Hakuna asiyejua kuwa CCM imekuwa ikiingiza mkono wake katika maamuzi ya mahakama hasa katika kesi za kupinga matokeo ya Ubunge. Sasa ushauri ninaotaka kuwapa ni kuwa ni bora mwingilie kwa kuomba kila mlikopinga matokeo mshindwe kesi ili kuhepuka uchaguzi mdogo. Hata kule Arusha muombe rufaa ya CDM ipite na Kamanda G.L aendelee na ubunge wake. Kwanini natoa ushauri huu?
Ukweli ni kuwa kila uchaguzi mdogo utakaofanyika CCM itashindwa tu na huu ni ukweli usiopingika. Na katika trend ya kushindwa katika chaguzi ndogo mjue ndiyo Chama kitazidi kuporomoka na kujenga mazingira ya kushindwa 2015. Someni alama za nyakati na kutumia busara ndogo. Hii haiitaji shule kutambua. Makamanda wako juu kila mtakapoweka mguu ni mweleka. Mimi siyo mtabiri wa nyota bali busara ya kawaida inanionyesha hivyo.
Ukweli ni kuwa kila uchaguzi mdogo utakaofanyika CCM itashindwa tu na huu ni ukweli usiopingika. Na katika trend ya kushindwa katika chaguzi ndogo mjue ndiyo Chama kitazidi kuporomoka na kujenga mazingira ya kushindwa 2015. Someni alama za nyakati na kutumia busara ndogo. Hii haiitaji shule kutambua. Makamanda wako juu kila mtakapoweka mguu ni mweleka. Mimi siyo mtabiri wa nyota bali busara ya kawaida inanionyesha hivyo.