Ushauri wa bure kwa Dr Mwakyembe, achana kabisa na katiba mpya

sangu mnene

Member
Sep 5, 2012
92
35
Nimelazimika kuwaza tena suala la katiba pendekezwa baada ya Warioba kudai ataongea mchakato ukianza source Mwanainchi-27/12/2015. Sijui anachowaza Dr Mwakyembe, kama anataka kuandika katiba mpya kwa kuanzia pale ilipoishia kamati ya jaji Warioba ni vema na ni haki,aendelee kwa amani kabisa.Lakini kama anataka aendelee na katiba pendekezwa ya CCM,namshauri aachane nayo kabisa,ni bomu litakalowagawa watanzania.

Akumbuke kuwa katiba pendekezwa;

  1. Ilipingwa vikali na uongozi wa dini ya kiislamu, jambo hili liliwaunganisha waislamu wote
  2. Ilipingwa vikali na viongozi wa dini ya kikristo,jambo hili liliwaunganisha wakristo wote
  3. Katiba pendekezwa inapingwa na takriban wasomi wote
  4. Wafanyakazi waliipinga katiba pendekezwa waziwazi bila woga, hasa walimu
  5. Vyama vya upinzani karibu vyote viliikataa katiba pendekezwa,hata vile vilivyounga mkono baadaye viligeuka
  6. Wanafunzi wa vyuo na sekondari waliunga mkono rasimu ya Warioba
  7. Kukataliwa kwa rasimu ya Warioba kumepelekea CCM kuchukiwa sana Zanzibar
  8. CCM ilichukiwa sana bara, imani kwa CCM ililejea pale Polepole alipotangaza kuwa amehakikishiwa na Magufuli kwamba akiingia madarakani atairudisha rasimu ya Warioba
  9. NGO ziliipinga katiba pendekezwa waziwazi bila woga wala mawaa
  10. Waandishi wa habari waliweka tofauti zao kando na kuitetea rasimu ya Warioba kwa nguvu zote n.k

Nimkumbushe tu Dr Mwakyembe, watanzania hawachelewi kubadilika, Vita alivyovianzisha Dr Magufuli vinahitaji uungwaji mkono wa wananchi wote.Leo kila mtu anampenda rais. Lakini, kazi yote aliyofanya rais Dr Magufuli itaonekana si kitu, kama mchakato wa katiba iliyopitishwa kitapeli utaanza tena.Ukitaka umoja wa taifa hili uendelee kuwepo,na watu waendelee kuiunga mkono CCM basi rudisha rasimu ya Warioba,vinginevyo nakushauri achana kabisa na kufufua mchakato wa katiba.Kujaribu kuitetea katiba pendekezwa ni sawa na kuchezea moto karibu na petroli.ACHA,ACHA KABISA DR MWAKYEMBE KUTETEA KATIBA PENDEKEZWA,ACHA KAMA ULIVYOACHA KUNYONYA, hilo ni bomu kwa utawala mujaarabu wa Dr Magufuli,nakusihi achana na katiba pendekezwa rudi kwenye rasimu ya Warioba.Maneno yangu haya ni hakika,kweli na thabiti, ni suala la muda tu,akipuuzia matokeo tutayaona. Alamski!
 
Ni ushauri mzuri na ana masikio atasikia na kulifanyia kazi.
 
Kama mlichagua CCM irudi madarakani mnatarajia wapitishe katiba gani?

Tuache unafiki.Ukipenda boga penda na ua lake.

Ni wakati wa kuvuna tulichopanda.

CC: WARIOBA,Polepole.
 
Last edited by a moderator:
Kama mlichagua CCM irudi madarakani mnatarajia wapitishe katiba gani?

Tuache unafiki.Ukipenda boga penda na ua lake.

Ni wakati wa kuvuna tulichopanda.

CC: WARIOBA,Polepole.
 
Last edited by a moderator:
Subiri wakishakuharibikiwa na magufuli kuanza kupuuzwa na wanainchi ndipo watakapo kumbuka ushauri wako.
 
mwakyembe hana muda na mambo ya katiba, anawaza kupiga madili ya wizi tu kama alivyoiba makontena bandarini na kuagiza mabehewa feki ya tren
 
Naomba nianze kwa kuomba msamaha kwa atakayekwazika na haya nitakayosema. Mtu mmoja toka Mbeya aliniambia kuwa kuna aina mbili ya wanyakyusa,wale wa Tukuyu na wa Kyela. Wanyakyusa wa Kyela hujiamini,wana asili ya kiburi na wana misimamo isiyoyumba. Ni vigumu mno kumbadilisha msimamo mtu wa Kyela.Inasadikiwa kuwa lazima nguvu ya ziada itumike, ama kwa maombi au kwa nguvu za mizimu.

Dr Mwakyembe anatokea Kyela, sijui msimamo wake wa moyoni ukoje. Kama anaamini kwa dhati kuwa katiba pendekezwa ndiyo inayofaa na si rasimu ya Warioba, basi tumekwisha.Mtu wa Kyela habadiliki, hata aonywe vipi, ataishia kuvunjika shingo.Naomba watanzania, tuombe kila mtu kwa dini yake, ili moyo wa Dr Mwakyembe ulainike.La sivyo atang'ang'ania katiba, na kama rais atakataa, yupo tayari kujiudhuru,sababu ni mnyakyusa wa Kyela.Mungu tusaidie, tuondokane kabisa na jinamizi hili baya kabisa la katiba feki ya ccm
 
Nimelazimika kuwaza tena suala la katiba pendekezwa baada ya Warioba kudai ataongea mchakato ukianza source Mwanainchi-27/12/2015. Sijui anachowaza Dr Mwakyembe, kama anataka kuandika katiba mpya kwa kuanzia pale ilipoishia kamati ya jaji Warioba ni vema na ni haki,aendelee kwa amani kabisa.Lakini kama anataka aendelee na katiba pendekezwa ya CCM,namshauri aachane nayo kabisa,ni bomu litakalowagawa watanzania.

Akumbuke kuwa katiba pendekezwa;

  1. Ilipingwa vikali na uongozi wa dini ya kiislamu, jambo hili liliwaunganisha waislamu wote
  2. Ilipingwa vikali na viongozi wa dini ya kikristo,jambo hili liliwaunganisha wakristo wote
  3. Katiba pendekezwa inapingwa na takriban wasomi wote
  4. Wafanyakazi waliipinga katiba pendekezwa waziwazi bila woga, hasa walimu
  5. Vyama vya upinzani karibu vyote viliikataa katiba pendekezwa,hata vile vilivyounga mkono baadaye viligeuka
  6. Wanafunzi wa vyuo na sekondari waliunga mkono rasimu ya Warioba
  7. Kukataliwa kwa rasimu ya Warioba kumepelekea CCM kuchukiwa sana Zanzibar
  8. CCM ilichukiwa sana bara, imani kwa CCM ililejea pale Polepole alipotangaza kuwa amehakikishiwa na Magufuli kwamba akiingia madarakani atairudisha rasimu ya Warioba
  9. NGO ziliipinga katiba pendekezwa waziwazi bila woga wala mawaa
  10. Waandishi wa habari waliweka tofauti zao kando na kuitetea rasimu ya Warioba kwa nguvu zote n.k

Nimkumbushe tu Dr Mwakyembe, watanzania hawachelewi kubadilika, Vita alivyovianzisha Dr Magufuli vinahitaji uungwaji mkono wa wananchi wote.Leo kila mtu anampenda rais. Lakini, kazi yote aliyofanya rais Dr Magufuli itaonekana si kitu, kama mchakato wa katiba iliyopitishwa kitapeli utaanza tena.Ukitaka umoja wa taifa hili uendelee kuwepo,na watu waendelee kuiunga mkono CCM basi rudisha rasimu ya Warioba,vinginevyo nakushauri achana kabisa na kufufua mchakato wa katiba.Kujaribu kuitetea katiba pendekezwa ni sawa na kuchezea moto karibu na petroli.ACHA,ACHA KABISA DR MWAKYEMBE KUTETEA KATIBA PENDEKEZWA,ACHA KAMA ULIVYOACHA KUNYONYA, hilo ni bomu kwa utawala mujaarabu wa Dr Magufuli,nakusihi achana na katiba pendekezwa rudi kwenye rasimu ya Warioba.Maneno yangu haya ni hakika,kweli na thabiti, ni suala la muda tu,akipuuzia matokeo tutayaona. Alamski!

Kwa hii template mpya ya Jamii forums sijui tunachangia vipi< which is a problem hapa kwa wahusika, wanafikiri tunakuja humu kwa ajili ya urembo wa page, no tunafuata content sasa msitusumbue na complication za kubadilisha muonekano kila siku, anyway sikubaliani kabisa na mtoa hoja kwamba eti Mwakyembe anaweza kujiuzulu, hana ubavu huo na hathubutu ndio maana kangangania pamoja na kujua wazi kuwa awtu wa kyela hawamtaki hata kidogo. Ni mzandiki na hicho kiburi chake alipewa tu nguvu na watanzania wakati akimkaanga Lowassa kwa sababu wananchi tulitaka iwe vile.
 
Serikali ya mh. Magufuli inaweza kuongeza umaarufu wake au ikaanza kuyumba kutokana na maamuzi ya katiba mpya. Busara inahitajika kabla ya kufanya maamuzi
 
JK alipoteza umaarufu, CCM ikachukiwa hadi leo. Mawaziri waliosimamia baadhi wamepoteza ubunge
Mwakyembe akumbuke kuwa hawezi kuanzia pale katiba mpya ilipoishia kwasababu za kisheria

Agenda nzima ya Magufuli itapotea haraka sana hili suala lisipoangaliwa
 
Katiba pendekezwa ya ccm ipo palepale,ila watadili nayo awamu ya pili ya miaka 5 ya mwisho ya Magufuli ili wamtengenezee njia Rais wa awamu ya 6.
 
Back
Top Bottom