana mastori kibao .uyu mwana akadai kuwa alikuwa mbele kitambooo. kumbe yule mwana alikuwa njagu.si unajua balaa lake?akaenda akawatonya wenzake basi ikabidi tuwaachie chenji pale na kijiwe tukakiua , sema haina majotrooooooo,
one day nini nitaku alert.
 
msiwamaindi wala nini, si unajua njaa town haichagui sura bingwa? sasa si unajua mzuka hausubiri wala nini, na unajua tena washkaji zako wakiona shori na kigiza kishatua basi inakuwa kelele miingi,wasije wakakumaindi nini na kukutenga wakidhani ww sio mgumu. basi nistue mapema bingwa manake na mi giza nini inakuwa soo si unaelewa wangu? poa basi bestee, mi nakuskizia utanstua, niko humu leo kutwa nzima napunguza maisha!
uskonde malaika,mimi kama vipi mida ya jioni kiaina hivi nitakucheki nini ..kigiza kisikuogopeshe mtu wangu kwangu huu mkoko wa kitaa nini nitaupiga fulu tenki na nikaunguza wese hadi homu kwenu,siunajua mwisho wa mwezi? mazeri wa kitaa katoa dili basi nikawashtua wana nini tukatia chetu mfukoni tukasepa...sasa hivi tunakula stori na wana nini manake mimi ndio faza wakijiwe baada ya kugongewa kitu pale ubalozini cha kwenda mbele.kwa hiyo mimi nitatangulia then nitawapa mchongo masela wote wa kijiwe nao wajikate zao mbele ci unajua?basi michongo yenyewe kama ndo hii mimi nitakucheki wana nikiwaambia kuwa huyu ni shori wangu basi wenyewe watachili.
 
hahaha,maneno ya kijiweni yameniishia,najiskia kama nshavuta ganja tayari,lol! inabidi unipeleke kijiweni aisee
uskonde malaika,mimi kama vipi mida ya jioni kiaina hivi nitakucheki nini ..kigiza kisikuogopeshe mtu wangu kwangu huu mkoko wa kitaa nini nitaupiga fulu tenki na nikaunguza wese hadi homu kwenu,siunajua mwisho wa mwezi? mazeri wa kitaa katoa dili basi nikawashtua wana nini tukatia chetu mfukoni tukasepa...sasa hivi tunakula stori na wana nini manake mimi ndio faza wakijiwe baada ya kugongewa kitu pale ubalozini cha kwenda mbele.kwa hiyo mimi nitatangulia then nitawapa mchongo masela wote wa kijiwe nao wajikate zao mbele ci unajua?basi michongo yenyewe kama ndo hii mimi nitakucheki wana nikiwaambia kuwa huyu ni shori wangu basi wenyewe watachili.
 
Mwana hiyo flow blow by blow, mpaka pigo la below, daaaaaayum.

Nimekuona nimekuona. Ndiyo maana machizi wengine tunaamua kusepa kiseja ka watawa au kama ndani ya Kishtobe maji marefu, au unakamata kitu bila mpango wa midokyumenti wala nini, kwa maana ukienda mimbari maana yake ushakubali angalau kuchukua fifty, na masela washasota sana usawa huu kuchukua fifty, achilia mbali kupigwa chini hundred kabisa kama uzushi wa viwanja vingine tulivyo huku.

Ndiyo maana mi nawaangalia tu masela wanaoingia kichwa kichwa kwa sunguratope machojuu, inatokea mtu anapigwa mbata mpaka kuona nyota kama hivyo, anadata hivihivi.

Ndiyo maana masela wengine tunakwambia kuoa ndoto, hata aje sista wa Kirumi. Tunabakia "Raiders of The Lost Ark" kama vile babu Ford. Nyie oeni tu, si tuna-raid.
 
Mwana hiyo flow blow by blow, mpaka pigo la below, daaaaaayum.

Nimekuona nimekuona. Ndiyo maana machizi wengine tunaamua kusepa kiseja ka watawa au kama ndani ya Kishtobe maji marefu, au unakamata kitu bila mpango wa midokyumenti wala nini, kwa maana ukienda mimbari maana yake ushakubali angalau kuchukua fifty, na masela washasota sana usawa huu kuchukua fifty, achilia mbali kupigwa chini hundred kabisa kama uzushi wa viwanja vingine tulivyo huku.

Ndiyo maana mi nawaangalia tu masela wanaoingia kichwa kichwa kwa sunguratope machojuu, inatokea mtu anapigwa mbata mpaka kuona nyota kama hivyo, anadata hivihivi.

Ndiyo maana masela wengine tunakwambia kuoa ndoto, hata aje sista wa Kirumi. Tunabakia "Raiders of The Lost Ark" kama vile babu Ford. Nyie oeni tu, si tuna-raid.
hahah! Kiranga kumbe nawe umo? hahaha..wewe jamaa upo pande zote kama kama kuta za yai. pamoja mzeya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom