Ni kweli hakuna haja ya kuficha.Unakuta mtangazaji anaelezea hisia zake au matusi hadharani bila aibu.Kwa mfano kipindi cha Kibonde nawenzie wakati mwingine wanaongea mambo ya chumbani bila aibu au wanajadili siasa na kuwataja wanasiasa wa vyama bila aibu hii au soni.Saa nyingine wanatekenyana na kutongozana hadharani ! sasa hiyo taasisi au mali zao binafsi hao watangazaji hawana heshima hata kidogo ! jee wakurugenzi mnapenda matusi hayo ? mbona mko kimya ? hawa watangazaji wanawapaka choo sana kwa taarifa yenu ! sisi wasikilizaji hatuhitaji matusi yao au kutongozana kwao au kusikia habari za mabibi au mabwana zao ! tunataka habari zatakazotusisimua na kutufurahisha.