USHAURI WA BURE:Swala Kuhusu Ufugaji wa Mifugo aina yoyote, Uliza hapa utapata Jibu bure

Wapo kuku kama 50, nawafunga ndani lakini wanazunguka ndani ya fensi.yes nilipa chanjo ya new castle miez kama miwili na nusu iliyopita mkuu.
Nawalisha mchanganyiko wa pumba za mahindi, mahindi, mashudu, dagaa, mifupa na chokaa pia uwa nawapatia na majani atleast mara 3 kwa wiki.
Asante mkuu

Well, kwa dalili ulizozitaja, itakuwa ni Newcastle disease, Huwa inaweza kutokea hata kama umechanja, kutokana na vaccine failure, na ndo maana walioathirika ni wachache kwa maana wanakinga tayari, otherwise maumivu yangekuwa ni makubwa. Ikitokea incidence nyingine fanya yafuatayo:

1. Mtenge kuku mgonjwa kutoka kwa wenzake

2. Wape kuku wote antibiotic, preferably OTC 20% kwa muda wa siku tano, hii ni pamoja na kuku mgonjwa

Zaidi ni kwamba usisahau kuwachanja tena dhidi ya Mdondo 2wks from now!!.

Karibu sana Kiongozi!
 
mbona mtaalam kaingia mitini?yanaonekana maswali tuu,majibu hayapo!

Hapana mkuu, sijaingia mitini, mimi nipo ila kuna majukumu mengine muhimu kama lilivyokuwa muhimu suala hili hapa JF. Hivyo kwa kuzingatia umuhimu huu wa sehemu hizi zote, nimetenga Muda wa kuja kurespond kwa maswali hapa JF, na Muda wa ku attend hizo other life duties. So usiwe na wasi, wewe visit JF regularly utakutana na majibu ya maswali yote yaliyo ulizwa hapa.

Pamoja sana!!
 
Well, kwa dalili ulizozitaja, itakuwa ni Newcastle disease, Huwa inaweza kutokea hata kama umechanja, kutokana na vaccine failure, na ndo maana walioathirika ni wachache kwa maana wanakinga tayari, otherwise maumivu yangekuwa ni makubwa. Ikitokea incidence nyingine fanya yafuatayo:

1. Mtenge kuku mgonjwa kutoka kwa wenzake

2. Wape kuku wote antibiotic, preferably OTC 20% kwa muda wa siku tano, hii ni pamoja na kuku mgonjwa

Zaidi ni kwamba usisahau kuwachanja tena dhidi ya Mdondo 2wks from now!!.

Karibu sana Kiongozi!
Nashukuru sana mkuu,
Hili ni swali tofauti kidogo kuna chanjo nyingine nimewahi kusoma sehemu inaitwa malnex kama sijakosea uwa wanachanjwa vifaranga wa siku moja kwa lengo la kuwafanya wawe imara wanapofika wakati wa kutaga.nilikua naomba kufahamu kama kuna madhara endapo vifaranga hawatapewa hyo chango mana mara nyingi imekuwa haizungumziwi sana.nashukuru mkuu.
 
Mimi nataka kufuga mbuzi je nitegemee changamoto zipi?

1. Ukizingatia kuwa Mbuzi wanakula majani, changamoto kubwa ni uatikanaji wa majani, lakini hili linategemea sana wewe unafugia wapi. Kama ni Kwenye vijiji au periurban areas, this is not a big problem

2. Kwa upande wa magonjwa, tatizo kubwa la mbuzi ni Minyoo, hii itamfanya mbuzi ashindwe kukua vizuri na kuwa na afya njema. Hivyo ni vizuri kujiandaa na utaratibu mzuri wa kuwapa mbuzi wako dawa za minyoo regularly. Check with your Vet.

3. Tatizo lingine kwa upande wa magonjwa ni Kuharisha ( Diarrhoea), Hii, kuna bacterial, parasitic na viral causes, tarajia hili here and there. Be close with your Vet. Huwa linadhibitika kirahisi tu

4.Kwa upande wa magonjwa pia tarajia Orf , Huu ni ugonjwa wa kutoka vidonda, midomoni, puani na maeneo mengine some times, ni viral disease, your Vet atakushauri tatizo likitokea, huwa linatokea kama outbreak. Ukiona mbuzi mmoja kaota hivi vidonda, Mtenge na wenzake haraka sana, na wapatie antibiotic mbuzi wote zizini. Hata wale wasiokuwa na dalili yoyote.

. Changamoto nyingine ni uwizi, (Theft). Hili ni tatizo sana maeneo ya mijini, japo vijijini pia lipo hapa na pale. Hivyo ni vyema ukahakikisha unafuga miofugo yako mahali ambapo pana usalama, ikiwezekana fuga na mbwa mazingira hayo hayo, jaribu pia kupiaga mahesabu, kama business inaweza kusupport kumwajiri mlinzi, it will much better, has maeneo ya mjini.
 
Nashukuru sana mkuu,
Hili ni swali tofauti kidogo kuna chanjo nyingine nimewahi kusoma sehemu inaitwa malnex kama sijakosea uwa wanachanjwa vifaranga wa siku moja kwa lengo la kuwafanya wawe imara wanapofika wakati wa kutaga.nilikua naomba kufahamu kama kuna madhara endapo vifaranga hawatapewa hyo chango mana mara nyingi imekuwa haizungumziwi sana.nashukuru mkuu.

Bila shaka ni Marek's disese. Hili ni tatizo zaidi kwa kuku wa kisasa, na huwa wanachanjwa siku ya kwanza kabisa kwenye hatchery. Kwa kuku wa kienyeji it is more or less not a problem. Hili lisikupe hofu!!

Wish u a good luck. Ufugaji can change your life altogether kama utafuga kwa kuwashirikisha wataalamu. Kuwa karibu sana na mtaalamu yeyote aliye karibu nawe!
 
Bila shaka ni Marek's disese. Hili ni tatizo zaidi kwa kuku wa kisasa, na huwa wanachanjwa siku ya kwanza kabisa kwenye hatchery. Kwa kuku wa kienyeji it is more or less not a problem. Hili lisikupe hofu!!

Wish u a good luck. Ufugaji can change your life altogether kama utafuga kwa kuwashirikisha wataalamu. Kuwa karibu sana na mtaalamu yeyote aliye karibu nawe!

Asante sana mkuu umekuwa msaada mkubwa.uendelee na moyo huohuo
 
Saluti mtaalam! Ndo naanza kufuga kuku 10. Ila nataka niwe na kuku kama 5000 je ni namna gani ya kutengeneza mabanda bora? Kama kuku 100 banda lao liwe na ukubwa gani? Eneo langu la kazi ni heka 3 je linatosha kutimiza hiyo ndoto ya kuku 5000? Aksante
 
Asante sana Analyst nashukuru sana kwa kweli hawa hawakuwa na kinyesi chenye damu ila majimaji na kweli maranda ilibidi nibadili asubuhi na jioni ndio kilichonisaidia nikuwa na 200 walikufa kama 18 wakitibiwa ila sasa wamepona na wana afya nzuri, ila nitarudia dose mara nionapo dalili hizo. Sikuwahi kuwa na kuku wenye huu ugonjwa ila naona imetokea kwa kuwa nina hybrid wakubwa wanaotaga nadhani wana immunity tayari na vile sikuweka footbath wala boots za kuingilia (laxity) ikala kwangu lol. Basi ninajitahidi usafi sasa
 
Mkuu naomba fomula nzuri ya chakula cha kuku wa kienyeji,hapa nilipo kuna mahindi,mashudu ya alizeti,mbaazi,mtama na mpunga..dagaa wapo lakini ni ghali na wanakuja kwa uchache..naomba unishauri ratio nzuri ya kuwachanganyia nina lengo niwe nawauza kila baada ya mmuda mfupi kama miezi minne mpaka mitano.
 
Mtaalam analysti unauzungumziaje ufugaji wa Bata Mzinga; changamoto zake, mazingira ya kuwafugia yaweje, magonjwa yanayowashambulia, vyakula ambavyo ni preferably kwao, na nifanyaje ili watage mayai mengi kwa wakati mmoja mbali na lishe ninayowapa.
 
Last edited by a moderator:
Modes hamtutendei haki nilitegemea huu uzi utakuwa umeshawekwa kwenye sticky tafadhali utundikeni hapo juu

Analyst ubarikiwe sana
 
Hellow wana JF,

Nimetambua ukweli kuwa JF ni jukwaa linalowafikia watanzania waliowengi kirahisi hasa baada ya maendeleo makubwa ktk Sayansi na Teknolojia ktk nchi yetu.

Pia nimetambua kuwa JF inamchanganyiko wa watu wenye Taaluma mbalimbali ambazo tukizitumia vyema, basi JF inaweza kuwa ni jukwaa litakalokuwa na mchango mkubwa ktk kuyafikia malengo ya maendeleo ya Milenia (MDGs)

Mimi nikiwa kama Mtaalamu wa Mifugo. Nimeamua kuwasaidia watanzania wenzangu kwa kutumia utaalamu nilionao kupitia JF (kwa kushirikiana na wataalamu wa mifugo wengine waliomo humu JF). Natoa wito, kwa mtu yeyote aliye na swali kuhusiana na aspect yoyote ile ya Ufugaji, aulize hapa, ushauri utatolewa bure.Ushauri huu nitautoa mimi mwenyewe au Mtaalamu mwengine yeyote aliyemu humu kupitia uzi huu. Wafugaji wazoefu pia tunawa encourage kushare uzoefu wao ktk matatizo yatakayokuwa raised na wafugaji wengine.

Ninaamini Uzi huu utakuwa na manufaa kwa wafugaji na watu wengine ambao wangependa kufuga ili kujiongezea kipato, ukizingatia hali ya maisha inaendelea kuwa ngumu kadiri siku zinavyosonga mbele.

Karibuni!!

Nimeipenda thread yako, BIG UP
 
Mtaalam nina mpango wa kuanza kufuga mbuzi!
Hivi mbuzi wa kisasa au wa kienyeji huchukua muda gani mpaka kuzaa na huweza kuzaa vitoto vingapi kwa ujumla?.
Pia naomba unipe ushauri namna ya kuwatunza ili waweze kuwa na afya bora pamoja na kuzaa kwa wingi!
 
Hellow wana JF,

Nimetambua ukweli kuwa JF ni jukwaa linalowafikia watanzania waliowengi kirahisi hasa baada ya maendeleo makubwa ktk Sayansi na Teknolojia ktk nchi yetu.

Pia nimetambua kuwa JF inamchanganyiko wa watu wenye Taaluma mbalimbali ambazo tukizitumia vyema, basi JF inaweza kuwa ni jukwaa litakalokuwa na mchango mkubwa ktk kuyafikia malengo ya maendeleo ya Milenia (MDGs)

Mimi nikiwa kama Mtaalamu wa Mifugo. Nimeamua kuwasaidia watanzania wenzangu kwa kutumia utaalamu nilionao kupitia JF (kwa kushirikiana na wataalamu wa mifugo wengine waliomo humu JF). Natoa wito, kwa mtu yeyote aliye na swali kuhusiana na aspect yoyote ile ya Ufugaji, aulize hapa, ushauri utatolewa bure.Ushauri huu nitautoa mimi mwenyewe au Mtaalamu mwengine yeyote aliyemu humu kupitia uzi huu. Wafugaji wazoefu pia tunawa encourage kushare uzoefu wao ktk matatizo yatakayokuwa raised na wafugaji wengine.

Ninaamini Uzi huu utakuwa na manufaa kwa wafugaji na watu wengine ambao wangependa kufuga ili kujiongezea kipato, ukizingatia hali ya maisha inaendelea kuwa ngumu kadiri siku zinavyosonga mbele.

Karibuni!!

Mimi kuku wangu hutoka manundu mengi kichwan tatizo nini? Na tiba yake
 
Nataka kufuga Nyuki ktk Shamba langu,je naweza pata muongozo,au Link yeyote jinsi ya kufuga Nyuki Kisasa??
 
Asante sana mtaalam. Kwanza noomba uwashilikishe wataalam wengine wa mifugo unaowafahamu ili nao washiliki katika mpango hu wa kutusaidia wafugaji. Pili naomba ushauri wa wataalamu kwamba, nilikuwa na vifaranga wa kuku wa asili 16 walipo fikia wiki 2 niliwatenga na mama zao kwa kuwaweka kwenye box nikafunga taa(bulb 60W) chakula nilichotumia ni pumba ya mahindi peke yake. Baada ya siku 4 walikuwa wamedhofika sana ikabidi niwarudishe kwa mama zao baada ya hapo walikufa vifaranga 7 na 9 bado wapo ingawa bado wamedhofu na manyoya yametoka toka. Vet officer alinishauri nitumie chakula kiitwacho "stater",dukani nilikosha hicho chakula nikapewa mbadala nitengeneze mchanganyiko wa: Pumba 20kg,chokaa 1kg,mifupa 0.5kg,mashudu 2kg,premix 0.25kg,dagaa 2kg na chumvi vijiko 6 vya chakula. Natumia mchanganyiko huo kwa vifaranga 12 wa wiki 2 nimewatenga na mama zao siku ya 3 sasa. Naomba ushauri zaidi kutoka kwa wataalam.
 
Ahsante sana Analysti kwa uzi huu. Mimi nataka kuanza kufuga nguruwe, nina eneo la heka moja Dsm, nitegemee changamoto zipi? vipi masoko yake? Vipi hali ya hewa dsm ni favourable kwa mfugo huu? Nataka nianze na kumi, ila baada ya mwaka 1 niwe na nguruwe walau 100.
 
Mkuu tunashukuru sana kwa msaada huu wa maelezoyakinifu. Mimi nataka fuga nyuki ila sijua a wala b naomba maelekezo ya yaawali .
 
Back
Top Bottom