Ushuhuda Toka Loliondo....Serikali Inaficha Nini Loliondo..Wakati Wanajua Hakuna Tiba?

This is a b..... f..... government and their leaders -- kuendekeza vitu vya imani huku watu wanakufa. Katika miaka ya mwanzoni ya 80 Nyerere alimfukuza kasi DC mmoja (enzi hizo wakiitwa ma-AC) Idi Sungura kwa kuendekeza mambo kama haya.

Gazeti la The African la Jumamosi hii lina habari ukurasa wa mbele kuhusu malalamiko ya mratibu wa masuala ya HIV/Aids Mkoa wa Manyara aitwaye Elizabeth akisema tangu Babu aanze tiba yake wanaokwenda kupima vvu kwa hiari kutoka mkoa huo na wale wanaoutumia ARVs imepungua sana. Gazeti lilimnukuu mratibu huyo akilalamika kwamba wanaogua ukimwi hawaendi kupata dawa zao kama zamani na akasema kwamba wala hawaendi kupima tena wanaporudi baada ya kupata kikombe kwa babu.

Hii sasa ni hatari -- ile kampeni nzima ya JK aliyoanzisha ya kupima vvu kwa hiari sasa inakufa na watu wanakufa, huku yeye mwenyewe wala hatoi tamko lolote -- kwa mfano kuwahimiza wale wenye vvu wakitoka kwa Babu waendelee na ARvs.
 
Usiende kipolitik kwa babu utarudi na ugonjwa wako,tulia jipange kiimani zaidi usimtest babu,musa alitumia fimbo kugawa bahari ya shamu.YESU alimpaka matope kipofu aliponawa akaona.kanywe kikombe tena kwa unyenyekevu utapona kama wenzako.HALELUYA BABU UKO JUU.
 
Mimi nazungumzia ushuhuda wa watu niliowaona, watatu ni ukimwi karibu wote wanaendelea vizuri. Kisukari hao ndiyo wengi kabisa, sasa sijui kwako mpendwa lakini nionavyo muda si mrefu ukweli utajulikana kuhusu babu wa Loliondo. Lakini mpaka sasa imani ya watu ipo juu ya tiba ya babu.
 
Pole sana, watu wamepona wengi tu. Ili wewe naona issue yako ni serious anza kuhesu siku

Mzee hii sasa dhihaka. Mtu anatoa ushuhuda wewe unamdhihaki hii si haki. Kama kuna watu wamepona unatakiwa na wewe utoe ushuhuda hapa jamvini. Ushuhuda wa kupona ni vyeti vya daktari kabla na baada ya kupata kikombe vinginevyo tutakuwa tunawadanganya Wadanganyika wetu ili wafe kwa imani potofu kwamba kikombe kinaponya magonjwa sugu.
 
Ki ukweli hakuna aliyepona kutokana na hiyo dawa ya loliondo, na hakuna atakaye pona...!

Na wale washabiki wa huyu kigagula, watakuja na visingizio vyao kuwa watu hawaponi kwa sababu hawana imani.

Kuna dada mmoja ameohojiwa kwenye kipindi cha njia panda... Naye anadai kuwa amepona ila kupima tena hajapima ili kuthibitisha madai yake... kwa ufupi anakubali kuidanganya nafsi yake kuwa amepona.
 
Mimi nazungumzia ushuhuda wa watu niliowaona, watatu ni ukimwi karibu wote wanaendelea vizuri. Kisukari hao ndiyo wengi kabisa, sasa sijui kwako mpendwa lakini nionavyo muda si mrefu ukweli utajulikana kuhusu babu wa Loliondo. Lakini mpaka sasa imani ya watu ipo juu ya tiba ya babu.

Jamaa si katoa ushuhuda kwamba naye alidhani amepona kumbe siyo. Watu wote wakitoka loliondo wanasema wamepona lakini huko ni kupona psychologically virusi vinakuwa bado vinashambulia. Mbona hapa jamvini tupo kibao na kuna ndugu zetu wameenda huko na kurudi kwa nini tusitoe ushuhuda wa kisayansi yaani vyeti badala ya kusema tu anaendelea vizuri?
 
Mimi nazungumzia ushuhuda wa watu niliowaona, watatu ni ukimwi karibu wote wanaendelea vizuri. Kisukari hao ndiyo wengi kabisa, sasa sijui kwako mpendwa lakini nionavyo muda si mrefu ukweli utajulikana kuhusu babu wa Loliondo. Lakini mpaka sasa imani ya watu ipo juu ya tiba ya babu.


Ndiyoooo.. ukweli sasa hivi utajulikana! Watu wanakufa -- jamaa yangu mmoja amekufa kwa ukimwi baada ya kutoka kwa Babu. Kabla ya hapo alikuwa anaendelea vizuri na ARV zake.

Watu kadha wa kisukari nao wanalalamika hawaponi. Serikali inaogopa nini kusema ukweli? Isiendekerze mambo ya imani kwani tukishaingia huko tumeangamia woote. Ulimwengu mzima watatucheka. hata hivyo ma-babu wa namna hii wameshazuka wengi tu kwingineko duniani -- na hakuna chochote cha maana kilichopatikana na wananchi walizirudi tiba zao za mahospitalini.
 
Huu mimi ndiyo naita ujinga sasa. Usipone wewe ulaumu serikali eti inaficha kitu! Kitu gani? tuambie wewe sasa. Unataka kutuambia umati wote ule bila kujali dini zao, kabila,itikadi za kichama, uSimba na UYanga, wake kwa waume, wote wajinga mjanja wewe tu? Stop pointing fingers on the Gov kwa masuala yenu binafsi. Hawezi kupona kila mtu, wengine wamelaaniwa kwao, utapona vipi? Bora ukacheki na mizimu ya kwenu pia.
 
Mkuu ayo ni mambo ya imani. Kama huna imani na kama una ngoma basi kilichopo subiri siku itimie. Hamna imani alaf mnalalama lalama,itakula kwenu!

kuwa mstarabu na majibu yako mtu kisha sema hakuruka foleni isitoshe alikuwa na imani Mijitu mingine bana eti imekula kwako ndo nini?
 
Mi nadhani ifikie mahala ambapo Babu akamatwe kwa utapeli na mauaji (ya bila kukusudia). Surely, we cannot go on like this!! Serikali inashabikia vitu vya kipambaf kabisa -- what's wrong with ther JK government?
 
Nina wasi wasi sana na mtoa habari hii au anayesema anatoa ushuhuda unaposema wajitokeze wiki mbili zimepita jamaaa wa chama fulani cha wagonjwa wa ukimwi walijitokeza na kusema wamepata afadhali baada ya kupata kikombe tena mwenyekiti alisema yeye hata kulala ilikuwa tabu mpaka miguu yake ipigwe pigwe sana maana ilikuwa inasumbua na wakasema wako tayari kupimwa after three weekes na vyomob vya habari vijitokeze wao wako tayari. Sasa una po conclude loliondo hakuna kitu nakuwa na wasiwasi sana najua umefanya ivi kuwasupport kina maggid na wenzie na ulipowataja tu maggid na wenzie nimegundua kaka hii story umetunga usioombe kupata UKIMWI unajifanya muathirika utaupata kweli we fanya mchezo tu halafu unatumia jina hata siyo lako eti mollel nani alikuwambia usipotaja jina hatutakuamini? Kama kweli una HIV ni PM kesho nije nikuone physically siyo unatunga tunga tu vitu.:tape::tape::tape:
 
Kweli Wanzania tumewekwa pabaya!! Watu tunadanganyana mchana kweupeee bila aibu. Serikali inahamia Loliondo ati wanaenda kuangalia mazingira kumbe wanaenda kupata kikombe!! Watu wanakimbia kutoka mahospitalini kwenda kwa waganga wa kienyeji (Kwangu Babu ni sawa tu na waganga wengine wa kienyeji). Ukiona taifa linafikia hatua hii kwamba hata viongozi hawwaamini madaktari na hospitali ambazo ziko chini yao ujue kuna tatizo kubwa sana katika jamii husika. Tanaznia tumefika hapo, tujiombee.
 
Imani, imani, imani -- ndiyo umekuwa wimbo wenu mkubwa wa kuwatapeli na kusababisha vifo kwa Watanzania. Imani my foot!! Hakika JK kaifikisha nchi kwenye lowest level since independence!

Halafu eti mwaka huu tunasherehekea nusu karne ya uhuru! Uhuru gani wakati tumerudi katika karne ya 12!!!
 
Babu alikuambia ukinywa kikombe usiache ARV sasa ww mbona umeacha ghafla?

halafu imani hukuwa nayo?
 

Ndiyoooo.. ukweli sasa hivi utajulikana! Watu wanakufa -- jamaa yangu mmoja amekufa kwa ukimwi baada ya kutoka kwa Babu. Kabla ya hapo alikuwa anaendelea vizuri na ARV zake.

Watu kadha wa kisukari nao wanalalamika hawaponi. Serikali inaogopa nini kusema ukweli? Isiendekerze mambo ya imani kwani tukishaingia huko tumeangamia woote. Ulimwengu mzima watatucheka. hata hivyo ma-babu wa namna hii wameshazuka wengi tu kwingineko duniani -- na hakuna chochote cha maana kilichopatikana na wananchi walizirudi tiba zao za mahospitalini.

Nakubaliana nawe -- ukweli utajulikana sasa hivi -- kwani watu hawaponi kabisa -- wanadanganya tuu. Nadhani wanaona haya kusema ukweli baada ya kusota wiki kadha porini wasionekane wajinga. Ujinga hauondoki kwa unafiki!!!
 
Nauguliwa na mke wangu kisukari na sote tumekuwa tunatafakari kwenda huko -- pesa siyo tatizo kwani tunatumia hela nyingi sana kwa kununua vidonge. Kidonge kimoja cha Amaryl glimepride 2mg ni sh 1,700/- na anakula vinne kwa siku -- peke yake hapo ni sh 6,800. Bado Glucophage metformin na vile vya presha ambavyo lazima ameze pia. Kwa siku ni karibu sh 10,000/-

Lakini tumepeleleza sana kwa wenye kisukari tunaowafahamu waliokwenda kupata kikombe -- wawili wamesema hakuna chchote, hali zao zilirudi kama zamani na wakawahi kuendelea na vidonge vyao. Hivyo tumeamua kutokwenda na kuendelea kutumia vidonge na kufuata masharti ya milo. Tuna hakika ni utapeli na laghai kubwa sana inafanyika na inashangaza kwa nini serikali imeingia kichwa kichwa. Itapata tabu sana kujinasua katika laghai hiyo.
 

Afande akipata kikombe kwa Babu.

Jesus Christ is the only answer.

Source JESUS IS LORD


Askari kupata kikombe siyo ushuhuda wa kupona! Mimi nadhani serikali isiingie kwenye ushabiki wa kijinga ifanye experiment ya kitaalamu na inayoeleweka. Ichukuwe wagonjwa watano wa kisukari wanaofahamika kutokana na kumbukumbu za za hospitali (waki-liase na hospitali kadha na za binafsi pia) wawapeleke Loliondo kupata vikombe vyao. Baada ya hapo warudi na waanze kuratibiwa kwa vipimo kama kweli watakuwa wamepata unafuu.

Ajabu serikali haitaki kufanya kitu simpo kama hiki badala yake imeingia ushabiki wa ajabu kabisa eti na kugharamia mabilioni ya walipa kodi kwa ajili ya barabara kwa babu.
 
Nauguliwa na mke wangu kisukari na sote tumekuwa tunatafakari kwenda huko -- pesa siyo tatizo kwani tunatumia hela nyingi sana kwa kununua vidonge. Kidonge kimoja cha Amaryl glimepride 2mg ni sh 1,700/- na anakula vinne kwa siku -- peke yake hapo ni sh 6,800. Bado Glucophage metformin na vile vya presha ambavyo lazima ameze pia. Kwa siku ni karibu sh 10,000/-

Lakini tumepeleleza sana kwa wenye kisukari tunaowafahamu waliokwenda kupata kikombe -- wawili wamesema hakuna chchote, hali zao zilirudi kama zamani na wakawahi kuendelea na vidonge vyao. Hivyo tumeamua kutokwenda na kuendelea kutumia vidonge na kufuata masharti ya milo. Tuna hakika ni utapeli na laghai kubwa sana inafanyika na inashangaza kwa nini serikali imeingia kichwa kichwa. Itapata tabu sana kujinasua katika laghai hiyo.

Afadhali wewe umefunuliwa. Yaani kweli kabisa Watanzania tumefikishwa kwenye kona!!
 
Eti imani, Ndio nini imani? wewe watu wanakufa unasema hawakuwa na imani! Watanzania tunazidi kujidhalilisha leo karne ya 21 bado tunafikra za enzi ya mawe? Eti hujapona co's hukuwa na imani sasa mtu alitokatoka vipi mpaka kwenda Loliondo na adhabu ya safari,Nauli ghali foleni siku 13 alafu mijitu inaongelea imani. mambo ya Kibwetere msitulete hapa kutetea Ubaradhuli na Ushirikina, jana Rafiki yangu kipenzi alikuwa Muathirika wamemzika kwao.Dodoma alikuwa ana hali nzuri akaacha kutumia ARVs toka arudi Lolys kwa Babu yenu tar 21 Jan 2011 wiki iliopita alinipigia simu dada yake akanipa nionge nae alikuwa anatia huruma alikuwa anaongea kwa tabu sanaa moja ya kauli zake za mwisho kwangu aliniusia kuwa Watu wasighilibike wakaendelea na Uasherati kwa kujipa Matumaini eti kuna KIKOMBE au BAKULI Hakuna kitu kama hicho namsikitikia na ananiuma sana rafiki yangu Bora angeendelea na Dozi ya ARVs Pole sana Wanafamilia yake R.I.P JAROME
 
Back
Top Bottom