Wasomi/wataalamu wa mambo ya siasa wanasema inawezekana Arumeru wamefuata mkumbo wa kutaka mabadiliko. Hii ni kutokana na CCM na ishu ya kujivua gamba bila mabadiliko yeyote. Watu wamechoshwa na mambo yale yale tangu karne zile.
Hao wasomi na wataalam ni wa MAGAMBA,hivi kweli Dr.Benson wa udsm naye unaweza kusema ni msomi mwenye tija?na ina maana wamekosekana wasomi wengine wenye vision mpaka kila mara kukimbilia kupata maoni kwa hili KUWADI la magamba?nahurumia vijana wetu wanao fundishwa pale udsm na jitu hili.Wanavyo sema wananchi wa Arumeru wamefuata mkumbo kwani wao hawana maono na kujua nani mwenye nia halisi ya kuwasaidia? acheni utafiti wenu usiokuwa na kichwa wala miguu.Tunaikumbuka sana REDET kwa kupindisha ukweli.
Tafakari....
Huku watu wameelimika na si kama huko.....
Arusha wanatambua hako zao na si rahisi kuendelea kuumuia wakati wanajua ni wakati wa ukombozi....
Hakuna cha mkumbo kwa kuwa mambo ya sisiemu ni sifuri tu
Ni moto wa mabadilimo awtu wala wasijidanganye eti mkumbo. Na bado kazi inaendelea. Tunasubiri Segerea ambako kila mwenye akili timamu anaona nini hatma yake. Magamba sasa watashika pua baada ya kichwa kule Arumeru
Hawajatutendea haki Wanaarumeru hao wanaojiita wasomi/wataalamu. Ninaweza kusema wametutukana,na wanaweza wakawa wametoka mikoa ile isiyojitambua na isiyosoma alama za nyakati au wametumwa na magamba.
sidhani kama ni hivyo. neno ulilotumia ni kama nadharia tu. ukitaka kujua kama ni mkumbo fuatilia historia ya Meru otherwise you may have wrong assumption. hakuna mkumbo ni upeo wa demokrasia na weledi wa watu wa Arumeru.
Wasomi/wataalamu wa mambo ya siasa wanasema inawezekana Arumeru wamefuata mkumbo wa kutaka mabadiliko. Hii ni kutokana na CCM na ishu ya kujivua gamba bila mabadiliko yeyote. Watu wamechoshwa na mambo yale yale tangu karne zile.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.