Ushauri wangu kwa cdm.

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Mimi ni mwanachama wa cdm na kila nilipo naihubiri cdm,hata kwangu hukutani na kitu chunye rangi ya njano au kijani zaidi ya mimea iliyowekwa na mwenyezi Mungu. Naomba kila siku tuendelee kukubalika kwa wananchi ili waje waikabidhi nchi 2015. Tumesikia vuguvugu la vijijini namna viongozi wengi wa cdm wanavyochaguliwa kila nafasi inapojitokeza. Hii ni ishara ya mwangaza kwa wakazi wa mbuga hii isiyo na mwenyewe na bado kuna vijiji vingi vitachukuliwa kabla ya 2015. Ombi langu, naomba viongozi wanaoaminiwa na kupewa uongozi na wananchi wawe wazalendo kwa kufanya mazuri kwa manufaa ya wote. Wapewe semina kila walipo ili wananchi waone utofauti wa nyinyiemu ambao wamekuwa wakifanya kazi ya kuvuna rasilimali zetu kwa manufaa ya matumbo yao na cdm ambao wanakuja kukomboa wananchi. Wasiwe na visirani vya uchu wa madaraka na kuanza kutukanana hadharani. Najua kuna watu mko karibu nao mnaweza kukubaliana na ushauri huu,mi mwenyewe nikiwa sehemu ya kazi nahakikisha nahubiri ubovu wa serikali ya jk na wahuni wenzie kulingana na mapungufu yanayojitokeza sehemu ya kazi ambayo yalitakiwa yakamilike kwa uwezo wa rasilimali zetu. Ni ushauri tu, tukosoane na kukubaliana. Mungu ibariki tz, Mungu ibariki cdm! Mungu walaani wale wote wanaokula bila mali za umma wakisahau kuwatumikia wananchi.
 
Back
Top Bottom