ushirikiano au umoja wa Chadema na NCCR unakuwaje tishio kwa Waislam?u

KALABASH

JF-Expert Member
Jan 26, 2011
493
205
Jana usiku katika kipindi cha majadiliano Radio Kheri Sheikh Mohamed Issa aliwatahadharisha sana Waislamu kuwa waangalifu na makini na huu umoja na ushirikiano uliojitokeza hivi karibuni kati ya Chadema na Nccr na athari zake kwa Waislamu katika swala la uongozi wa Tanzinia kwa siku zijazo. Nilisubiri afafanue ni kwa vipi umoja kati ya vyama viwili vya upinzani uwe tishio kwa Waislamu badala ya kuwa tishio kwa chama tawala sikusikia ufafanuzi wowote. Wana JF au washirika wa Sheikh Mohamed Issa mnaweza kunisaidia kupata tafsiri ya kauli hii?
 
Aisee,

Redio Kheri ndio ya wapi hiyo na inamilikiwa na nani?...

Taifa la Wajinga hili...tunaishi kwa hisia hisia, na kuchunguza nani kafanya nini, na anataka nini!..huh!
Kuna ubaya gani kama CUF kashirikiana na ccm, na Nccr na cdm?...Mambo ya udini yapo hapo?
 
hivi redio kheri au imani kuna mtu wenye shahada,stashada au hata cheti cha uandishi wa habari?na ili uwe shee unabidi uwe na elimu gani?maana reasoning inabidi iwepo.
 
This is too much! Jamani tushirikishe ubongo kidogo tunapotoa matamko yaani hata hayo makubaliano hujayaona tayari kwa hisia tu unaconclude? Amekusanya lini maoni ya waislamu wote ili kujua wanalichukuliaje suala hilo? Amejuaje kama hautainufaisha jamii yote ya kitanzania bila kujali dini zetu? Matamko haya yanatakiwa kukanushwa la sivyo yakiachwa kuna uwezekano watu wakayachukulia kama ni ya kweli. Tuangalie uhalisia jamani tusiendeshwe na hisia tu kama vile tuna akili bila utashi/ufahamu wa kuchambua mambo.
 
Nilichoka siku moja niliisikiliza hii redio kidogo nizirai aisee
Shekh mmoja alikuwa anasema eti anashangaa muislamu mzima unashabikia ligi za soka za ulaya wakati asilimia 95 ya wachezaji sio waislam ni wakristo
Akaenda mbali zaidi eti utakuta Saudi Arabia inacheza na Brazil unakuta muislam anashabikia Brazili wakati Brazili yote ni wakristo, aka hoji utamshabikia vipi kafiri uache kushabikia muislamu mwenzio kwa mujibu wa maamrisho ya Allah

Hapo ndipo niliamini kweli elimu dunia ni muhimu isee, kuna matatizo makubwa kuwa na elimu ya kukariri koran na hadith tu bila elimu dunia
 
Hawana lolote hawa viongozi wa dini (siyo wote) ila wengi wao wanatumiwa na vikundi ( nchi fulani) fulani vyenye/zenye nia mbaya haswa na hili bara letu lilivyo na mali ghafi nyingi basi kazii kweli kweli!! Kila mmoja kwa nafasi yake duniani hapa anajaribu kum-overpower mwenzake ili aendelee kuishi. Cha ajabu viongozi wetu hawasikii wala kutaka kusikiliza au kujifunza.
 
tukiendelea kushabikia na kuruhusu itakidi za namna hii zitutawale tutaishia pabaya,,mungu atusaidie busara zituongeze
 
mim nadhan hakuna haja ya kupoteza muda na huyo sheikh ambaye sijui amesoma mpaka wapi.naiheshimu elimu na kuwapenda hata wasiosoma lakini siwezi kuvumilia watu kama hao(wasio soma) wenye akili ndogo zilizokuzwa na kustawishwa katika malalamiko na kulialia kiujaribu kuvuruga amani na demokrasia yetu changa. kama ana akili anaweza atueleze madhara ya uhusiono na ndoa kamilim kati ya cuf na ccm.uislamu na waislamu wanadhalilishwa na watu wa aina hii.
 
mim nadhan hakuna haja ya kupoteza muda na huyo sheikh ambaye sijui amesoma mpaka wapi.naiheshimu elimu na kuwapenda hata wasiosoma lakini siwezi kuvumilia watu kama hao(wasio soma) wenye akili ndogo zilizokuzwa na kustawishwa katika malalamiko na kulialia kiujaribu kuvuruga amani na demokrasia yetu changa. kama ana akili anaweza atueleze madhara ya uhusiono na ndoa kamilim kati ya cuf na ccm.uislamu na waislamu wanadhalilishwa na watu wa aina hii.
Umenena vyema lakini tatizo linakuja kama hatua za makusudi za kukomesha hali hii hazitachukuliwa na serikali yetu basi tutegemee hali hii itaendelea na kusababisha machafuko. Kwanini mtu anavunja Katiba anaachwa? Kwanini mtu anapotosha watu kwa makusudi haonywi? Kunatatizo mahali hebu tujiangalie upya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom