Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,179
- 85,337
Tumekusanyika wote, tumependeza kweli, ni kozi mbalimbali na tumetengwa vivyo hivyo!! Mimi nahitimu kozi ya Elimu ya Watu wazima (Bachelor of Education in Adult Education) ni furaha kweli. Ila kuna kitu kinaniumiza sana kila nikikumbuka shule niliyopangiwa.
Kweli hii si shule bali ni majengo tu, hayana madirisha mazuri, sakafu chafu, imetoboka toboka! Nashindwa kufundisha kutoka na vumbi lile, ubao wa kufundishia haueleweki, ofisini sina hata rula, inabidi nijinunulie kalamu! Lakini mbaya zaidi ni hawa wafuatao; wanafunzi wawili wenye ulemavu wa viungo, inabidi wakae chini pale mbele maana hawawezi kukaa kwenye madawati na pia baskeli zao hazipiti kwenye milango ya madarasa. La pili, wanafunzi wangu wanaonekana kukata tamaa ya maisha kabisa na kila ninavyojaribu kuwaelimisha hawaonekani kabisa kunielewa. Wanauliza maswali magumu kuliko uwezo wa kuyajibu, hawana maabara hata moja, kuna gunia moja na box ambalo tumehifadhia mifano ya test tube, spatula na n.k
Walimu wenzangu nao wanaonekana wamefika mwisho wa maisha yao, ni walevi wa kutupwa (si walaumu) na nguo zao zinaonyesha fadhaiko kubwa na kukata tamaa kwa hali ya juu, ni kilio kikubwa. Niko kwenye nyumba ya kupanga, naonekana kama ndio Mungu wao, mwenyewe nimepigika!
Siku moja nikaenda Halmashauri kufuatilia madai yangu, nilichokikuta ilikua ni pigo jingine, kauli za wahasibu wale zilinikatisha tamaa sana sana, ni kauli zilizojaa jeuri na kiburi, mbaya zaidi namuona kijana mmoja ambae tulimaliza mwaka mmoja kwa kozi tofauti (Accounts) ni mmoja wa wahasibu/cashier wa pale, yeye anapendeza jamani si haba hakuna ulinganisho wa mimi na yeye kwa namna yoyote ile. Naelekea kwenye ofisi za TSD huko nako nakuta kituko majibu ya hovyo sana, roho inauma sana.
Ninaporudi jioni nimechoka sana maana hata basi la kurudia kwangu nililikosa na hivyo kupanda Landrover, nimejaa vumbi sana, nimechoka na kesho natakiwa tena niwepo darasani nifundishe wanafunzi wangu!!! Usiku ule unakuwa usiku wa maumivu makali sana kwangu, nikijiuliza kuwa kwanini nilifanya chaguo baya? Maana nilifaulu kwa kiwango cha Division One point Seven kwa form six.
Asubuhi naamua kuongea na wanafunzi wangu badala ya kufundisha tu kila siku, tunabadilishana mawazo, maana si mwalimu wala si wanafunzi wanaoneka wana ari ya kusoma tena!!!!! Nawauliza, ni wapi alipo Asha Amiri? wanacheka na mmoja anasimama na kuongea kwa kejeli, "ameshaolewa, yaani mwalimu huna habari?"
Ni jioni sasa, nipo nje pale nyumbani, wanakijiji wanaendelea na shughuli zao, huyu anachota maji hawa wanarudi machungani, nina kiredio kidogo nasikiliza nisichokielewa! Maana hakika mawazo yangu yako mbali sana, ile degree haina maana tena, sina wa kumfundisha maarifa yale! Naonekana kituko pale kijijini kwa kutaka kuwafundisha watoto wale!!! Ghafla, napata ujasiri wa ajabu, yes ujasiri wa ajabu sana. NIMEAMUA KUACHA KAZI. Kesho ni Ijumaa kwa hio nitaomba niende mjini mara moja lakini hapo ndipo mwisho wa kukaa hapa.
Narudi mjini na kuamua kuanza maisha ya tofauti sana na kujaribu kuisahau ndoto ile kwamba ningekuwa Mwalimu mzuri, nimeachana na vituko vya kukatwa pesa ya MWENGE kwa ajili ya kufungua miradi ya watu binafsi, nimeachana na maumivu yale ya kudharauliwa na watumishi wenzangu walioko halmashauri, sijawahi pia kukaa nikafahamu mshahara wangu ni shilingi ngapi hasa, maana kila siku unabadilika kwenye payslip.
Walimu wana haki sawa na watumishi wengine, tuwapende, tuwajali na tuwatunze!!!
Mwalimu Elli
Kweli hii si shule bali ni majengo tu, hayana madirisha mazuri, sakafu chafu, imetoboka toboka! Nashindwa kufundisha kutoka na vumbi lile, ubao wa kufundishia haueleweki, ofisini sina hata rula, inabidi nijinunulie kalamu! Lakini mbaya zaidi ni hawa wafuatao; wanafunzi wawili wenye ulemavu wa viungo, inabidi wakae chini pale mbele maana hawawezi kukaa kwenye madawati na pia baskeli zao hazipiti kwenye milango ya madarasa. La pili, wanafunzi wangu wanaonekana kukata tamaa ya maisha kabisa na kila ninavyojaribu kuwaelimisha hawaonekani kabisa kunielewa. Wanauliza maswali magumu kuliko uwezo wa kuyajibu, hawana maabara hata moja, kuna gunia moja na box ambalo tumehifadhia mifano ya test tube, spatula na n.k
Walimu wenzangu nao wanaonekana wamefika mwisho wa maisha yao, ni walevi wa kutupwa (si walaumu) na nguo zao zinaonyesha fadhaiko kubwa na kukata tamaa kwa hali ya juu, ni kilio kikubwa. Niko kwenye nyumba ya kupanga, naonekana kama ndio Mungu wao, mwenyewe nimepigika!
Siku moja nikaenda Halmashauri kufuatilia madai yangu, nilichokikuta ilikua ni pigo jingine, kauli za wahasibu wale zilinikatisha tamaa sana sana, ni kauli zilizojaa jeuri na kiburi, mbaya zaidi namuona kijana mmoja ambae tulimaliza mwaka mmoja kwa kozi tofauti (Accounts) ni mmoja wa wahasibu/cashier wa pale, yeye anapendeza jamani si haba hakuna ulinganisho wa mimi na yeye kwa namna yoyote ile. Naelekea kwenye ofisi za TSD huko nako nakuta kituko majibu ya hovyo sana, roho inauma sana.
Ninaporudi jioni nimechoka sana maana hata basi la kurudia kwangu nililikosa na hivyo kupanda Landrover, nimejaa vumbi sana, nimechoka na kesho natakiwa tena niwepo darasani nifundishe wanafunzi wangu!!! Usiku ule unakuwa usiku wa maumivu makali sana kwangu, nikijiuliza kuwa kwanini nilifanya chaguo baya? Maana nilifaulu kwa kiwango cha Division One point Seven kwa form six.
Asubuhi naamua kuongea na wanafunzi wangu badala ya kufundisha tu kila siku, tunabadilishana mawazo, maana si mwalimu wala si wanafunzi wanaoneka wana ari ya kusoma tena!!!!! Nawauliza, ni wapi alipo Asha Amiri? wanacheka na mmoja anasimama na kuongea kwa kejeli, "ameshaolewa, yaani mwalimu huna habari?"
Ni jioni sasa, nipo nje pale nyumbani, wanakijiji wanaendelea na shughuli zao, huyu anachota maji hawa wanarudi machungani, nina kiredio kidogo nasikiliza nisichokielewa! Maana hakika mawazo yangu yako mbali sana, ile degree haina maana tena, sina wa kumfundisha maarifa yale! Naonekana kituko pale kijijini kwa kutaka kuwafundisha watoto wale!!! Ghafla, napata ujasiri wa ajabu, yes ujasiri wa ajabu sana. NIMEAMUA KUACHA KAZI. Kesho ni Ijumaa kwa hio nitaomba niende mjini mara moja lakini hapo ndipo mwisho wa kukaa hapa.
Narudi mjini na kuamua kuanza maisha ya tofauti sana na kujaribu kuisahau ndoto ile kwamba ningekuwa Mwalimu mzuri, nimeachana na vituko vya kukatwa pesa ya MWENGE kwa ajili ya kufungua miradi ya watu binafsi, nimeachana na maumivu yale ya kudharauliwa na watumishi wenzangu walioko halmashauri, sijawahi pia kukaa nikafahamu mshahara wangu ni shilingi ngapi hasa, maana kila siku unabadilika kwenye payslip.
Walimu wana haki sawa na watumishi wengine, tuwapende, tuwajali na tuwatunze!!!
Mwalimu Elli