Ushauri wa bure kwa CHADEMA

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Umefika wakati sasa chama kikubwa kama CDM kuwa na vitu vyake binafsi muhimu vitakavyo iweka CDM juu zaidi ya sasa,

Najaribu kutoa ushauri kwa CDM kuwa wasione hatari kwa wao kuanzisha CDM TV na CDM RADIO ambavyo vitakuwa vikifanya kazi moja tu ya kusambaza na kuitangza CDM Mijini na Vijijini,

Hii itasaidia CDM kukwepa Mgomo uliopo sasa wa vyombo vya habari kama TV wa kutotangaza hata hotuba za viongozi wa chama pindi wanapokuwa ktk mikutano yao

kwa kuwa CDM sasa inawanachama na wakeleketwa wengi kuna umuhimu wa kuwa na media hizo ambazo mwisho wa siku zitakuwa zikibeba ujumbe muhimu kwa wana chadema na hata masio wanachadema

Ni ushauri tu kwa manufaa ya CDM na watu wake
nawasilisha

41784_148053981881068_35_n.jpg
 
Niushauri mzuri mpiganaji mwenzangu,nilishaongea na Mkt MOWE kuhusu ilo akasema watalifanyia kazi.Chadema viva.........
 
bonge la ushauri aisee. CDM mmesikia? Fanyeni mambo
vyombo vya habari siku zote huwa vinatangaza habari zenye mshiko sasa kama.habari.zenu.muda.wote ni kueneza uongo hata mkianzisha hiyo.tv ama radio mtakasa wasilikilizaji jaribuni kubuni mkakati.mwingine la sivyo uanzishaji.wa tv ama radio itakula.kwenu
 
Ushauri mzuri sana. Jana nimeangalia chanel kadhaa, sikuona hata moja ikionesha kinachoendelea rukwa.
 
Umefika wakati sasa chama kikubwa kama CDM kuwa na vitu vyake binafsi muhimu vitakavyo iweka CDM juu zaidi ya sasa,

Najaribu kutoa ushauri kwa CDM kuwa wasione hatari kwa wao kuanzisha CDM TV na CDM RADIO ambavyo vitakuwa vikifanya kazi moja tu ya kusambaza na kuitangza CDM Mijini na Vijijini,

Hii itasaidia CDM kukwepa Mgomo uliopo sasa wa vyombo vya habari kama TV wa kutotangaza hata hotuba za viongozi wa chama pindi wanapokuwa ktk mikutano yao

kwa kuwa CDM sasa inawanachama na wakeleketwa wengi kuna umuhimu wa kuwa na media hizo ambazo mwisho wa siku zitakuwa zikibeba ujumbe muhimu kwa wana chadema na hata masio wanachadema

Ni ushauri tu kwa manufaa ya CDM na watu wake
nawasilisha

41784_148053981881068_35_n.jpg

Mdau hapo kwenye red nimekubali kabisa...maana kwa siku za karibuni nashangaa sana kuona kwamba mikutano ya CDM inayofanyika mikoani haionyeshwi! Inanitia shaka kama kweli hakuna mkono wenye MAGAMBA katika hili!
 
Labda hakuna waandishi wa habari huko Rukwa na sumbawanga maana CCM huwa inawachukua waandishi enaenda nao huko.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom