ushauri nasaha unahitajika.

Sasa ninaona tatizo.

Shem, opsss kaka mbu huyu shemejio anasumbuliwa na guilty conscious kwani anajichukulia kuwa ndiye chanzo cha wao kukosa watoto (Ile abortion ya ujanani) sasa kung'ang'ania kwake ni denial status hataki kukubaliana na ukweli (na kweli si rahisi kukubali kuwa eyey ndo chanzo) so ana amini iko siku atafanikiwa na ku-prove wrong walimwengu. Isitoshe pengine alikwishaapa kwa mumewe kuwa yeye ujanani alikuwa 'mtoto mzuri' sasa report ya dr imetoa visivyo so anatamani kuprove wrong madr. ili amhakikishie Mr. kuwa kweli yeye alikuwa mtulivu na madr. ndoi waliokosea.

Kwa hali hii Kaka ni ngumu kusolve unless mdada akubali kuwa hata fanikiwa na mume amsaidie kumpa confidence kuwa yameshamwagika hayazoleki but amwonyeshe upendo na kumhakikishia atampenda despite all.

...kwa muono wangu, nadhani huyo bi mdogo hataridhika mpaka Bw'mkubwa roho itapomtoka... Iweje baada ya kutendewa yote hayo yeye bado kang'ang'ana tuuuu apate mtoto wake wa kumzaa mwenyewe?

Ingekuwa Bi mdogo huyo hajawahi kubeba mimba kweli, lakini ripoti za kidakitari tayari zinaonyesha alipata mimba, ikakwama kwenye mirija (ectopic) na ndio ikawa chanzo cha upasuaji ule na kuondoa mrija, ...

Bw'mkubwa yeye keshaona ya kale hayanuki, anampenda mkewe na anamchukulia kama mzazi mwenzake kwa hao mabinti zao, Bi mdogo yeye aahhh... Hataki, hataki, hataki,... anataka mimba yake, na asukume mtoto wake.

Mw'j1, shukran sana. Tuwasubiri na wengine watavyochangia hiyo "Guilty conscious" ya bi mdogo huyo itatibikaje..nawe utuletee tafakari pana zaidi kutatua/kupunguza usongo huo.
 
well,
kwangu mimi the whole situation looks UNBEARABLE!

...shukran Geoff, lakini fafanua basi kidogo bana. Huwezi kwenda kwa dakitari ukamwambia unaumwa kichwa halafu yeye akakupa panadol bila kukuuliza kama unahoma, unaharisha au kutapika, umejigonga nk...
 
Sasa ninaona tatizo.

Shem, opsss kaka mbu huyu shemejio anasumbuliwa na guilty conscious kwani anajichukulia kuwa ndiye chanzo cha wao kukosa watoto (Ile abortion ya ujanani) sasa kung'ang'ania kwake ni denial status hataki kukubaliana na ukweli (na kweli si rahisi kukubali kuwa eyey ndo chanzo) so ana amini iko siku atafanikiwa na ku-prove wrong walimwengu. Isitoshe pengine alikwishaapa kwa mumewe kuwa yeye ujanani alikuwa 'mtoto mzuri' sasa report ya dr imetoa visivyo so anatamani kuprove wrong madr. ili amhakikishie Mr. kuwa kweli yeye alikuwa mtulivu na madr. ndoi waliokosea.

Kwa hali hii Kaka ni ngumu kusolve unless mdada akubali kuwa hata fanikiwa na mume amsaidie kumpa confidence kuwa yameshamwagika hayazoleki but amwonyeshe upendo na kumhakikishia atampenda despite all.

nakuunga mkono Mwanajamii one

pia hilo suala la watoto wakambo aliowalea toka utotoni kuhamia kwa mama yao ukubwani lingeangaliwa kama inawezekana, kujibizana nao kunaweza kuwa kunatokana na masuala wanayodiscuss na mama yao mzazi kuhusu bi mdogo...
hiyo inawezekana kabisa wanawake wanapokaa pamoja
 
She should say to herself, believe and agree/admit that what's done is done. She should let it go and decide that what she is going to do from today on is what matters now........... She should do it before its too late coz when the lovely and understanding hubby's fed up, she gonna loose everything and end up being totally frustrated.

Wengine tunatafuta waume waelewa wa hivyo hatupati....... Dada yangu alipata shida na mumewe kisa mume alikuwa anataka dada abebe mimba ya pili six months after kujifungua mtoto wa kwanza tena kwa operation!! Ye anachezea shilingi ******!
 
...Tatu baada ya wao wawili kukubaliana waitishe kikao cha pande zote mbili na kuwaeleza situation yao na MAAMUZI yao kama wanandoa. Kisha watoe MSIMAMO wao nahisi hata hao wapiga kelele watafunga vinywa!

Mbona kuna wengi tu hawana watoto na karama na baraka zao wapewazo na mwenyezi MUNGU wanazitumia kusaidia mayatima na wasiojiweza?!

...ushauri nasaha,

naona kweli kuna haja ya huyo Bwanamkubwa kuitisha kikao hicho haraka iwezekanavyo na kutoa msimamo huo kwa pande zote husika.

Nadhani baada ya hapo, wazazi wa huyo bi mdogo hususan mama yake na mama zake wadogo wataacha kumbugudhi binti yao na yeye (bi mdogo) na 'false hopes' zake...
 
...shukran Shishi,

kama nilivyosema awali, huyo bi mdogo alificha 'maradhi' yake mwanzoni, ndio maana nikasema aliutumia vibaya ujana wake, na Mw' Mungu hajapenda bado kumpatia mtoto...kwanini nasema hivi;

Bi mdogo katika siku za awali za ndoa tuseme miaka miwili na ushee alikataa ushauri wa mumewe kwenda kufanyiwa utaalamu wa madakitari. Badala yake, alitumia sana mitishamba pamoja na huduma za 'watafiti' wa jadi kwa kudhani labda kafungwa kizazi au labda miti shamba ingemsaidia.

By the time Bi mdogo ame exhaust means zote za kienyeji kutafuta mtoto, ndipo Bw Mkubwa alipompeleka mkewe kwa madakitari bingwa kujua kulikoni, na huko ndiko alipoambiwa mrija upande mmoja ulitolewa wkt wa abortion (ujanani), na upande wa pili umeziba, na hautaweza kuzibulika!

Pamoja na hayo, Bw'mkubwa alikubali IVF treatment ya kwanza, ikafeli... IVF treatment ya pili, ikafeli,... sasa Bw'mkubwa anasema imetosha. Mamilioni kadhaa yamepotea, Mw'Mungu hajapenda. Bi mdogo hataki...!

Bw'mkubwa keshampa rukhsa, kama anataka mtoto kwa hali yeyote iliyo, basi rukhsa waachane akatafute atayeendelea kutumia mamilioni kwa IVF treatment, Bi mdogo hataki...!

Si karaha hiyo? :D


duh karaha kweli... sasa basi anakandamizia ya nini kama daktari ameshasema kuwa haiwezekani... tena bahati yake huyo bwana hajamtosa bado anampenda..mmmh makubwa haya!
 
Mkuu Mbu samahani kwa kuchelewa kukujibu kuhusu hili. Nilikuwa sijaingia hapa kwa muda wa siku mbili sasa, ndiyo nimeiona PM yako sasa hivi baada ya kuingia hapa. Ngoja nilitafakari hili kwa kina halafu nami nitoe mchango wangu.
 
mbona unasema mke tu nyie ndio one sided people mbona hata wanaume kibao wako infertile............nasikia kaka wako jako alikuwa hivyo na alifanya adoption na nadhani ni jambo zuri tu...............
 
mbona unasema mke tu nyie ndio one sided people mbona hata wanaume kibao wako infertile............nasikia kaka wako jako alikuwa hivyo na alifanya adoption na nadhani ni jambo zuri tu...............

Jile umeisoma mada vizuri? Hii mbona amespecify na si kwamba anageneralize. Ameomba tumsaidie mtu wake wa karibu ambaye tatizo lake specific ni hili la mkewe kutokuwa na uwezo wa kupata mtoto.

Unawashaurije wote wawili yaani mke na mume wahusika!
 
Mkuu Mbu hizi ndiyo ndoa zetu za Kitanzania na hata za Kiafrika huingiliwa mno na wazazi, ndugu na jamaa na hata marafiki wa karibu wa pande zote mbili na hatimaye kuziathiri ndoa hizo na hata kuweza kuvunjika.

Wenzetu wazungu kwenye situation kama hii (Mke na Mume) wanaweza hata kwenda mahakamani kuwazuia hao mama wa binti kuwatembelea, kuwapigia simu na hata kukutana nao kwa lolote lile au kwa maneno mengine kuvunja uhusiano nao ili kulinda ndoa yao. Kwetu hili bado halijaingia kabisa.

Hichi kikao ulichoshauri kiitishwe ni muhimu ili mke na mume watoe msimamo wao kuhusu bughudha za mama wa binti na wao wenyewe wanataka nini kwenye hili suala la kuwa na mtoto au la. Nafikiri baada ya kikao hicho itapatikana amani ili wana ndoa waendelee na ndoa yao au waachane ili bi mdogo akajaribu bahati yake ya kupata mtoto kwingine.

Imeshatokea mara nyingi tu hata wale ambao waliambiwa na madaktari kwamba hawawezi kushika mimba kabisa au hata wakishika mimba zitatoka baada ya miezi michache wakashika mimba na kujifungua mtoto mwenye afya nzuri tu, hivyo huyu binti naye anaweza kubahatika na kushika mimba na kujaliwa naye kuwa na mtoto wake mwenye afya nzuri.
 
Huyu bibiye ashukuru kapata mwanaume mzuri, anayempenda kiukweli. Angekuwa mwanaume mwingine angepata misuko misuko kwenye ndoa yake baada ya kubainika alitolewa fallopian tube moja na nyingine imeziba baada ya kufanya abortion enzi za usichana wake.
Jambo la msingi hapa yeye atulie tu, ilimradi jamaa karidhika na yeye japo hana uzazi ashukuru kwa hilo. Vile vile jambo lingine atubu kwa muumba wake kwa dhambi aliyofanya ya abortion, Mungu wetu wa rehema anaweza kumsamehe na kujaaliwa tena kupata mtoto kwa miiujiza.
 
...shukran kwa wote mliochangia, ama kwa hakika nami nimejifunza mengi pia kutokana na michango yenu. Nitafikisha busara zenu kwa wahusika wakuu kwenye sakata hili.
 
Mbu!

Kuna namna tofauti unavyoweza kusaidia;
cha kwanza ni kujua state ya huyo dada, she seems to be proud and a hero of herself, thats why she wants her baby plus trying to cover up her past through denials and competition. Mimi ningeshauri apate psychiatrists wamsaidie kwanza kumuweka sawa kuhusu elimu ya uzazi na umuhimu wa maandalizi bora ya uzazi na afya yake. She wont get pregnancy kama ana stress

Cha pili ni kuhusu yeye kuwa mke mdogo, hata wewe ungekuwa mwanamke, ungetamani mazao yako mwenyewe, hasa ukizingatia laiyetangulia alipata watoto, so there is a social pressure on her; cha maana ni kumsaidia tu

Tatu ni kuhusu stte ya huyo jamaa, lazima akumbuke kwamba kutosheka kwake siyo kipimo cha mahitaji ya familia, he needs to support his wife

Nne ni kuhusu IVF, kaifanyia wapi?? mimi ningeshauri aende india kuna wataalam wazuri sana!!

Sasa twende mbele

  • Tumsaidie jamaa ajaribu IVF ya nje ya nchi kwani lazima mama aridhike na all options available kabla ya kukubali matokeo
  • pia kuna baadhi ya watu walitoka nje kwa muda kupunguza stress na wakafanikiwa
  • Tukumbuke kwamba kitendo cha bi mdogo kwenda kwenye mitishamba na mambo kama hayo ni hisia za kuchezewa na bi mkubwa, kwa hiyo tujaribu kumsaidia apunguze presha na imani potofu, ili afuate maisha yaliyonyooka. cha maana hapa ni kumrejea muumba
  • Bwanamkubwa atake askitake lazima amsaidie huyu dada kumaliza available options, kwasababu sometimes huyu dada may go overboard just to prove that she can not conceive, hapo ndio UKIMWI nao hupata nafasi
  • Mwisho kabisa ni kuondoa hayo mawazo ya dada kuharibu ujanani kwani si lazima iwe chanzo cha kutopata mtoto, kuna baadhi ya matatizo yanaletwa na sisi wanaume ndani ya ndoa na kuharibu uzazi
 
the_promise.jpg

...kwa mke na Mume, ambaye (mke) aliyemuoa ni Infertile, (mirija na kizazi kimeharibika).

BTW; Adoption is out of question!

Mkuu naomba ushare hii kwenye Infertility and Adoption Support Group, ni social group mpya tunahitaji hizi experience na michango ya wana JF ili tuwe na mahali pa kuzungumzia haya mambo na kusaidiana.

Nitaacha comment zangu kwa huyu dada kwenye Infertility and Adoption Support Group kwa faida ya wengine.
 
Mkuu naomba ushare hii kwenye Infertility and Adoption Support Group, ni social group mpya tunahitaji hizi experience na michango ya wana JF ili tuwe na mahali pa kuzungumzia haya mambo na kusaidiana.

Nitaacha comment zangu kwa huyu dada kwenye Infertility and Adoption Support Group kwa faida ya wengine.

Asa MNDEE mbona hujatupa mlango wa hiyo sehemu? atashareje hii experiece huko?
 
Mbu!

Kuna namna tofauti unavyoweza kusaidia;
cha kwanza ni kujua state ya huyo dada, she seems to be proud and a hero of herself, thats why she wants her baby plus trying to cover up her past through denials and competition. Mimi ningeshauri apate psychiatrists wamsaidie kwanza kumuweka sawa kuhusu elimu ya uzazi na umuhimu wa maandalizi bora ya uzazi na afya yake. She wont get pregnancy kama ana stress

Cha pili ni kuhusu yeye kuwa mke mdogo, hata wewe ungekuwa mwanamke, ungetamani mazao yako mwenyewe, hasa ukizingatia laiyetangulia alipata watoto, so there is a social pressure on her; cha maana ni kumsaidia tu

Tatu ni kuhusu stte ya huyo jamaa, lazima akumbuke kwamba kutosheka kwake siyo kipimo cha mahitaji ya familia, he needs to support his wife

Nne ni kuhusu IVF, kaifanyia wapi?? mimi ningeshauri aende india kuna wataalam wazuri sana!!

Sasa twende mbele

  • Tumsaidie jamaa ajaribu IVF ya nje ya nchi kwani lazima mama aridhike na all options available kabla ya kukubali matokeo
  • pia kuna baadhi ya watu walitoka nje kwa muda kupunguza stress na wakafanikiwa
  • Tukumbuke kwamba kitendo cha bi mdogo kwenda kwenye mitishamba na mambo kama hayo ni hisia za kuchezewa na bi mkubwa, kwa hiyo tujaribu kumsaidia apunguze presha na imani potofu, ili afuate maisha yaliyonyooka. cha maana hapa ni kumrejea muumba
  • Bwanamkubwa atake askitake lazima amsaidie huyu dada kumaliza available options, kwasababu sometimes huyu dada may go overboard just to prove that she can not conceive, hapo ndio UKIMWI nao hupata nafasi
  • Mwisho kabisa ni kuondoa hayo mawazo ya dada kuharibu ujanani kwani si lazima iwe chanzo cha kutopata mtoto, kuna baadhi ya matatizo yanaletwa na sisi wanaume ndani ya ndoa na kuharibu uzazi

...Mkuu MTM, haya mambo uliyoyaongea ndio niliyoambiwa na huyo bwanamkubwa hivi karibuni. Yaani, kwa hakika huo ndio wasiwasi wake kwamba huenda baadhi ya watu watasema yeye katosheka kwakuwa tayari ana mabinti zake wawili, ingawa hapa haijalishi watoto ni wa jinsia gani. Mtoto ni mtoto tu.

Lakini vile vile, aliniambia umri ni factor vile vile inayomkwaza kuendelea na mambo haya ya IVF. Anasema haonelei ni busara age gap ambayo tayari itakuwepo baina ya last born wake wa sasa na huyo mtoto atayezaliwa...i.e more than 12yrs (apart).

Pili, Bwana mkubwa tayari yumo kwenye hizi mid-ages za Kitanzania, (35-45yrs), anafikiria kuchelewa kuzaa huyu bi mdogo huenda kukawavurugia maisha yao huko kwenye fainali za uzeeni... imagine Mtoto bado atakuwa anahitaji gharama za elimu nk wakati huo huyu Mtu mzima tayari kikongwe kwa life span ya Tz...

Mwisho, wasiwasi wake mkubwa kwanini hataki IVF nyingine, ni kwamba iwapo bi mdogo yuko sooo obsessed kumzalia Bwana mkubwa mrithi wake (mtoto wa kiume), ndio kusema wakigonga mwamba na kuzaa wa kike, kilio kitakuwa oooh, tujaribu tena,...BTW, mbona kwa Ex-wife mlizaa wawili... almuradi kutaka ku prove another point, ... sijui umeelewa?

Nadhani haya mambo ni kwa pande zote mbili uzito wake, au?

ps. Note... matibabu Mumbai, na Uingereza tayari yeshafanyika.
 
Duh... Hapo sasa naona issue imekuwa more complicated but interesting; nijuavyo mimi, one has to give way! either mwanamke akubali yaishe au bwa'mkubwa, its like a tug of war hapo!!!

Ila tufahamu kwamba wanawake ni watu wa misimamo, akitaka kitu chake ni lazima apate au ahakikishe hakiwezekani, sasa asije akafikia kutafuta alternative means kama kutembea nje ya ndoa ili kuhakikisha tu kwamba yeye ndio mwenye matatizo

The only way forward in counselling and keeping their relationship active and busy! travels, investiments, education etc...
 
Mbu mm naona kama lengo la jamaa kuwa na watoto basi wakubaliana atafute mwanamke mwingine awe wa 2 awe anajimegea kupata watoto na raha ya familia ni watoto. Sasa tatizo la hawa wanawake infertile iwa wanakuwa wana wivu balaa.
 
Duh... Hapo sasa naona issue imekuwa more complicated but interesting; nijuavyo mimi, one has to give way! either mwanamke akubali yaishe au bwa'mkubwa, its like a tug of war hapo!!!

Ila tufahamu kwamba wanawake ni watu wa misimamo, akitaka kitu chake ni lazima apate au ahakikishe hakiwezekani, sasa asije akafikia kutafuta alternative means kama kutembea nje ya ndoa ili kuhakikisha tu kwamba yeye ndio mwenye matatizo

The only way forward in counselling and keeping their relationship active and busy! travels, investiments, education etc...

...MTM, it is complicated indeed...lakini kwa uzoefu wangu nimejifunza pia kwamba ukiyaendekeza sana haya majambo matokeo yake mtakwama hapo kwenye tope.

Inafikia wakati inabidi papigwe msitari chini kama ilivyoshauriwa hapo awali...kuitisha kikao cha wazazi pande mbili na Mume akiwa ndiye mwenye mamlaka ya nyumba kutoa msimamo wa mwisho. Kinyume na hapo mvutano hautokwisha kwani kila mtu atakuwa anavutia kwake.

Hilo la Bi mdogo kuanza kutembea nje ilhali tayari anajua tatizo mwilini ni lake haitakuwa na maana yeyote isipokuwa yale yale ya kujidanganya nafsi yake kwamba labda akifanya hili au akifanya lile atafanikiwa...(UJINGA)

Kama nilivyosema awali,... There is a tiny hope Bi mdogo ku conceive tena kwa hizo njia za IVF lakini kwakuwa umri wao tayari ni mid-ages ...huenda itakuja letesha Birth defects/complications ambazo Bwanamkubwa huyo kesha note na keshasema 'jua limekuchwa', wamshukuru mungu.

Vilevile, Bwanamkubwa huyo keshasema iwapo mke bado ana hamu ya uzazi, basi ruksa kuolewa na mtu mwingine mwenye hamu na mtoto mwingine. Yeye (Bwanamkubwa) keshajiamulia basi, juhudi zote zimetosha.

... Sasa tatizo la hawa wanawake infertile iwa wanakuwa wana wivu balaa.

Fidel80, hilo tatizo la wivu (wakijinga) hata mimi nishaliona... ndio maana nakwambia hata akizalishwa mmoja, huenda akataka na wa pili ili ngoma iwe draw na Ex-wife wa huyu mheshimiwa.

Maisha haya, :D... Mheshimiwa asipojiangalia atakuja lea wajukuu badala ya watoto,...haipendezi mwanaume kesha retire ilhali bado anahangaikia ada za shule za watoto... ndio kuwatwika mzigo mabinti zake (wakubwa) bureee...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom