GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,278
- 6,672
Habari zenu wana Jamvi, yuko dada mmoja ambaye ni jirani yangu kaniomba ushauri ambao binafsi nimeshindwa kumshauri. Hivyo naomba mawazo yenu. Ni kitu ambacho kidogo kimenishangaza. ni dada mwenye watoto wawili kwa maelezo yake ni kuwa mumewe alimpa karipio kali kuwa hataki mtoto tena, anasema kwa bahati mbaya siku za hivi karibuni alizembea kutumia vidonge vya uzazi, sasa imeshaingia.
Anachonieleza ni kuwa kwa jinsi anavyomjua mumewe anaogopa kumwambia kwani anaweza kujikuta akipata talaka kwa kosa hilo tu! Pia swala la kutoa anaogopa kwani anahisi iwapo yatatokea matatizo atazusha tatizo kubwa zaidi! Je afanye nini kujinasua na tatizo hilo?
Anachonieleza ni kuwa kwa jinsi anavyomjua mumewe anaogopa kumwambia kwani anaweza kujikuta akipata talaka kwa kosa hilo tu! Pia swala la kutoa anaogopa kwani anahisi iwapo yatatokea matatizo atazusha tatizo kubwa zaidi! Je afanye nini kujinasua na tatizo hilo?